Metronidazole 400mg
JF-Expert Member
- Aug 25, 2016
- 941
- 2,062
Wengi wetu leo hii ukimwambia unataka Mungu akupe nini atakwambia pesa/utajiri.
Hata ibada nyingi kwenye haya makanisa binafsi ya mitume na manabii maombi makubwa ni Pesa! Mali! Utajiri.
Mfalme Suleiman alipoulizwa na Mungu anataka nini! Mfalme Suleiman akamwomba Mungu ampe hekima.
Hili si jambo dogo hata kidogo! Hakuomba Mali aliomba Hekima.
Mungu alishangazwa mno na hili pengine hakutegemea, akampa hekima aliyoomba lakini zaidi aamuongezea na utajiri mali na ukuu.
Mpaka leo hii hakuna mtu anayefikia utajiri aliokuwa nao mfalme Suleiman.
Lakini Bwana Mungu hakuishia hapo, akaona mali zote hizi na hekima aliyoomba, havitamfaa kitu kama hatapata ridhiko la matamanio ya kimwili.
Akaona amuongezee mvuto na nguvu za kumiliki wake wa ndoa mia saba (700) na Masuria (nyumba ndogo) mia tatu (300).
Acheni Mungu aitwe Mungu akitaka kukupa hukupa vyote, Mia 7 kwa mia 3.
Tafakari matendo ya Mungu kwa hekima kuu.
Hata ibada nyingi kwenye haya makanisa binafsi ya mitume na manabii maombi makubwa ni Pesa! Mali! Utajiri.
Mfalme Suleiman alipoulizwa na Mungu anataka nini! Mfalme Suleiman akamwomba Mungu ampe hekima.
Hili si jambo dogo hata kidogo! Hakuomba Mali aliomba Hekima.
Mungu alishangazwa mno na hili pengine hakutegemea, akampa hekima aliyoomba lakini zaidi aamuongezea na utajiri mali na ukuu.
Mpaka leo hii hakuna mtu anayefikia utajiri aliokuwa nao mfalme Suleiman.
Lakini Bwana Mungu hakuishia hapo, akaona mali zote hizi na hekima aliyoomba, havitamfaa kitu kama hatapata ridhiko la matamanio ya kimwili.
Akaona amuongezee mvuto na nguvu za kumiliki wake wa ndoa mia saba (700) na Masuria (nyumba ndogo) mia tatu (300).
Acheni Mungu aitwe Mungu akitaka kukupa hukupa vyote, Mia 7 kwa mia 3.
Tafakari matendo ya Mungu kwa hekima kuu.