Didia
JF-Expert Member
- Nov 9, 2010
- 719
- 260
Ndugu wana jukwaa katika hali ya kushangaza maafisa wa bodi ya mikopo kwa kushirikiana na uongozi wa chuo kikuu cha Iringa zamani kikijulikana kama Tumaini wameamua kukata hela za wanafunzi wanao fadhiliwa na bodi chuoni hapo kinyume na mikataba kati ya wanafunzi na Bodi.
Katika sakata hilo wanafunzi wa mwaka wa pili na watatu wamejikuta katika hatari ya kupoteza kati ya shilingi 150,000 hadi 300,000 kufidia wizi huo. Baada ya kutafuta taarifa bila mafanikio kutoka katika uongozi wa chuo na kujaribu kuhoji uhalali wa swala hilo leo tarehe 5/11/2014 wanafunzi hao wamekumbana na vitisho vikali kutoka kwa Naibu makamu mkuu wa chuo akiwataka kuufyata au vinginevyo watakumbana la rungu la utawala.
Aidha tofauti na ilivyo zoeleka mpaka sasa uongozi wa chuo umekataa kata kata kutoa orodha inayo onyesha kiwango halisi cha ada inayo tegemewa kulipwa na bodi mwaka 2014/2015 ili wanafunzi wasaini ada hizo kwa madai kwamba chuo kina mamlaka ya namna gani kiendeshe mambo yake!
Swala lenyewe liko hivi:
1. Wanfunzi walipata ufadhali wa bodi ya mikopo (kwa mwaka 2012/2013 na 2013/2014) kwa mkataba wa kulipiwa ada 750,000/- ; 1000,000 au zaidi kutegemeana na matokeo ya kipima uwezo ( Means Testing)
2. Katika miaka iliyo tangulia Wanafunzi wameendela kulipiwa viwango hivyo na Bodi na wao kutakiwa kujazia tofauti
3. Katika hali ya kushanganza kwa mwaka huu wa masomo 2014/2015 wanafunzi wamekuta viwango vya ada inayo lipwa na bodi vimepunguzwa kwa kati ya sh. 150,000 na 300,000 na hivyo kutakiwa kulipa tofauti hiyo. Wamefanya kila linalowezeka kutafuta maelezo bila mafanikio
Kwa kutumia jukwaa na mimi kama mdau wa kupinga dhuruma na ufisadi nawasilisha taarifa hii ili tuwasaidie kupaza sauti na kukemea huu wizi
Didia
Nawasilisha
Katika sakata hilo wanafunzi wa mwaka wa pili na watatu wamejikuta katika hatari ya kupoteza kati ya shilingi 150,000 hadi 300,000 kufidia wizi huo. Baada ya kutafuta taarifa bila mafanikio kutoka katika uongozi wa chuo na kujaribu kuhoji uhalali wa swala hilo leo tarehe 5/11/2014 wanafunzi hao wamekumbana na vitisho vikali kutoka kwa Naibu makamu mkuu wa chuo akiwataka kuufyata au vinginevyo watakumbana la rungu la utawala.
Aidha tofauti na ilivyo zoeleka mpaka sasa uongozi wa chuo umekataa kata kata kutoa orodha inayo onyesha kiwango halisi cha ada inayo tegemewa kulipwa na bodi mwaka 2014/2015 ili wanafunzi wasaini ada hizo kwa madai kwamba chuo kina mamlaka ya namna gani kiendeshe mambo yake!
Swala lenyewe liko hivi:
1. Wanfunzi walipata ufadhali wa bodi ya mikopo (kwa mwaka 2012/2013 na 2013/2014) kwa mkataba wa kulipiwa ada 750,000/- ; 1000,000 au zaidi kutegemeana na matokeo ya kipima uwezo ( Means Testing)
2. Katika miaka iliyo tangulia Wanafunzi wameendela kulipiwa viwango hivyo na Bodi na wao kutakiwa kujazia tofauti
3. Katika hali ya kushanganza kwa mwaka huu wa masomo 2014/2015 wanafunzi wamekuta viwango vya ada inayo lipwa na bodi vimepunguzwa kwa kati ya sh. 150,000 na 300,000 na hivyo kutakiwa kulipa tofauti hiyo. Wamefanya kila linalowezeka kutafuta maelezo bila mafanikio
Kwa kutumia jukwaa na mimi kama mdau wa kupinga dhuruma na ufisadi nawasilisha taarifa hii ili tuwasaidie kupaza sauti na kukemea huu wizi
Didia
Nawasilisha