Hii Ndiyo Sababu Ya Kuwekeza Kwenye Majengo Ya Kupangisha Ili Ustaafu Mapema

Hii Ndiyo Sababu Ya Kuwekeza Kwenye Majengo Ya Kupangisha Ili Ustaafu Mapema

Aliko Musa

JF-Expert Member
Joined
Aug 25, 2018
Posts
209
Reaction score
315
Je umefanya maamuzi ya kufikia uhuru wa kifedha kupitia majengo ya kupangisha?. Je umefanya maamuzi ya kustaafu mapema zaidi kupitia majengo ya kupangisha?.

Je upo tayari kuanza kumiliki majengo ya kupangisha ukiwa unaendelea na ajira yako?. Je upo tayari kuanza kumiliki majengo ya kupangisha ukiwa unaendelea kukuza biashara yako?.

Kama ni jibu la maswali yote haya ni NDIO, endelea kusoma ukurasa huu. Nakuhakikishia kuwa hutajuta kutenga muda wako wa thamani sana.

Somo la leo hii: Kutambua lengo kuu la kufanya maamuzi ya kustaafu mapema. Huwezi kufika usipojua unakwenda.

Ili uanze kumiliki nyumba za kupangisha ukiwa bado umeajiriwa unahitaji kufahamu mambo yafuatayo kwa ndani zaidi;-

Moja: Kwanini kubwa.

Pili: Malengo makubwa.

Tatu: Mbinu bora.

Nne: Tabia za kiwekezaji.

Mambo haya unatakiwa kuyafahamu kwa kufuata mlolongo nilioandika hapo juu.

Kwa leo hii, ninakushirikisha kuhusu kwanini kubwa na malengo makubwa.

(a) KWANINI KUBWA.

Ili uweze kumiliki nyumba za kupangisha ukiwa kwenye ajira unahitaji mambo mawili. Moja ni maarifa sahihi ya nyumba za kupangisha na pili roho imara (strong spirit) ya kuhitaji kumiliki nyumba hizo.

Unaweza kuwa na maarifa sahihi na usifikie kwenye kumiliki nyumba za kupangisha kwa sababu una roho (imani) dhaifu.

Maarifa sahihi yanajengwa na kujifunza kuhusu nyumba za kupangisha. Roho (imani) huimarika zaidi unapozidi kujifunza bila kukoma.

Lakini huwezi kutumia maarifa sahihi uliyonayo yahusuyo majengo ya kupangisha kama hutakuwa na imani kubwa ambayo husukumwa na kwanini kubwa.

Mfano; wengi sana katika jamii zetu wanafahamu kuwa majengo ya kupangisha yanalipa. Wengine wakachukua maamuzi ya kusomea digrii (shahada) ya uwekezaji katika ardhi na nyumba na fedha, lakini kwa kukosa na kwanini kubwa waliishia kumiliki nyumba mbili au tatu za kupangisha.

Wanaopata mafanikio kidogo sana wanakuwa na imani dhaifu. Hapa nina maana hawawezi kuona wanamiliki nyumba za kupangisha kufuatana na maarifa waliyonayo.

Wanakuwa na maarifa sahihi lakini wanavutwa na fikra za kukutana na chanagamoto. Ukiwa na kwanini kubwa, unakuwa umejitoa kwa lolote linaweza kutokea.

Wakati huohuo ukiendelea kutumia maarifa sahihi ya nyumba za kupangisha. Ukiwa na imani kubwa ya kupata mafanikio makubwa kupitia nyumba za kupangisha bila kutafuta maarifa sahihi, utachelewa sana kufanikiwa na pengine usifanikiwe kabisa.

Kwanini kubwa ni kunganishi kati ya maarifa sahihi ulinayo na nguvu ya pekee ambayo wanadamu tunaitegemea (Mungu wa mbinguni).

Kulingana na imani yako unatakiwa kuunganisha maarifa sahihi na nguvu itendayo maajabu. Kila mtu anayo nguvu hii. Kwa kufanya hivi, hutaweza kukata tamaa kamwe.

Kwako utakuwa umehsindwa siku unayoingia kaburini. Ifuatayo ni mifano ya kwanini kubwa unayoweza kuwa nayo. Kuajiriwa ni chanzo cha changamoto nyingi kwa walio wengi kutokana na sababu tofauti tofauti.

Moja; imani (dini).

Wengi hushindwa kuwa karibu na Mungu wao kwa sababu ya kanuni na taratibu za kazi. Hii kwa inakuwa ni KWANINI KUBWA kiasi kwamba hawapati usingizi. Kila mara hufikiria kujinusua kwenye mtego huu. Na njia ambayo hufikiria ni kumiliki nyumba za kupangisha ili kuachana kabisa na ajira yao.

