Haya mambo ya ndani ya chupi.....ni muhimu lakini nadhani sisi Watanzania tumeyaongezea umuhimu zaidi....kiasi kwamba yamechukua sehemu kubwa ya fikra zetu hata kufikia hatua kuathiri mambo mengine zaidi ambayo tungetakiwa kuyatilia fikra kuyafanikisha.........
Ukubwa wa tatizo hili unaakisiwa na namna vijana walivyo nyuma kimaendeleo kwa kubuni miradi na mbinu za kupata mitaji ili kujikwamua kiuchumi....badala yake wakilalamika hata katika mambo yanayohitaji fikra ndogo kuyafanikisha.......
Utumwa wa fikra hizi umewafanya vijana....waishi katika ulimwengu wa kufikirika ambao ni kama paradiso kwao...kwani kuishi katika ulimwengu inakulazimu uwe na kipato ambacho wengi wao hawana vyanzo hivyo...na matokeo ya fikra hizo ili kuishi kwenye ndoto hizo kijana analazimika kutafuta njia za mkato za kujipatia vipato ambazo nyingi ni haramu na matokeo yake ndio tunashudia wizi wa kila aina bila ya kusahau na ujambazi......
Hata wale vijana waliopata ajira....wamejikuta wakiwekeza kila senti yao wanayoipata huko kwani wanadhani kuwa hakuna starehe kubwa kama hiyo....na kuikosa huko ni sawa mtoto kukosa maziwa ya mama....yaani mambo hayawezi kuwa sawa.......
Atalazimika kuishi maisha ya kuwavutia hao wanawake hata kama maisha hayo yatamgharimu kiasi gani.......
Ndio unashangaa kumkuta kijana mwezi mmoja wa ajira anakubali kuubeba mzigo wa mkopo wa gari...kazini kwake ili aendane na ndoto hiyo.....
Na wengine wanalazimika hata kupangana makazi katika maeneo ambayo hayaendani na vipato vyao ili mradi kuishi katika ulimwengu wa ndoto.......
Huu na wenyewe ni utumwa kama ulivyo utumwa mwimgine ambapo ukombozi wake....unataka kwanza ujitambue na kujielewa..........
WE BECOME WHAT WE THINK.....