Heko Usalama wa Taifa

Serayamajimbo

Senior Member
Joined
Apr 15, 2009
Posts
191
Reaction score
38
Happiness Katabazi

KATIKA mchakato wa mageuzi ambayo yamefanyika kwenye Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, mfumo wa sheria na siasa za nchi, taasisi za dola zimejikuta zikiwa nyuma wakati vuguvugu la mageuzi likienda mbele.

Moja ya tasisisi zilizokumbwa na fukuto hilo ni Idara ya Usalama wa Taifa (TISS), ambayo hapo awali, yaani chini ya utawala wa Serikali ya Awamu ya Kwanza na ya Pili, ilikuwa ni taasisi ambayo haikutambulika kisheria kutokana na muundo wake kuwa wa siri na wa gizani mno.

Matokeo ya utendaji wa idara hiyo uliiletea sifa ya kuogopwa sana na kuonekana ni chombo cha majungu, chuki na wauaji wa wananchi wenye misimamo tofauti na watawala wa serikali hizo mbili zilizopita zilizoongozwa na hayati Rais Julius Kambarage Nyerere na Rais mstaafu, Ali Hassan Mwinyi.

Maofisa wa Idara ya Usalama wa Taifa wakiwa katika umbile la kiraia ni wanajeshi na; idara hiyo ni chombo nyeti katika uhai wa dola letu.

Ni kweli kiasili, chombo hiki hufanya kazi kwa taratibu za idara zote za usalama wa taifa na kamwe mwanasiasa hawezi kukitumia; hata hivyo mwanasiasa anaweza kumtumia ofisa wa idara hiyo kwa siri kitendo ambacho ni cha ukiukwaji wa maadili.

Nchi inapoingia kwenye matatizo, migogoro ya kisiasa, lawama kubwa huelekezwa kwa taasisi hii kwani ndiyo inayotambua, kubashiri na kutoa ushauri wa nchi inavyoweza kukabiliana na hatari zozote zile za kiusalama na kiulinzi.

Hapa Tanzania, mageuzi ya mwaka 1992 yaliyoanzisha mfumo wa vyama vingi na mabadiliko mengine ya kisheria na Katiba, yalisababisha kuundwa kisheria kwa Idara ya Usalama wa Taifa.

Kutambulika rasmi kisheria hapa nchini kulianza mwaka 1996, baada ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitisha Sheria ya Idara ya Usalama wa Taifa Na.5 ya mwaka 1996 na kutambulika rasmi kwa jina la Tanzania Intelligence and Security Services (TISS), ambapo kwa sasa idara hiyo inaongozwa na Mkurugenzi Mkuu, Rashid Othman.

Cheo hicho cha Mkurugenzi Mkuu ni sawa na Mkuu wa Jeshi la Ulinzi na Kujenga Taifa (CDF), David Mwamunyange, na Mkuu wa Jeshi la Polisi, Inspekta Jenerali Said Mwema.

Kwa mujibu wa sehemu ya nne ya sheria hiyo inayounda (TISS), kazi na mamlaka iliyonayo ni kukusanya habari, kuchunguza na kutathmini habari zote zinazohatarisha usalama wa taifa na hatimaye kuishauri serikali hatua muafaka za kuchukua kwa maslahi ya taifa.

Ni wazi kwamba idara hii imechangia kwa kiasi kukubwa kudhibiti na kuzuia matendo mengi ya kihalifu ambayo yametendeka au yanayotarajia kutendeka kwa kutoa taarifa mapema kwa Jeshi la Polisi na taasisi nyingine husika ambazo mwisho wa siku ndizo zimeshiriki na kufanikisha kushindwa kwa matukio ya kihalifu.

Hivyo hatuna budi kuipongeza TISS kwa kazi nzuri wanayoifanya; haiwezi kuonekana moja kwa moja na wananchi kwa sababu moja ya miiko ya kazi zinazofanywa na idara hii ni siri.

Na idara hii imenyang’anywa mamlaka ya kukamata wahalifu kwani enzi za utawala wa Mwalimu Nyerere idara hii ilikuwa na mamlaka hayo chini ya ‘Detention Order’ yaani sheria ya kumuweka mtu kizuizini.

Kwa muktadha wa majukumu hayo, idara hiyo ilitakiwa ijiunde upya kutoka kwenye giza na usiri ili ifanye kazi kama chombo cha dola chenye majukumu ya kulinda amani, usalama na demokrasia. Kwa vyovyote vile idara hiyo haiwezi kufuta mfumo wa utaratibu wake wa kufanya kazi zake kwa siri kwa kuwa hiyo ndiyo namna pekee inayowezesha kupata taarifa na habari za kiusalama.

