Hapiness Katabazi kauona ukweli lazima aseme kuwa penye kutoa hongera basi itolewe.nyie mliozoea kulaumu kila kitu kazi kwenu.
Hongera Katabazi kwa kuamka.
awezekana na yeye ni mmoja wao, anatikisa kiberiti kujua njiti zimo au la. Ndio namna nyingine ya utendaji wa wasalama wa Taifa. Wataupataje umbeya kujua watu wanafikiri nini wajue pa kuanzia? Ile ya kwanza haikumpa feedback ya kutosha, sasa amegeuza sura angalau apate kwa wale wanaoamini mbadala wa ile ya kwanza.Ni kweli mkuu, baada ya kutuletea makala hiyo aliyo andika awali, kila mwenye akili atamwelewa. Aje hapa atufafanulie tofauti hizo mbili za makala zake zimetokana na nini? Maana zina rangi tofauti, nyeusi na nyeupe.
Hakuna anayeweza kushangaa kwa uliyosema.Hapiness Katabazi kauona ukweli lazima aseme kuwa penye kutoa hongera basi itolewe.nyie mliozoea kulaumu kila kitu kazi kwenu.
Hongera Katabazi kwa kuamka.
Nimebaki naduwaa...nahisi ntabaki salama!Nimesoma hoja yako mama, labda kama nimesoma haraka haraka,lakini sioni jambo lolote la kukufanyanya wewe uwapongeze usalama wa Taifa. To me hawa ndio watu ambao in the first place wametufanya tufike Tanzania hapa tulipo leo. Wangekuwa makini yote tunayo yaona leo yangeonekana mapema na yakarekebishwa.
Jamaa hawa wametekwa kabisa na uovu ulioko katika jamii leo,kwa hiyo hawana uwezo kabisa wa kutusaidia kama ilivyotegemewa unless a complete overhaul of the system is made.
Tanzania haijawahi kuwa na usalama wa taifa hata mwaka mmoja kama wapo basi watakuwa hawajui kazi na maana ya usalama wa taifa ninaweza kusema Tanzania tuna watu wa usalama wa viongozi wa taifa kazi inayoweza kufanywa na jeshi la polisi.
FBI au CIA kwa mfano vina vitengo vya kulinda maslahi ya mataifa yao CIA anaweza kuja kuishi Tanzania kwa muda mrefu tu anaweza kuja kama Mwalimu na ukiangalia wanaokuja wachache sana hufudisha masomo ya maana sana sana watafundisha PE au kwaya ya shule
Wengine huja kujifunza tamaduni zetu lakini hao wote lengo si tamaduni wanapiga mahesabu ni vipi nchi yao itafaidika na kitu gani toka Tanzania madini maliasili nk na kila siku wanapeleka ripoti makao makuu.
Angalia walivyo wepesi kukimbilia sehemu za majanga kama Haiti ni kweli watatoa misaada ya nguvu lakini ujue kuna kitu kinatafutwa kwa manufaa ya nchi zao hao ndio usalama wa taifa.
Tofauti na watu wetu kama nilivyosema tuna watu wa usalama wa viongozi wa taifa mtashinda nao bar mitaani hakuna wanachofanya cha maana hawana plan yeyote zaidi ya kuvizia vimagendo vidogo vidogo na dili za ujambazi ambazo nazo nyingi huwa wanahusishwa nazo utasema huo ni usalama wa taifa sasa polisi afanye nini.