Hii ndiyo dalili ya mtu mwenye kansa ya ngozi epuka!

Hii ndiyo dalili ya mtu mwenye kansa ya ngozi epuka!

ibra blogger

Member
Joined
Jan 19, 2018
Posts
13
Reaction score
22
Nini maana ya kansa ya ngozi?


Hii ni uharibifu wa ngozi unaotokea katika seli ya ngozi na kukufanya uweze kusikia maumivu makali sana, ugonjwa huu hutokea kwasababu mbalimbali kama zifuatazo;

1.Kukaa juani kwa muda mrefu- hii hufanya miale ya jua kisasyansi tunaita ultraviolent rays kupeneya katika ngozi yako na kuua seli zakocmiale hii huwaathiri hasa watu wenye albinism, macho ya bluu na nywele nyekundu.

Miale hii tunaweza kuipata hasa tutakapokaa maeneo yenye ikweta kama Uganda na Kenya.

2.Kua na kinga hafifu ya mwili-hii hutokea pale unapokua na magonjwa hatari kama UKIMWI hii hufanya kinga yako kua hafifu mno na kupelekea kushindwa kuzuia miale ya jua pindi inapo ingia katika mwli wako.


3.Kupiga X-RAYS mara kwa mara.


4.Pia wazee wagonjwa wanahatari ya kupata ugonjwa huu.


DALILI ZA MTU MWENYE UGONJWA HUU.


(a)Ngozi kuuma mara kwa mara


(b)Kutokwa na damu kwenye ngozi.


(c)Ngozi kuvimba na kua ngumu.


ZIFUATAZO NI KINGA ZA KANSA YA NGOZI.


1.Epuka kukaa juani hasa kuanzia saa 4 asubuhi mpaka saa11


2.Vaa miwani yaani sun glasses


3.Chagua lotion/au mafuta ya kujipaka yanayozuia mwanga wa jua.


4.Tembelea daktari kama tatizo lako likizidi.
 
jua la siku hizi sio poa kabisa linaunguza unarudi home unanuka mishikaki, mikono myeusi, sura nyeusi, mbupu nyeupe
 
Mleta mada tumekusikia lakini ki matendo kule kwetu Tandahimba tunashinda juani tukilima na wazee wanagonga 98 bila warara wala mkwaruzo
Ngozi ya mtu mweusi mwenye melanin za kutosha sidhani kama yupo hatarini kupata kansa ya ngozi eti kwa sababu kawa exposed kwenye miale ya jua mara kwa mara...

Watu walio na ulemavu wa ngozi ndio kundi pekee lililopo kwenye hatari ya kupata kansa ya ngozi...
 
Umesahau wadada ambao wanatumia kemikali hatarishi kujipaka mwilini...
 
Ngozi ya mtu mweusi mwenye melanin za kutosha sidhani kama yupo hatarini kupata kansa ya ngozi eti kwa sababu kawa exposed kwenye miale ya jua mara kwa mara...

Watu walio na ulemavu wa ngozi ndio kundi pekee lililopo kwenye hatari ya kupata kansa ya ngozi...
Watu weusi rumebarikiwa sana na Mungu kwa hilo.
 
Vp kwa sisi wakulima itabidi tutumie mbinu gani sasa maana tunashinda tukipiga jembe Juani daily
 
Asante mtoa kwa ushauri huu. Lete ushauri mwingine mkuu
 
Back
Top Bottom