Lakini pia katika dola ya kidemokrasia lazima chombo hiki kivae umbile la uwazi katika utendaji kazi wake ili wananchi wakijue, wajue majukumu yake na waweze kushirikiana nacho pale inapobidi.

Kwa vyovyote vile usalama wa taifa unalindwa na kusalitiwa na wananchi ambao ndiyo wenye nchi; hivyo ni bora wakajua masuala mbalimbali yanayowazunguka.

Idara hiyo isipojijengea haiba ya kupendwa na wananchi, na hasa wazalendo, mwisho wa siku itajikuta inashindwa kutekeleza majukumu yake ipasavyo na kwa urahisi zaidi.

Hivi sasa lawama nyingi zinahusu kuibwa au kuporwa kwa rasilimali za nchi kunakodaiwa kufanywa na matapeli kwa kushirikiana na baadhi ya wawekezaji. Idara hii inaelekezewa lawama hizo, kuhujumiwa kwa uchumi wa nchi, kuuzwa kwa mashirika ya umma kwa bei chee na sasa mikataba mibovu mbalimbali ambayo dola imeingia na wawekezaji lazima ielekezwe kwenye idara hii. Kwa vyovyote vile kashfa ya ufisadi wa BoT, EPA na ombwe la viongozi bora lazima shutuma zielekezwe kwenye idara hii.

Kumbe basi wajibu wake si kama ilivyosadikiwa hapo zamani; yaani kuwa kazi kubwa ya maofisa wa idara hii ni kubeba mikoba ya viongozi, kuwatayarishia malazi salama viongozi pindi wanaposafiri, kuwakuwadia mabibi viongozi, kuhesabu vizibo kwenye mabaa, majungu, chuki dhidi ya wananchi na viongozi wao.

Kwa hiyo tunapojikuta leo tuna mgogoro wa kisiasa katika vyama vya siasa vya ushindani vikiwa vimehujumiwa visifanye kazi, makundi yanayohasimiana kuibuka ndani ya CCM, ufisadi wa kupindukia mwaka mmoja kabla ya uchaguzi mkuu kufanyika, ni mambo yanayowaelemea maofisa wetu wa idara yetu ya usalama.

Kwa vyovyote vile mbeba lawama wa mwisho ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Yeye ndiye anamteua Mkurugenzi Mkuu wa idara hiyo. Idara hiyo nyeti isipofanya kazi vizuri rais atayumba, ataboronga na dola kwa ujumla itaonekana ni ya hovyo ndani na nje ya nchi.

Wananchi wanailalamikia dola kwamba inawanyanyasa na kuminya haki zao bila fidia ya kutosha. Hii inatoa tahadhari kwamba malalamiko hayo yanatokana na utendaji usioridhisha wa idara hiyo.

Natoa wito kwa viongozi wa idara hii kuamka na kushika nafasi kikamilifu kwenye kazi hiyo nyeti ya usalama kwa maslahi ya taifa letu bila kuyumbishwa na wanasiasa manyang’au na wachumia tumbo.

Hatujasikia idara hii kukosa uwezo au vitendea kazi; kwa hiyo haya mambo madogo madogo yanayotishia usalama wa nchi, hayawezi kutolewa visingizio kwamba haijawezeshwa.

Hivi sasa nchi yetu imekuwa na uhuru mkubwa zaidi wa kutoa maoni ambapo wananchi wamekuwa wakijadili kashfa mbalimbali hadharani kila zinapoibuka pasi mtu kukamatwa, kuwekwa mbaroni na kuteswa; tunaamini Idara ya Usalama wa Taifa inafanya kazi yake kwa maadili yanayostahili. Kwa hili tunaipa heko.

Nchi nyingine maofisa wa idara kama hii hawajaenda shule vizuri na wala hawajui maadili ya kazi zao.

Watanzania wengi wangeishia kuumia na kuteswa kwenye majumba ya siri yenye giza, nge na kila aina ya mateso. Tunasema haya kwa sababu tunajua yanayoendelea kufanywa na idara kama hii katika nchi nyingi za Afrika.

Mungu Ibariki Tanzania, Mungu ibariki Afrika
 
Muungwana heko kwa lipi walilolifanya hata baada ya sheria kubadilishwa? Unwapongeza kwa kazi wasioifanya wao?
 
Ni suala la Kujifunza tu kutoka kwa wenzetu waliofanikiwa zaidi kwenye nyanja hii. Wenzetu wana mpaka websites. Lakini Idara ya usalama wa Taifa wamehakikisha wanakua nyuma kiteknolojia ili tu kutunza siri.

