HII Itawezekana BONGO

HII Itawezekana BONGO

Magulumangu

JF-Expert Member
Joined
Jan 7, 2010
Posts
3,051
Reaction score
461
Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Sulemani Kova
Polisi kwa kushirikiana na wafanyabiashara jijini Dar es Salaam, wameanzisha mchakato wenye lengo la kuyafanya maduka yaliyopo Kariakoo yafanye kazi hadi saa sita usiku.
Kwa mujibu wa utaratibu uliopo sasa, maduka hayo yanafungwa ifikapo saa 12:00 jioni.
Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Sulemani Kova aliwaambia waandishi wa habari kuwa, jeshi hilo linawasiliana na wafanya biashara wa eneo hilo, ili kuanza majadiliano.
Alisema hatua ya maduka hayo kufunguliwa hadi saa sita usiku itasaidia kuongeza kipato cha wafanyabiashara, kukuza uchumi na kupunguza msongamano wa watu.
Kwa mujibu wa Kova, masuala ya msingi yatakayopewa kipaumbe katika mchakato huo ni yanayohusu ulinzi na usalama.
Kova alisema majadiliano hayo yamelenga kuimarisha ulinzi wa kutosha katika eneo hilo, ikiwa ni pamoja na kutumia mbinu ya kuweka taa kubwa na kufunga kamera za kuwabaini wahalifu.
Pia alisema mchakato huo utajumuisha kuanzishwa njia za simu ambazo zitatumika kwa haraka katika kutoa taarifa za uhalifu.
"Hatua hii itawasaidia hata watu wanaotoka kazini jioni, kwenda madukani kununua bidhaa pasipo uharaka wala msongamano,” alisema.
Alisema jambo la muhimu kwa wafanyabiashara hao ni kuzingatia masharti yanayohusu ulinzi.
Wakati huo huo jeshi la polisi limefanikiwa kuwakamata watu 11 wanaosadikiwa kuwa majambazi sugu, wakituhumiwa kwa makosa mbalimbali jijini hapa.
Miongoni mwa makosa hayo ni ujambazi wa kutumia silaha, wizi wa televisheni, pikipiki za miguu mitatu bhangi na gongo.
Kova alisema kuwa bado wanaendelea na operesheni ya kuwasaka majambazi sugu kwa lengo la kuondoa uhalifu jijini humo...

UCHUKUO WANGU..

Ujambazi unakua kwa kasi ya ajabu tz hata mchana je wakianzisha hii maduka mpaka usiku kutakalika kweli Kariakoo jamani?KOVA ATAWEZA KWA HILI
 
Ndiyo ina wezekana. Kukiwa na watu watakao jitokeza huo usiku na usalama toka kwa jeshi la polisi hata uhalifu utakua adimu. Na kama huo muongezeko wa muda una maanisha kipato zaidi kwa hayo maduka, basi wamiliki wa maduka kadhaa zinazo fuatana au wa mtaa mmoja wana weza kukusanya nguvu kugharamia ulinzi wa ziada toka kwa private security firms. Ni kitu kina wezekana ni planning tu na implementation. Tatizo Tanzania tuna sema hatufanyi.
 
hiyo kufanya shopping mchana tuu unaenda roho juu ndo iwe ucku!!?? hapo hawanipati kabisa.
 
Polisi wanashughulika na usalama wa wenye maduka. Sawa. Lakini jee usalama wa watakaonunua vitu usiku nao unashughulikiwa vipi?
 
Kila kitu kinawezekana lakini suala la msingi la kuangalia ni usalama MUUZAJI na MNUNUAJI
 
Nairobi insifika kwa kuwa na wimbi kubwa la ujambazi....lakini Nairobi hailali...biashara 24/7!!
wasiwasi wangu... wazo jema ila limlenga kuwanufaisha wafanya biasha... sie ma-kapuku tunaonuna bidhaa na kurudi kwetu si ndo tunaviziwa vuri na vibaka!!?! Tunahakikishiwaje usalama?1:confused2:
 
Hapa wana mpango wa kuharibu gesti za watu wanaolala kariakoo kwa kukosa sehemu za kulala na huamua kulala pembezoni mwa majengo kwa kutandika maboksi.
Kuhusu ulinzi inawezekana ni namna ya kujipanga tu
 
Nadhani, ni kumwaga polisi. kama wa mzimbazi station hawatoshi, azima ilala au magomeni. Wanaweza hata kuazima polisi wa msasani na zile sehem zilizotulia. Hii ifanywe ilhali wanafundisha polisi wengine. Kama hela za kulipa mishahara hazitoshi basi waongeze kataksi kadogo sana kwenye sales, ili kuchangia mishahara ya polisi. Wazo la kufungua biashara mpaka usiku, sio baya.
 
Wazo zuri and lenye FAIDA zaidi kwa Nnchi, Wafanya Biashara na Wezi,
LItaongeza matumizi zaidi kwa Mtanzania (though haulazimishi kununua), Kwa namna moja au nyingine Itaboresha Kutokomeza Giza Dar es Salaa, Wazo, muda wa kazi uongezwe pia kumnufaisha Mfanyakazi,
 
Back
Top Bottom