Sisi binadamu ni viumbe wa ajabu sana, wagumu kuelewa, wepesi kusahau. Pia ni wepesi kulaumu mambo yanapokwenda ndivyo sivyo lakini wagumu kupongeza pale mambo yanapoenda vizuri.
Leo nataka niwe tofauti na wengine kwa kutambua mafanikio ya uongozi wa sasa wa TFF chini ya Ndugu Wallace Karia.
Haya ni baadhi ya mafanikio ya uongozi wa sasa wa TFF.
1. Uteuzi wa mchezaji bora wa Afrika mwaka 1994 Emmanuel Amunike kuwa kocha mkuu wa Taifa Stars. Safari yetu ya AFCON ilianzia kwa maamuzi haya ya TFF. Wengi tuliponda sana uteuzi huo lakini sasa wote tunacheka na kufurahi.
2. Kuendesha Ligi kuu TPL bila mdhamini kwa msimu mzima huku mipango ikiendelea kuhakikisha mdhamini anayepatikana ananufaisha klabu shiriki kama zinavyonufaika na TV sponsorship ya Azam TV. Habari chini ya kapeti kuna mazungomzo yanayoendelea na mdhamini kutoka South Africa.
3. Kuwezesha kufanyika kwa mkutano wa FIFA hapa nchini uliohudhuriwa na viongozi wakuu wa soka duniani akiwemo Raisi wa FIFA Giani Infantino na Raisi wa CAF Ahmad Ahmad. Viongozi hao wawili walipata fursa ya kukutana na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa
4. Kuwezesha kurudishwa kwa fedha za maendeleo ya mpira kutoka FIFA zilizositishwa kutokana na matumizi mabaya ya fedha chini ya uongozi uliopita. Kutokana na kuridhishwa na uwazi pamoja na uwendeshaji wa shughuli za TFF chini ya uongozi mpya, FIFA itatoa TZS 11.5 Billion kwa ajili ya maendeleo ya mpira nchini.
5. Kuwezesha Taifa Stars kufuzu AFCON 2019 kwa mara kwanza baada ya miaka 39 ya kutoshiriki mashindano hayo makubwa barani Afrika. Hakika historia itawakumbuka.
6. Kuwezesha Tanzania kuandaa mashindano ya AFCON kwa vijana wenye umri chini ya miaka 17
7. Kujenga taasisi imara, ni dhahiri shahiri kwa sasa TFF kama taasisi ipo stable na imara chini ya uongozi wa Wallace Karia pamoja na changamoto kutoka kwa wale waliojaribu kuleta migogoro hapo kwenye shirikisho. Tunashukuru Jamhuri iliwachukulia hatua wale waliojaribu kuleta migogoro isiyo na manufaa.
Mungu aendelee kuwabariki viongozi wetu wa TFF chini ya Ndugu Wallace Karia
Sent using Jamii Forums mobile app
Leo nataka niwe tofauti na wengine kwa kutambua mafanikio ya uongozi wa sasa wa TFF chini ya Ndugu Wallace Karia.
Haya ni baadhi ya mafanikio ya uongozi wa sasa wa TFF.
1. Uteuzi wa mchezaji bora wa Afrika mwaka 1994 Emmanuel Amunike kuwa kocha mkuu wa Taifa Stars. Safari yetu ya AFCON ilianzia kwa maamuzi haya ya TFF. Wengi tuliponda sana uteuzi huo lakini sasa wote tunacheka na kufurahi.
2. Kuendesha Ligi kuu TPL bila mdhamini kwa msimu mzima huku mipango ikiendelea kuhakikisha mdhamini anayepatikana ananufaisha klabu shiriki kama zinavyonufaika na TV sponsorship ya Azam TV. Habari chini ya kapeti kuna mazungomzo yanayoendelea na mdhamini kutoka South Africa.
3. Kuwezesha kufanyika kwa mkutano wa FIFA hapa nchini uliohudhuriwa na viongozi wakuu wa soka duniani akiwemo Raisi wa FIFA Giani Infantino na Raisi wa CAF Ahmad Ahmad. Viongozi hao wawili walipata fursa ya kukutana na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa
4. Kuwezesha kurudishwa kwa fedha za maendeleo ya mpira kutoka FIFA zilizositishwa kutokana na matumizi mabaya ya fedha chini ya uongozi uliopita. Kutokana na kuridhishwa na uwazi pamoja na uwendeshaji wa shughuli za TFF chini ya uongozi mpya, FIFA itatoa TZS 11.5 Billion kwa ajili ya maendeleo ya mpira nchini.
5. Kuwezesha Taifa Stars kufuzu AFCON 2019 kwa mara kwanza baada ya miaka 39 ya kutoshiriki mashindano hayo makubwa barani Afrika. Hakika historia itawakumbuka.
6. Kuwezesha Tanzania kuandaa mashindano ya AFCON kwa vijana wenye umri chini ya miaka 17
7. Kujenga taasisi imara, ni dhahiri shahiri kwa sasa TFF kama taasisi ipo stable na imara chini ya uongozi wa Wallace Karia pamoja na changamoto kutoka kwa wale waliojaribu kuleta migogoro hapo kwenye shirikisho. Tunashukuru Jamhuri iliwachukulia hatua wale waliojaribu kuleta migogoro isiyo na manufaa.
Mungu aendelee kuwabariki viongozi wetu wa TFF chini ya Ndugu Wallace Karia
Sent using Jamii Forums mobile app