Pili; Upendo (familia, watoto na jamaa).

Hawa nao hukosa kabisa amani moyoni mwao kwa sababu ya kukosa muda wa kuonyesha na kujenga upendo ndani ya familia zao.

Migogoro mikubwa kati ndoa yao inasababishwa na changamoto za ajira zao. Hii inakuwa ni KWANINI KUBWA kwao. Hii huwafanya wapiganie kumiliki nyumba za kupangisha ili waachane kabisa na ajira yao.

Tatu; kipaji.

Wapo wafanyakazi ambao hukwamishwa kukuza vipaji vyao kwa sababu ya kanuni na taratibu za ajira zao. Hii huwafanya wakose amani katika mioyo yao.

Hii inakuwa ni KWANINI KUBWA kwao ya kuwasukuma kumiliki nyumba za kupangisha ili watumie vyema uwezo ulio ndani yao kutoa thamani kubwa mno kwa wengine.

Nne; mamlaka na utawala.

Wapo wafanyakazi ambao wana uwezo mkubwa wa kutawala na kuwaongoza wengine.

Na wana ndoto hiyo ya kutawala wengine wakiamini watakuwa wamefanya kusudi la kuwatumikia wananchi wao. Hawa nao wanaweza kuonekana hawana maana mbele zao wananchi kama watakuwa maskini.

Hivyo huamua kumiliki nyumba za kupangisha ili waweze kupata kipato cha kuweza kufikia maono yao. Hii kwao inakuwa ni KWANINI KUBWA ya kuwafanya wasipate usingizi kabisa.

Tano; Utajiri mkubwa wa kifedha.

Kuna kundi lingine ambalo husukumwa zaidi na kutaka kuwa matajiri na kuweza kufanya mambo mema wayatakayo. Hawataki kuomba omba.

Wanataka kukusanya pesa nyingi sana kiasi kwamba wataweza kufanya majaribio ya kuhamia sayari zingine.

Kwa makundi haya matano, ni lazima upate KWANINI KUBWA yako kama kweli unahitaji kupata mafanikio makubwa kwenye nyumba za kupangisha.

Hata uwe na shahada (digrii) tano zinahusu fedha na uwekezaji kwenye viwanja na nyumba, kama hauna kwanini kubwa huwezi kumiliki nyumba za kupangisha za kuweza kukufanya upate mafanikio makubwa.

Hata uwe mbobezi wa viwango vya kimataifa kwenye majengo ya kupangisha kama hauna KWANINI KUBWA, huwezi kupata mafanikio makubwa kupitia nyumba za kupangisha.

Karibu unishirikishe lengo lako kuu la kuamua kustaafu mapema kupitia majengo ya kupangisha. Tumia namba ya WhatsApp au jiunge na kundi langu la Telegramu hapo chini ili uwe karibu zaidi na mimi.

Siku nyingine nitamalizia kukushirikisha na mambo matatu yaliyobaki nayo ni; malengo makubwa, mifumo na mbinu bora sana na tabia za kiuwekezaji.

Mwandishi,

Aliko Musa.
 
Hiyo biashara ni kichaa
Ni biashara inayolipa yenye return nzuri for the years

It's a generational wealth .

Real estate will make u to reach your financial freedom surely.

Nyumba za kupanga zimenisomesha mimi toka vidudu hadi chuo

Dingi angu alijenga nyumba 1990 huko alifarikia kitambo sana hata shule nilikuwa sijaanza

Nyumba ile imekuwa ya kupangisha kwa miaka zaidi ya 28 hadi leo tuna kazi zetu tunakula hela saafi kabisa hatukosi hela za vitumbuu ilhali alieijenga hayupo duniani

Real watakula wanao,wajukuu,vitukuu,vilembwe,vilembwekeze ,vining'ina.

Ni generational wealth
 
Hiyo biashara ni kichaa
Ni biashara inayolipa yenye return nzuri for the years

It's a generational wealth .

Real estate will make u to reach your financial freedom surely.

Nyumba za kupanga zimenisomesha mimi toka vidudu hadi chuo

Dingi angu alijenga nyumba 1990 huko alifarikia kitambo sana hata shule nilikuwa sijaanza

Nyumba ile imekuwa ya kupangisha kwa miaka zaidi ya 28 hadi leo tuna kazi zetu tunakula hela saafi kabisa hatukosi hela za vitumbuu ilhali alieijenga hayupo duniani

Real watakula wanao,wajukuu,vitukuu,vilembwe,vilembwekeze ,vining'ina.

