Hebu Ngoja! Erasto Nyoni Aliingia Uwanjani huku akiwa anavaa Hereni?

demigod

JF-Expert Member
Joined
Jan 2, 2015
Posts
8,292
Reaction score
15,250
Aisee Mimi sijaliona vyema hili tukio.

Nasikia huyu Bench warmer aliingizwa dakika za 70 na akaonekana anaingia huku anavaa hereni.

Yaani Timu yako iko nyumba ya bao moja unapata muda wa kujivika hereni?

Tena ukizingatia una miaka 34 na zaidi.

Basi huyu jamaa hafai hata kusajiliwa DTB Kama ni kweli.
 
Legend alizivaa kutoka kambini! Wakati wa ukaguzi ili aingie, akqazivua na kuzificha mkononi! Alipoingia tu, akaanza tena kuziweka masikioni!

Hakika lilikuwa ni tukio la kushangaza sana. Mchezaji mkongwe kama yeye, anaingia uwanjani na kupoteza muda kuvaa hereni, badala ya kuipambania timu! Mpaka mwamuzi anamtoa nje akazivue! Lilikuwa ni tukio la aibu sana kwake
 
Yote hayo ni kweli ,Mimi nimeshuhudia
 
Nililiona lile tukio na japo mi yanga ila alinikera sana hasa pale refa alipomtoa akazitoe maana sijui zilikua hazikai ila ye anakomaa nazo tu hazingatii situstion kwamba wako nyuma ya muda na matokea
Mchezaji haruhusiwi kucheza akiwa kavaa hereni wala cheni, ndio maana alizificha wakati anaingia akavalia uwanjani,
 
Nyoni hereni za demu wake zilimsumbua kukaa masikioni akawa anahangaika kuvaa huku Yanga wanagongeana pasi refa akamwambia njoo nikuvishe vizuri alipomkaribia refa akamwambia acha uzwazwa kwenda kule nje ukavae vizuri upendeze!
 
Mchezaji haruhusiwi kucheza akiwa kavaa hereni wala cheni, ndio maana alizificha wakati anaingia akavalia uwanjani,
So what was the point..alikua halijui hili??
 
Uzee wote ule bado unavaa hereni? Uwenda ni ndumba zao alibeba na sisi hatujui
Yaani mchawi wakati wote utamjua tu. Hakosi kutajataja habari za kichawi maana anadhani kila mahali wanamchawia tu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…