Hebu Sikieni Furaha Yangu


hapo nimekuelewa mpenzi.
Remain as good as you are.
 

Mimi ni mkristo; lakini napata taabu sana mtu anaposema tu "namsubiri Mungu anipe" bila kutumia akili yake na uwezo/utashi aliopewa na Mungu kutafuta kile anachokihitaji, kwa mfano kutafuta mke/mme. Nadhani cha msingi ni kuomba Mungu akusaidie akili/hekima/utashi wa kupata kitu chema na si kusema "Mungu ataleta tu mimi nasuburi siku ifike!"

Sasa Miss Judith hebu twambie kwa mujibu wa imani yako ni vipi Mungu atakuletea mme, au utajuwaje kuwa huyu ndie katoka kwa Mungu!?

Amini na kwambia, hakuna ndoa smooth kwa 100%(Yesu alituambia, duniani mnayo dhiki jepeni moyo; tena imeandikwa, majaribu ni mtaji).

Usije ukaangamia kwa kukosa maarifa.

Ok tunashukuru kwa ulichofanya kwa hao wanandoa, wafikie lengo la kurudiana na si kupeana mimba tu.
 
By the way, tunashukuru kuwa na watu kama nyie hapa jamvini maana mnatukumbusha injili, sio vile tunajadili mambo ya ulimwengu tu bila hata kumtaja Mungu.

Wapi ndugu Makoyo naye alikuwa anasaidia mambo ya injili hapa!?
 
hapana kumbuka talaka si mpango wa Mungu na mie wakati ule nilikuwa nasoma, so nilikuwa sihitaji kuingia kwenye masuala ya ndoa na kusema kweli ile ilikuwa ni njia ya "kidiplomasia" tu ya kumkataa, lakini Mungu akajibu maombi yetu.

Judith,

Nimependa sana hadithi yako. Hapo umejaribu kutumia akili badala ya kuingia kwenye mambo kichwa kichwa! Mara nyingi neno moja tu, "nakupenda au I love you" linawalevya watu zaidi ya zile pombe za Kirusi!

Laitu wengi wetu tungekuwa tunajipa nafasi na kujifunga gavana kidogo, watu wenye vidonda wangekuwa wachache!
 
Najaribu kupata picha nini kilikuwa kinasonga mawazoni mwa huyu jamaa punde ulipomweleza hayo....... Unajua nini? Hukuwa umempenda nafikiri au hakuwa moyoni mwako kiviiiile in short hukuwahi kumfikiria kama a prospect husband ndo mana ilikuwa rahisi sana kwako kumwambia afanye hayo.
 

mpendwa chapa nalo jr, nashukuru kwa kunielewa. imeandikwa kuwa mwenye haki wangu ataishi kwa imani, so kwa kuwa umekiri kuwa nawe ni mkristo, nakusihi uendelee kuishi kwa imani.

kumtegemea Mungu sio kuipeleka akili yako likizo. kumbuka hata akili yako ni kipawa cha Mungu. tatizo watu hudhani kwamba wakiwa waangalifu sana na vigezo ndo watapata wenzi wa maisha wazuri na wanaomatch nao. lakini hekima ya Mungu si sawa na ya kibinadamu. Mungu aliweza kuyafanya hata mawe yaliyokataliwa na waashi kuwa mawe makuu ya pembeni. kumsubiri Mungu akupe mchumba siyo kufunga macho yako na kungoja uguswe bega kuwa uyu hapa mchumba, hapana. nami naishi katika jamii yangu na nasafiri mara kadhaa kwa mwaka nje ya nchi na napata fursa za kukutana na watu wa jamii mbalimbali. kote huko naweza kupata mwenza wa maisha. muhimu niwe seheme ya jamiii na nichangamane nao huku nikijiweka wazi haiba na tabia yangu yangu bila kificho. hekima ya Mungu ndiyo itakayoniongoza kufanya uamuzi siku hiyo ikifika. kumbuka nimesema kuwa nikiangalia pande zote naona maelfu ya wachumba wazuri walio tayari na huo si uongo, hivyo ashukuriwe Mungu anayetustahilisha haya yote na siye twapaswa kusema amina siku na saa ikifika.

