HESLB kulipwa deni la milioni 7 na Fred Vunjabei kwa miaka 20 inatafakarisha

HESLB kulipwa deni la milioni 7 na Fred Vunjabei kwa miaka 20 inatafakarisha

Yoda

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2018
Posts
48,475
Reaction score
70,102
Fred Ngajiro maarufu kama Vunjabei ameonyesha mtandaoni barua ya kumaliza kulipa deni la ufadhili wa masomo ya digrii ya kwanza aliyopewa na bodi ya mikopo ya wanafunzi wa vyuo vikuu(HESLB) huku akiwahamiza wengine kufanya hivyo pia.

Kama barua hiyo inayosambaa mtandaoni ni ya kweli basi inadhihirisha udhaifu mkubwa wa mfumo wa HESLB katika kukusanya madeni yake. Kuna vijana wengi waajiriwa ninaowafahamu wenye kipato kidogo sana kuliko Fred waliomaliza miaka 10 iliyopita na waliopata mkopo mkubwa kuliko Fred ambao wamemaliza kulipa mikopo yao muda mrefu kuliko yeye.

HESLB inahitaji kufikiria namna mpya ya kuhakikisha sio waajiriwa tu ndio wanaopewa mzigo wa kulipishwa kwa haraka deni la HESLB bali hata wafanyabiashara binafsi. Pia hili linaleta maswali kama Vunjabei amekuwa akiripoti mapato yake kwa usahihi TRA miaka yote hiyo na hiyo milioni 7 ndio iliyopatikana kwa yeye kuwa anakatwa 15% kwa muda wote huo katika mapato yake.


Pia soma Fred Vunjabei amaliza deni la mkopo chuo (HESLB)
 
Ni kweli unachosema Mkuu, kwa sehemu kubwa Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu inalega lega kwenye ukusanyaji wa Madeni.

Imejikita zaidi kwa Watumishi wa Umma kwa kuwa ni rahisi kuwafikia kuliko wengi waliopo Sekta Binafsi na Biashara.

Ni vyema kubadirisha mbinu za kudai hayo madeni yao. Kama mtu ana leseni ya Udereva/Leseni ya Biashara/Hati ya Kusafiria n.k Serikali inashindwa nini kuweza kulink mifumo yote hiyo kuweza kuwabaini Wadaiwa wake.

NB; Kila mnufaika wa Mkopo wa Elimu ya Juu ana wajibu wa Kulipa Deni lake kama alivyokopeshwa ili kuongeza Wigo wa Serikali kuwakopesha wadogo zetu na Watoto wetu
 
Fred Ngajiro maarufu kama Vunjabei ameonyesha mtandaoni barua ya kumaliza kulipa deni la ufadhili wa masomo ya digrii ya kwanza aliyopewa na bodi ya mikopo ya wanafunzi wa vyuo vikuu(HESLB) hukua akiwahamiza wengine kufanya e hiyo na hiyo milioni 7 ndio iliyopatikana kwa yeye kuwa anakatwa 15% kwa muda wote huo katika mapato yake.
Uzalendo muhimu Mimi watz hawapendi kulipa madeni then huyo Fred amefanya Kazi serikalini na private so nadhani kwa mujibu wake mtaji aliupata katika ajira yake ya serikalini mil 20 then akaanza Biashara so tunaweza kuona kuwa uzalendo matter most
 
Acha unonko dogo. Wewe soma tu au lipa tu. Unaifundsha serikali wanikamate? Ukome.
 
Back
Top Bottom