Umeelezea kifupi sana Kanjunju....kwa miaka mingapi sasa unapata hedhi? kuna mabadiliko yoyote? kama yapo ilikuwaje huko mwanzo tofauti na sasa? Ilianza lini? unapata hedhi kwa jumla ya siku ngapi ukijumlisha hizo 3 unazotoa mabonge? unabadilisha pad mara nagpi kwa siku? zilnaloa damu completely? unapata maumivu makali unapopata hedhi?
Ni maswali muhimu kujua ili kukupa ushauri mzuri...
Generally, hedhi si kawaida kuwa na mabonge ya damu. Mara nyingi mabonge ya damu yanaonyesha kuwa unatoa damu nyingi kupita kawaida kwa hedhi. Damu nyingi inajumuisha pia kutoa kwa siku nyingi (zaidi ya siku 5).
Kama utapenda kuwa na 'privacy' (nakushauri hivyo) ukajibu maswali hayo kwa PM fanya hivyo...nitajitahidi kukupa ushauri unaostahiki.