Idd Ninga
JF-Expert Member
- Nov 18, 2012
- 5,497
- 4,775
THAMANI YA POPI.
1)Tumeirudi miaka,ile tisini na ine
Anathaminiwa paka,na wale watu wengine
Tumeiruka mipaka,tumenda pande nyingine
Ya binadamu thumuni,thamani ya popi kubwa
2)Utu wazidi ponyoka,ni dhambi kubwa pengine
Wamsujudia nyoka, awe ndo Mungu mwingine
Sidhani tutanyooka,tusipotenda mengine
Ta binadamu thumuni,thamani ya popi kubwa.
3)Haswa kwa anaebweka,kweli mijitu mingine
Akili zimebweteka,kwa hili acha wanune
Kunapo kukurupuka,vipi akili wakune
Ya binadamu thumuni,thamani ya popi kubwa.
SHAIRI- THAMANI YA POPI
MTUNZI- Idd Ninga,Tengeru Arusha
+255624010160
iddyallyninga@gmail.com.
1)Tumeirudi miaka,ile tisini na ine
Anathaminiwa paka,na wale watu wengine
Tumeiruka mipaka,tumenda pande nyingine
Ya binadamu thumuni,thamani ya popi kubwa
2)Utu wazidi ponyoka,ni dhambi kubwa pengine
Wamsujudia nyoka, awe ndo Mungu mwingine
Sidhani tutanyooka,tusipotenda mengine
Ta binadamu thumuni,thamani ya popi kubwa.
3)Haswa kwa anaebweka,kweli mijitu mingine
Akili zimebweteka,kwa hili acha wanune
Kunapo kukurupuka,vipi akili wakune
Ya binadamu thumuni,thamani ya popi kubwa.
SHAIRI- THAMANI YA POPI
MTUNZI- Idd Ninga,Tengeru Arusha
+255624010160
iddyallyninga@gmail.com.