Heshima kwa walimu ipo wapi?

ameline

JF-Expert Member
Joined
Jan 8, 2013
Posts
2,292
Reaction score
1,151
Nashindwa kuelewa serikali ina mpango gani na walimu jamani? mtu anajitahidi kusoma kacertificate kake au kadiploma, au hata kadegree kamoja jamani kwa tabu zake zoote, wengine kwa kuungaunga wengine kwa kuunganisha anabahatika kuchaguliwa then unampeleka sehemu kama hii kweli?? hebu chunguza hilo eneo kama utampata hat mkaza mjomba wa raisi kikwete au hata mawaziri au kiongozi yeyote wa kisiasa, nani atakaekubali ndugu yake alale kwenye nyumba kama hii? Mimi siyo mwalimu lakini ninaumia sana ninapopata taarifa kama hizi, mara ooh mwalimu mkuu kaangukiwa na nyumba, mara oooh mwalimu anaishi ofisini,. this is too much! kama mtu anashindwa kukufanyia dogo kama hili jamani utatarajia kubwa litoke wapi? hebu wananchi tuamke jamani, tunajua kuna mambo meengi sana yamefanywa na serikali ili kuboresha elimu lakini kwa hili, hamjaniambia kitu,. kuna msemo tunaoutumiaga kule uchagani unasema hivii..."UKUNDI MANYA KYA NUMBA AMBIYA KYICHUMI" maana yake ni kwamba ukitaka kujua kilicho nyumbani mwa mtu angalia mlango wa kuingilia, au angalia getini mazingira utakayoyaona ndivyo nyumbani kulivyo,.sasa kweli mwalimu ataishi kwenye nyumba kama hii then elimu ifanikiwe vip hapa? mwanafunzi atashindwa kuingia form one bila kujua kusoma? ari ya kufundisha ipo wapi? tusidanganyane bwana, kama ni kuboresha elimu tusifanye theoritically bali tujaribu kupractice kweli,.Tusiishie kutazama chama tu jamani tuangalie na watu waliomo huko kwenye chama, tuache unafiki, tuungane kuleta mabadiliko.



[h=3]hii ndio nyumba ya mwalimu mkuu iliyobolewa na mvua.[/h]
Nyumba ya mwalimu mkuu Chilaile wilaya ya Nachingwea yabomolewa na mvua
Wanafunzi wakimjengea mwalimu mkuu baada ya kubomolewa na mvua
Hebu niambieni wadau jamani kwa mtindo huu tutafika kweli? madogo wanaacha kusoma wanajenga nyumba, jamaniiii????:A S cry:
 
namna hii heshima ya wanafunzi kwa mwalimu wao inapungua!!!!
 
We made a critical mistake in 2005 and 2010. Then, it's high time to make corrections in 2015.
 
namna hii heshima ya wanafunzi kwa mwalimu wao inapungua!!!!

Just imagine, kama mwalimu anaishi kwenye nyumba kama hii je hao wazaz na watoto si wanalala nje? maana kwenye baadh ya vijiji mwl anaheshimika sana
 
We made a critical mistake in 2005 and 2010. Then, it's high time to make corrections in 2015.

Tukiwaambia watu, wanatuita tunasiasa uchwara, sasa hao ambao ni wa ukweli wamefanya nini?
 
heshima ya mwalimu iko kwenye kula vimbi la chaki na kuugua kifua!
 
heshima ya mwalimu iko kwenye kula vimbi la chaki na kuugua kifua!

yaan hata hizo mbao zao za machaki hawataki kuzibadili waeke zile za markerpen kama huko vyuon,. kwanini hawatak kuboresha maisha ya walimu jamani????mbona sector nyingine wanaboreshewa??aaah:A S angry:
 

sibora hata huyo ccm wamemjengea kibanda umiza walimu wengine hawana hata hicho.kweli hatari
 
kwa hali hii elimu nchi hii haiwezi kukua mpaka pale serikali itakapoanza kumthamini mwalimu.
 
Kuda....dadeki walai "USIPOSIMAMIA JAMBO MOJA UTAFELI KATIKA MAMBO YOTE"
Hawa CCM wamesimamia maslai ya chama cha mal0ri(CCM), inabidi 2we tayari kwa hari na akili ikiwezekana 2we tayari kumwaga damu, cuz YESU ALIMWAGA DAMU TUOKOKE angamia uwaokoe waTZ.
 

best una hasiraaaa, angalia aliekaa pembeni yako usimtwange ngumi...lol ni kweli mambo mengine yanatia hasira sana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…