Unapokuwa msiri saaaana....mwishoni siri hizo hugeuka kuwa habari. Watu watasoma ishara tu na kujua kila kinachoendelea. Njia nzuri na bora kabisa ya kuficha jambo ni kuliweka wazi lile linalostahili kuwa wazi. Waangalie Mossad, wana website na inahabarisha wananchi juu ya masuala mbalimbali, lakini hutakaa ujue siri zao....kwa sababu wanakufanya uamini kama mwananchi wa kawaida kuwa unaweza kutumia Internet ukapata habari zao....upo?

Waangalie FSB, CIA, MI5,CSIS, e.t.c mfumo ni uleule, kuondoa udadisi, kuna mambo wanayaweka wazi na inasaidia kulinda 'siri halisi",.. sasa nyinyi mnachanganya ngozi na utumbo, pua na mapafu, uso na ubongo..whats up??. Acha cha nje kiwe nje ili cha ndani kihifadhiwe.

LASTLY IDARA HII NI KATI YA IDARA AMBAZO HAZINA NAMNA YA KUKWEPA KUFANYA KAZI HALISI WANAYOKUSUDIWA KUFANYA. Asili ya Kazi hiyo, inaifanya kuwa na matokeo makubwa mabaya kama vile mlipuko wa bomu pale linapofanyika jambo kinyume na Makusudi sahihi ya kuwa na chombo hiki. YOU https://jamii.app/JFUserGuide UP IT EXPLODES!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!SHAURI YENU!!!!!!
 
mdogo wangu Happiness ameingizwa katika somo ambalo sidhani kama ana uwelewa nalo wa kutosha. TISS ilivyo sasa ni aibu kwa vyombo vya usalama wa taifa duniani. Believe me I know.
 
mdogo wangu Happiness ameingizwa katika somo ambalo sidhani kama ana uwelewa nalo wa kutosha. TISS ilivyo sasa ni aibu kwa vyombo vya usalama wa taifa duniani. Believe me I know.
Kwa kweli ni chombo muhimu sana, ila kwa sasa wanasiasa kwa njaa zao na kutaka umaarufu wameweza watumia wachache ambao hawana maadili ndani ya chombo hicho kuiyumbisha inchi.

Wakati wa mchonga bwana huwezi mrubuni usalama, walikua wazalendo but now nahisi hawatumii njia muafaka wa kuwapata hawa watu, kwani wengi si wazalendo, ni aibu tupu, ndo maana hali ya usalama wa rai every day inaenda vibaya. We siku hizi raia akitoa ripoti kuna muhalifu askari anaenda mwambia fulani ndo kakutaja. Huu si ubaradhuli kabisa. Shame on them.

Nahisi serikali ijipange hapo kwanza kwa kuwaanisha wote ambao si waaminifu then kuwashughulikia na kutumia njia sahihi za kuwapata wazalendo ikibidi kuwafundisha au kuwakumbusha nn uzalendo.
 
yangu macho, kama kuna mahafisa wa ngazi za juu katika jeshi letu wamejiunga na CIA na TISS wapo sijui wanawachunguza au wameamua kufanya butubutu mpira uwende, sijui kwasababu tz hatuna siri
"yangu macho" lakini pengine wanavuta kasi wanapoamka ngoma mdundo, cha muhimu mfumo wake ungegawanywa katika vikundi vidogo vidogo kwani hata CIA wana IU 1 mpaka 10 na kila kikundi kinamfumo wake wa uwajibikaji. yangu macho pengine wanafanya kazi kwa kificho sana mpaka hatujui kama wapo,
 
INASIKITISHA SANA NA SINA IMAN NA CHOMBO ICHI IKIWA KUMTIA HATIAN ZOMBE WALISHINDWA. Hii nchi ipo hatarini. Hata hvyo ninaiman taifa hili ni taifa kubwa duniani nasiku moja mifumo yote tangu usalama wataifa, majeshi yetu yote ya ulinz na usalama yatakuwa ktk ubora wa kimataifa. Hili ni taifa kubwa na kwa hakika nilazima litimie, wahujumu wa taifa hili makabur yao yatakuwa jehanamu na watanzania kushuhudia vitanz vyao hakika umauti utawapata kama sunami. MUNGU IBARIKI TANZANIA NA WATU WAKE. Amen
 
Happiness You are to shallow, unawapongeza kwa lipi? or you are just propagating for them??????
 
hiki chombo kimepoteza taswira yake kabisa sasa hivi imekuwa ni show mtaani no maadili kabisa kiukweli imeingiliwa kabisa na atuwezi kupata kile tunchotarajia kutoka kwao ona ufisadi,mikataba mibovu, ubinafsishaji, siri zinavuja ovyo, maadili hakuna yani kwishinei kabisa na uzalaendo enzi ya mwl utamjuaje usalama fisadi utamsikia wapi, siri utazipata wapi
 
upuuzi mtupu.......hawastahili pongezi zozote.
 