Ni generational wealth
 
Ni biashara inayolipa yenye return nzuri for the years

It's a generational wealth .

Real estate will make u to reach your financial freedom surely.

Nyumba za kupanga zimenisomesha mimi toka vidudu hadi chuo

Dingi angu alijenga nyumba 1990 huko alifarikia kitambo sana hata shule nilikuwa sijaanza

Nyumba ile imekuwa ya kupangisha kwa miaka zaidi ya 28 hadi leo tuna kazi zetu tunakula hela saafi kabisa hatukosi hela za vitumbuu ilhali alieijenga hayupo duniani

Real watakula wanao,wajukuu,vitukuu,vilembwe,vilembwekeze ,vining'ina.

Ni generational wealth

Asante kwa ushuhuda wako rafiki yangu.
 
Mimi sina hela,ila nafkilia ninyanyue kq gorofa kwa ajiri ya kupangisa,niipige modogo mdogo
 
Mimi sina hela,ila nafkilia ninyanyue kq gorofa kwa ajiri ya kupangisa,niipige modogo mdogo

Hongera sana rafiki,

Jiunge na makundi yangu ya WhatsApp na Telegram ili upate nafasi ya kujifunza kwa ukaribu.

Karibu.
 
Kama umewahi pata hasara kuchukua muda wa kujifunza rafiki yangu.

Real estate inalipa hasa kwa ambao wapo makini na uwekezaji wao.

Kama umewahi pata hasara kuchukua muda wa kujifunza rafiki yangu.

Real estate inalipa hasa kwa ambao wapo makini na uwekezaji wao.
Ngoja nikusaidie kwa hili.
Iko hivi.
Ukiwa mfanyakaz biashara ni sawa kwako maana unajenga mdogo mdogo. Ila kama unafanya biashara na una target ya miaka 5=10 haifai. Coz tuseme umenunua kiwanja milion 50 na umejenga nyumba ya ml 70 ni 120 hiyo. Wewe unakuja kupangisha kwa laki 7. Ambayo ni ml 8.4 kwa mwaka. Ukiwa ni mfanyabiashara hiyo ni hasara full. Hiyo hiyo hela ukiingiza sokon kwa biashara yoyote kama uko smart kichwan kwa mwaka hukos ml mpaka mia 4 mpaka 5.
Mi nina nyumba 5 moja nalala na familia ila hiz nne ziko kibiashara. B4 nilikuwa napangisha ila baadae nikaona hasara yake nikabadili 3 zikawa airbnbn moja iki kariakoo ndio inalipa kwa kupangisha nyingine zote hasara kwa mtaji ulioingiza. Na ukae ukijua nyumba inapangishwa bei gali kutokana eneo au bei uliyonunulia kiwanja. Coz nyumba unayopangisha milion kwa mwez mikochen kwa mfano ikiwa sala sala utapangisha laki nne. Wewe hujajiuliza tu kwanini akina Mo Dewji hawafanyi hiyo biashara? Mzee Azam ndio kajenga Fumba Town juz juz tu. Ni kwamba return yake inachukua miaka mpaka 15. Sasa kwanini kama unajiamin usifanye biashara nyingine yenye return muda mfupi na wakat unajua nchi bado ni masikin sana wenye milion 200 tu ni wa kuokoteza so unaweza kufanya biashara nyingi bila ushindan na ndani ya mwaka miaka miwili uko poa. Sisem ucjenge au ucwekeze kwenye ujenz nachosema kwa kijana sio biashara labda uniambie umeamua kukaa hapo hapo ulipo. Kwanza ukiwa na mia tu ukaingia hapo Guanzhou miaka miwili tu tunakusahau. Usiogope maisha kias hicho chief. Kwasababu tu tumetoka familia masikin. Ni bora ununue viwanja vikae ila sio nyumba.
 
