Nikiangalia kwa uzoefu wangu ktk suala hili la mikopo, naona wazi kuwa HESLB huwa haitupi kipaumbele sana watu wa diploma japokukuwa idadi yetu huwa ni ndogo ukilinganisha na wale wa kidato cha sita. Nakumbuka mwaka 2011 nilichaguliwa UDOM-BSc. Applied Geology wakaninyima mkopo nikaahirisha kusoma. Mwaka huu tena nimechaguliwa UDSM-BSc. in Geology na mkopo nimekosa kabisa. Na ni wengi wa diploma tumetengwa tena mwaka huu na HESLB kana kwamba sisi tuna uwezo wa kujisomesha. Ipo haja ya kufanya kitu hapa, NACTE nao wanapaswa kutuunga mkono hapa.