Wkt bunge limekaa ilipitishwa hoja ya kuwaangalia upya wanafunzi waliokosa mikopo kwa mwako wa masomo 2012/13 na likaamuru bodi kuwaangalia upya wanafunzi wanaoendelea na masomo na likaja na hoja kwamba wanafunzi wote waliokosa mikopo watume tena upya. Lakini mpka leo hii nayaandika haya hakuna lolote linaloendelea na hatujui nini kinachoendelea, tulitegemea nasi angalau kufikiriwa maana pesa hakuna wazazi mambo hawako vizur kwa sasa na mpka sasa hata ada sijalipa nikitegemea walau bodi itanisaidia kupunguza mzigo huu lkn wako kimya. Sijui hatima ya maisha yangu ya chuo kwa sasa, tunaomba bodi itoe tamko kama pesa zetu tulizotengewa wamezihamishia kwa wa mwaka wa kwanza kufuta aibu watwambie tujue moja maana tumechoka kusubir. Mfano hapa Mzumbe walitusainisha majina lakini mwisho wa cku hatujui yale majina yameishia wapi? Bodi mna siri gani na second yr tunaomba mtufahamishe tatizo sis hatuitaji migomo ila haki yetu ni muhimu