Hii Mpya;muhimu Soma

Sanda Matuta

JF-Expert Member
Joined
May 9, 2007
Posts
949
Reaction score
142
FORMULA MILK.
Imesikika na kutekelezwa na wauza mudauka wote wa jiji la Dar es salaam kwamba maziwa hayo yamepigwa marufuku kuuzwa kwenye maduka,sababu kubwa ikiwa imeelezwa (KUTOKA HUKO JUU ORDER ILIPO TOKA) ya kwamba hii ni kutokana na WAZAZI WENGI KWA SASA HAWATAKI KUNYONYESHA MAZIWA YAO (BREAST FEEDING) waki tegemea maziwa hayo mengine yaani Formula.

Sasa maswala ni kwamba moja,Vipi kwa wale ambao kunatokana na kukutwa na HIV wametakiwa na Madaktali wao wasinyonyeshe watoto ila wawape hizo formula milk?

Pili,nini kitatokea na vile vichanga vinavyopoteza wazazi wao kwenye kuzaliwa?

Tatu,kwa wazazi ambao tayari wamewwazoesha watoto wao hayo maziwa ya formula,hii ni kutokana na muda mwingi wakunyoshesha hawana kwakuwa labda wanakua wapo makazini au sehemu nyingine za kujiongezea kipata baada ya maisha kuwa magumu kipindi cha sasa unlike zamani where woman sat at home to rise children.

Jamani hii tanzania yetu inaenda wapi?wengine wanapiga hatua mbele sie tunaenda kinyume nyume.Isiwe kwamba kuna mtu kakosa % yake kwenye containers za maziwa hayo huko bandalini?
Au je maamuzi hayo yana weza kuwa backed na sababu za KIDAKITARI kama hivyo ndivyo basi JF DOCTOR embu nisaidie hapa
 
Sanda,

Hilo tamko binafsi lilinipita......hivi ni nani/Wizara/Waziri/Ofisi/Afisa alitoa tamko hilo.....ili tupate kuelimishana naye hapa..........
 
huu utakuwa ukurupukaji uliotukuka, 'huko juu' kunamaanisha nani? rais, makamu rais, waziri mkuu, waziri wa chakula, afya na maendeleo ya jamii, WAZIRI WA MIUNDOMBINU au WAZIRI WA FEDHA UCHUMI NA MIPANGO?)
 
huu ni utakuwa ukurupukaji uliotukuka, 'huko juu' kunamaanisha nani? rais, makamu rais, waziri mkuu, waziri wa chakula, afya ya jamii, WAZIRI WA MIUNDOMBINU au WAZIRI WA FEDHA UCHUMI NA MIPANGO?)

Inawezekana - na mimi nadhani - ni udaku.
 
Mimi nilisikia kuwa ni batch moja tu ya Lactogen ndo ilikutwa na matatizo.
Kimsingi uamuzi uliochukuliwa na serikali kupitia Mamlaka ya Chakula na Dawa(Tanzania Food and Drugs Authority-TFDA) ni mzuri lengo ni kuokoa watoto wasidhurike maana yalikutwa yana kiwango kikubwa cha baadhi ya ingredients.
Kwa ufupi batch moja ndo ilipigwa marufuku. Kwa hilo tuwapongeze TFDA.
 

Kweli,hata sisi tulisikia hivyo lakini embu jalibu kwenda madukani sasa ivi!alafu uje utujuze hali ikuje
 

Yeyote aliyefanya hili (ninadhania kuwa ni mwanamme) inabidi afungwe jela kwa miaka sita au zaidi huku akichapwa viboko 12 kila siku asubuhi na jioni na siku akitoka jela achapwe viboko 72 vya matakoni ili aende akamuoneshe mkewe.

Maamuzi mengine hata yanatia kichefuchefu kuyasikia, hili hata linapita lile la Mama Ghasia (soma fujo na ukosefu wa amani) la kutaka wanawake wavae nguo za utamaduni wa kiarabu......or whatver she meant

Grrrrrrrrrrrr
 

Kama ni batch moja tu, kwa nini pingamizi litokee kwa yote. Hii kama kweli imetokea itakuwa moja ya maamuzi ya kipuuzi kabisa yaliyowahi kutolewa Tanzania.
 
i wish ingekua Udaku kama usemavyo.
Nenda dukani sasa ihi ilie kopo la S26 namab mbili lilikua alfu 12 sasa ni alfu 16

S26? may be imeonekana fake, na sio kuwa formula milk zote zimepigwa marufuku! au lactogen sio formula.