Mambo mengine ni mazito na wewe Happiness hujui lolote kuhusu usalama na aliyekupa hizo info uweke kwenye gazeti lenu amekudanganya.

Idara ya Usalama wa Taifa tanzania ilikuwa makini enzi za ujamaa leo hakuna kitu pale. Uozo unaouona ktk polisi na jeshini ni uozo huo huo upo idara yetu ya usalama.
 
Uumhh, mwandishi Happiness angeweka bayana yale ambayo yeye anawasifia hawa jamaa au kwa sababu siku hizi hakuna vile vifungo vya nyumbani au kubebwa na kupelekwa kusikojulikana kama tu ukiisema vibaye serikali?
 
mdogo wangu Happiness ameingizwa katika somo ambalo sidhani kama anauwelewa nalo wa kutosha. TISS ilivyo sasa ni aibu kwa vyombo vya usalama wa taifa duniani. Believe me I know.

Mwandishi anashangaza kuandika makala kama hii hasa wakati huu. Huo msukumo sijui ameupata wapi. Labda aliombwa kuwaandikia PR piece itakayowatengenezea taswira chanya katika jamii. Baada ya kuwasikika wakihusika na skandali za EPA, Meremeta, n.k. hadi kumdondosha mama meghji na kumpa PM (mtoto wa mkulima) kigugumizi Bungeni, tunachokiona ni kuwa umuhimu wao sasa umekuwa zaidi katika kusaidia wakuu na maswahiba wao kuhujumu uchumi wa nchi.
 
Hawa jamaa wana mchango wao mkubwa tu kwenye AMANI na UTULIVU tuliyonayo Watanzania. Tunaweza kubishana sana kwa hili. Wakubwa wao tu ndio wamekuwa wakiwaunga mkono hata mafisadi wa wazi kabisa.
 
Kila mtu anao mwono wake katika kutoa sifa pale aliporidhishwa na jambo.

Happiness labda anasifia uwezo wa TISS katika kutunza siri za mienendo michafu ya viongozi na wafanyabiashara wakubwa katika kuhujumu nchi, kutokufatilia mikataba kandamizi na ya kijinga kabisa ambayo maafisa wa serikali wanaisaini kwa niaba ya nchi kwa kutojua au kwa makusudi maalumu.

HEKO anazotoa kama ziko kwa mwelekeo huo, basi hajakosea maana tukiziandika zitafika kurasa mia kadhaa.
 
mimi nadhani labda huyo hapness anazungumzia kwamba sasa hiyo TISS, inatambulika kwa wtu wote sio kama ilivyokuwa zamani ambacho ilikuwa inaonekana ni kitu kama cha kufikirika tu

lakini tukija katika kuipongeza nadhani hapo ni hapana,
KAMA KUNA IDARA AMBAYO INAIANGUSHA HII NCHI NA KURUDISHA MAENDELEO NYUMA BASI ITAKUWA NI HII IDARA, nadhani ndani ya hiyo idara kuna department moja tu ya Siasa, department ya kushughulikia upinzani na mtu yoyote anaeonesha ana misimamo mikali ya kisiasa,
SIDHANI KAMA KUNA KITENGO CHA MAANA KABISA NDANI YA HII IDARA KINACHOSIMAMIA UCHUMI NA MASLAHI YA KWELI YA HILI TAIFA (ISSUE KAMA ZA EPA, RICHMOND, MADINI NA NYINGINEZO ZISINGETOKEA KABISA KWA MASLAHI YA TAIFA HILI)

HAWEZI MTU KUTOKA IRANI na kuja kuitawala nchi bila hao jamaa kuchukua hatua, eti kisa ajagombana na CCM, kwa hiyo hao jamaa wapo na siasa tu, lakini mwisho wa siku huyo MwIrani ka fu*k everywhere, ka corrupt mpaka huo usalama wenyewe

kwa kifupi hao jamaa wapo hapo kwa usalama wa wanasiasa tu
 
Pengine mwandada Katabazi amelazimika kusafisha jina (kwa uoga wake mwenye wa au kwa shinkizo) baada ya makala zake mbili,moja ya 13 February 2008

na makala yake hii ya 22 July 2007
 
Pengine mwandada Katabazi amelazimika kusafisha jina (kwa uoga wake mwenye wa au kwa shinkizo) baada ya makala yake hii ya February 2008
Ni kweli mkuu, baada ya kutuletea makala hiyo aliyo andika awali, kila mwenye akili atamwelewa. Aje hapa atufafanulie tofauti hizo mbili za makala zake zimetokana na nini? Maana zina rangi tofauti, nyeusi na nyeupe.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…