Sasa wakati tambaza inasambaratishwa kuna wale waliletwa Iyunga technical Mbeya walisafiri kwa treni ya Tazara du kumbe Mbeya nako kulikuwa na watoto wamevurugwa kutoka mbozi Chunya kyela ileje umalila watoto wababe hatari wanakula kile kitu cha moshi vijeba vimejazia muda wote ngumi mkononi vikawa vimeshajua time table ya wale wajanja wa mjini wanaingia na treni jioni ... wakaenda pale Tazara station kuwasubiri ile treni inaingia inapaki wakalakiwa kwa nderemo na vifujo watoto wa iyunga kila begi ya Tambaza ikishuka wanasachi mikate na dikodiko zingine pamba wanatest wanajisevia ukileta uzuri unachanjwa na wembe alafu pale pembeni wale wababe wenyewe wa shule wametulia wamevaa mizura wanakula moshi..... aise ilikuwa patashika kuna watoto wa tambaza walikuwa na roho nyepesi walirudia palepale station.