Ipi hasa imepigwa stop, S26 au lactogen? kama ni kwa ajili ya kiwango, walitakiwa wadhibiti uingiaji maziwa fake. Hivi TFDA kazi yao (ToR) ni kupiga vitu marufuku na kuviteketeza, hakuna cha zaidi wanachoweza kufanya kuhakikisha vyakula na dawa fake haziingii nchini?
 
Hata mimi pia nina mtoto na week yote hii nimekuwa nikihangaika kutafuta hayo maziwa ya formula milk, yaani yamekuwa adimu balaa, na hata ukiyapata basi ni bei juu kupita kiasi, na maduka nayo yanachukulia advantage kupandisha bei cos wanajua lazima utanunua. Leo nimepata kwenye duka moja pale Tx market kinondoni kwa sh 15,000/= na mwanzo kabla hayajapigwa marufuku yalikuwa yanauzwa 11,500 mpk 12,000/=

sijui nchi hii inakwenda wapi, kuna vitu vingi vya kupiga marufuku wanaacha na kupiga marufuku maziwa ya watoto.

Ushauri hebu nendeni madukani na muulize kama mtapata ili tuje tujadiliane tufanye nini kuhusu hili. Maana ni janga kwa wote wenye watoto.
 

Utata ni reference ya 'huko juu' to my knowledge mkurugenzi wa TFDA ni mwanamke, Margareth Ndomondo-Sigonda, hope she knows better. kuwa formula fake na kufikia kupiga marufuku kimya kimya-this happens only in Tanzania. Wenzetu hata toy tu isiyo na ubora wa 100% wanaipigia kelele kutwa kucha kwenye media.
 

Jaribu GAME, japo ni expensive kuliko kwenye maduka ya kawaida, but I wonder kama yatakuwepo bado kutokana na demand kuwa kubwa.
 
Hiyo siyo kweli. Ni batch moja tu. Mengine utayakuta kwani hayana matatizo.Kesho nitacheki then nitawaambia hiyo batch number na tatizo hasa lilikuwa nini?
Ni vema tufanye uchambuzi wa kina kabla ya kuanza kupinga pinga kila kitu. Au tunataka mpaka watoto wafe ndo tuanze kulaumu mamlaka husika kutochukua hatua?
 

Je una hakika la hilo?... hebu tuangalie hapa chini huenda ikawa ndio sababu....au kama ulivyosema sababu ya ka-ten%...maanake TZ kwa mizengwe ya ka ten ndio yenyewe......




 
Na kumjibu MAMA ni kuwa niliona TFDA waliitish mkutano na media wakatoa tangazo.Pia press release zilitoka kibao. Nakumbuka kumuona mkurugenzi wa tfda mama Ndomondo kwenye gazeti la kulikoni akiwa na sample ya lactogen iliyozuiwa na pembeni yake akiwa na mkurugenzi mwenzie wa mambo ya chakula. May be tuwaombe TFDA kama wanasoma Jf waweke tangazo hilo ili wanajamii walisome
 

mleta mada alivyoiweka ni kama vile infant formula zote zilikuwa recalled, on top hapa zote S26 na lactogen zimetajwa kwa nyakati tofauti kuwa zimepigwa marufuku kwa sababu zinasababisha akina mama WASIBREAST FEED! na hiyo marufuku imetoka juu.


Asante kwani sasa naelewa kuwa TFDA walipiga marufuku batch moja ya lactogen, je mlaji wa kawaida atawezaje kugundua batch ilikuwa recalled?
 
Nat867, na mie nilimuona huyo mama Mkurugenzi wa TFDA akielezea kasoro zilizopo kwenye hiyo batch, kwa jinsi alivyoeleza ilikuwa ni kwa nia nzuri tu ya afya ya watoto wetu, isipokuwa kuwa tu inaonekana hiyo batch ndo watu walikuwa wanaipenda, jamani watz, kitu kama wataalamu wamesema hakifai, kwa nini tusiwaelewe?? Wala haikuelezwa kuwa ni ku discourage wanawake ambao hawanyonyeshi watoto wao.....sijui... ila hiyo siyo sababu iliyotolewa na wataalam
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…