Dkt. Gwajima D
Minister
- Nov 28, 2015
- 966
- 6,019
Wapendwa Wana Jukwaa letu pendwa, salaam.
Sisi familia ya Advocate Gwajima, tunawashukuru sana kwa ushirikiano wenu na upendo wenu kipindi chote cha mwaka 2024.
Tunawatakia Heri ya Mwaka Mpya 2025 na Baraka tele mwanzo hadi mwisho wa mwaka huu. Tunawaombea na kuwatakia Upendo, Furaha na Amani vikatawale kwenye familia zenu daima, muukatae ukatili kwa nguvu zote na akili zote na fahamu zenu zote, na Mungu wa mbinguni awe pamoja nanyi na mipango yenu yote aifanikishe, Amina✍🏻
Zaidi ya yote, nawashukuru Sana kwa Tuzo ya JF ambayo, umenipa hamasa ya kuendelea kuitumikia jamii yetu huku nikiendelea kwa bidii zote kupokea hoja zenu na maoni yenu na kufanyia kazi na kuendelea kuomba na kuheshimu ushirikiano wenu daima. Hakika, ushirikiano wa jamii ni mtaji na nguzo ya kwanza ya kufanikisha wajibu wetu.
Salaam kwa Uongozi wote wa JF na washirika wake na wafuasi wake wote. Mungu awabariki.
Sisi familia ya Advocate Gwajima, tunawashukuru sana kwa ushirikiano wenu na upendo wenu kipindi chote cha mwaka 2024.
Tunawatakia Heri ya Mwaka Mpya 2025 na Baraka tele mwanzo hadi mwisho wa mwaka huu. Tunawaombea na kuwatakia Upendo, Furaha na Amani vikatawale kwenye familia zenu daima, muukatae ukatili kwa nguvu zote na akili zote na fahamu zenu zote, na Mungu wa mbinguni awe pamoja nanyi na mipango yenu yote aifanikishe, Amina✍🏻
Zaidi ya yote, nawashukuru Sana kwa Tuzo ya JF ambayo, umenipa hamasa ya kuendelea kuitumikia jamii yetu huku nikiendelea kwa bidii zote kupokea hoja zenu na maoni yenu na kufanyia kazi na kuendelea kuomba na kuheshimu ushirikiano wenu daima. Hakika, ushirikiano wa jamii ni mtaji na nguzo ya kwanza ya kufanikisha wajibu wetu.
Salaam kwa Uongozi wote wa JF na washirika wake na wafuasi wake wote. Mungu awabariki.