sualal kuwa kila ndoa ina matatizo sio jambo la kuogopa. hata nje ya ndoa nako kuna matatizo, muhimu ujue msaada wako watoka wapi wakati wa matatizo, ukitegemea dunia ndio ikupe msaada, utaangamia vilivile na maarifa yako hayo. jiulize ndoa ngapi zimevurugika na maarifa yaliyopatikana mfano katika ulingo wa beijing? maazimio ya beijing si mabaya, bali kuyafuata bila kumpa Mungu nafasi yake. hapa jamvini watu wanaongelea mambo ya magari, pesa, kazi nzuri, elimu, umbo la mwili, sura, umri nk kama vigezo, wamesahau kuwa hayo ni mambo ya kupita tu, na ukitumia akili peke yake wawezza kutumbukia humo na mwisho ndoa yenye majuto kwani aliyechaguliwa kwa hivyo vigezo naye hutegemea hivyo vigezo viongoze ndoa yake na mwisho vigezo hivyohivyo vitageuka kero na hata kukuvunjia hiyo ndoa yako. tafakari hapo ndugu yangu

By the way, tunashukuru kuwa na watu kama nyie hapa jamvini maana mnatukumbusha injili, sio vile tunajadili mambo ya ulimwengu tu bila hata kumtaja Mungu.

Wapi ndugu Makoyo naye alikuwa anasaidia mambo ya injili hapa!?

nashukuru kwa kunitia moyo, lakini nakuomba nawe uliitie jia la Bwana wakati wote na mahali popote hata hapa JF. nashukuru pia kwa kumtia moyo makoyo, naamini akisoma hii post atafarijika sana. ubarikiwe ndugu
 

mpendwa, ni kweli haikuwa rahisi kukubali mtihani wangu ule, ni kwa vile tu siwezi kuandika kila kitu hapa lakini kweli ilikuwa shida sana hadi nikamhakikishia mara nyingi kuwa akifanya hivyo na akamtukana basi nitamkubali. hata tulipoachana siku ile, aliendelea kunipa feedback ya kila alichokuwa akizungumza na huyo mtalaka wake kwa simu na hata siku walipokutana naye uso kwa uso na kwa pamoja tulipanga amweleze nini saafari nyingine atakapompigia.

mi kwa upande wangu sikuwa na plan ya kuolewa wala kuwa na BF wkati ule na kwa kweli hata kama mkewe angemtukana hatimaye nisingemkubali. ni kwa sababu tu nilimuonea huruma na maisha yale ya talaka na kuamini kuwa Mungu aweza kufanya kitu nyumbani mwake ndio maana nilikwa naendelea kuwa close naye na kwa kweli ni mkarimu sana na tunatoka naye out mara nyingi sana hata sasa. imefikia sasa ananiona kama mdogo wake tu na hata kuniomba mapenzi kwa sasa amepunguza sana
 

ni kweli kabisa ndugu DC, asante na ubarikiwe sana
 

haya mambo ya kwenye tamthilia! hongera kwa kuunganisha tena!
 

Miss Judith je umeshaolewa?....................................hapo kwenye red walikubaliana na wewe umeconfirm kwani u r so happy kuwa wameoana or r u happy kuwa hujaolewa?
 
Miss Judith je umeshaolewa?....................................hapo kwenye red walikubaliana na wewe umeconfirm kwani u r so happy kuwa wameoana or r u happy kuwa hujaolewa?

inaonekana umeanzia mjadala katikati, hilo nimeishajibu, jaribu kufuatilia. thanks though
 
hongera kwa kuepusha misongamano subiri wa kwako utayeandikiwa kila la heri
 

Amen Mpendwa; sasa wapi wewe unahudhuria kati ya watwanga injili wakuu hapa Tz ambao naamini wote wanalitaja Jina la Yesu ila kuna tofauti za hapa na pale; ni kwa Baba Askofu Kakobe, Mtume na Nabii Mwingira, Gamanywa, Makuti kawe, Mtu wa ufufuo pale Ubungo, Mzee wa Upako Lusekelo, Mama mwenye prefix nyingi yaani "Mfanyabiashara, Dk., Mhe Mbunge, Mch.Kiongozi Getrude Lwekatale", Kwa Mnigeria pale Banana, kwa wengine wanaochipukia(maana ni wengi siku hizi) au upo kwa wakongwe wa kulihubiri neno la Kristo yaani RC and the other Protestants!?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…