Ngoja nikusaidie kwa hili.
Iko hivi.
Ukiwa mfanyakaz biashara ni sawa kwako maana unajenga mdogo mdogo. Ila kama unafanya biashara na una target ya miaka 5=10 haifai. Coz tuseme umenunua kiwanja milion 50 na umejenga nyumba ya ml 70 ni 120 hiyo. Wewe unakuja kupangisha kwa laki 7. Ambayo ni ml 8.4 kwa mwaka. Ukiwa ni mfanyabiashara hiyo ni hasara full. Hiyo hiyo hela ukiingiza sokon kwa biashara yoyote kama uko smart kichwan kwa mwaka hukos ml mpaka mia 4 mpaka 5.
Mi nina nyumba 5 moja nalala na familia ila hiz nne ziko kibiashara. B4 nilikuwa napangisha ila baadae nikaona hasara yake nikabadili 3 zikawa airbnbn moja iki kariakoo ndio inalipa kwa kupangisha nyingine zote hasara kwa mtaji ulioingiza. Na ukae ukijua nyumba inapangishwa bei gali kutokana eneo au bei uliyonunulia kiwanja. Coz nyumba unayopangisha milion kwa mwez mikochen kwa mfano ikiwa sala sala utapangisha laki nne. Wewe hujajiuliza tu kwanini akina Mo Dewji hawafanyi hiyo biashara? Mzee Azam ndio kajenga Fumba Town juz juz tu. Ni kwamba return yake inachukua miaka mpaka 15. Sasa kwanini kama unajiamin usifanye biashara nyingine yenye return muda mfupi na wakat unajua nchi bado ni masikin sana wenye milion 200 tu ni wa kuokoteza so unaweza kufanya biashara nyingi bila ushindan na ndani ya mwaka miaka miwili uko poa. Sisem ucjenge au ucwekeze kwenye ujenz nachosema kwa kijana sio biashara labda uniambie umeamua kukaa hapo hapo ulipo. Kwanza ukiwa na mia tu ukaingia hapo Guanzhou miaka miwili tu tunakusahau. Usiogope maisha kias hicho chief. Kwasababu tu tumetoka familia masikin. Ni bora ununue viwanja vikae ila sio nyumba.

Sawa,

Nashukuru sana kwa ushuhuda.

Karibu tena.
 
Biashara ya kujenga nyumba ya kupanga ni nzuli sana lkn pesa inarudi taratibu sana, yaaani unakuja kuirudisha pesa yako baada ya miaka 10 tofauti na biashara nyingine, mjamaa amejenga nyumba yenye dhamani ya milion 70 hapo kuanzia kununua kiwanja mpaka nyumba kukamilika, amenga vyumba 3 , chamba cha kwanza anapangisha 200000 kwa mwezi kutokana na jinsi kilivyo maana kina mlango mmjo lkn kwa ndani kuna vyumba viwili vya kulala ,sebule jiko na choo, unalipia laki 2 kwa kila mwezi, chumba cha pili unalipa 150000 kwa mwezi hiki kipo chumba na sebule choo na jiko na .cha tatu unalipia laki, kila chumba kina mita yake ya umeme ,ukija piga hesabu kwa mwezi anaingiza 450000 (laki 4 na nusu ) sasa mpaka aipate milion 70 itachukua miaka mingapi?, hii sio biashara ya kufanya urudishe pesa ili ufanya biashara nyingine, mfano mioni 70 ukanunua hata dala dala ambayo kwa kila cku inakuingizia laki ndani ya mwezi hukosi milioni 2 ambapo kwa mwaka hukosi milioni 20,ndani ya miaka 3 pesa yako imerudi unakwenda kufungua biashara nyingine
 
Ngoja nikusaidie kwa hili.
Iko hivi.
Ukiwa mfanyakaz biashara ni sawa kwako maana unajenga mdogo mdogo. Ila kama unafanya biashara na una target ya miaka 5=10 haifai. Coz tuseme umenunua kiwanja milion 50 na umejenga nyumba ya ml 70 ni 120 hiyo. Wewe unakuja kupangisha kwa laki 7. Ambayo ni ml 8.4 kwa mwaka. Ukiwa ni mfanyabiashara hiyo ni hasara full. Hiyo hiyo hela ukiingiza sokon kwa biashara yoyote kama uko smart kichwan kwa mwaka hukos ml mpaka mia 4 mpaka 5.
Mi nina nyumba 5 moja nalala na familia ila hiz nne ziko kibiashara. B4 nilikuwa napangisha ila baadae nikaona hasara yake nikabadili 3 zikawa airbnbn moja iki kariakoo ndio inalipa kwa kupangisha nyingine zote hasara kwa mtaji ulioingiza. Na ukae ukijua nyumba inapangishwa bei gali kutokana eneo au bei uliyonunulia kiwanja. Coz nyumba unayopangisha milion kwa mwez mikochen kwa mfano ikiwa sala sala utapangisha laki nne. Wewe hujajiuliza tu kwanini akina Mo Dewji hawafanyi hiyo biashara? Mzee Azam ndio kajenga Fumba Town juz juz tu. Ni kwamba return yake inachukua miaka mpaka 15. Sasa kwanini kama unajiamin usifanye biashara nyingine yenye return muda mfupi na wakat unajua nchi bado ni masikin sana wenye milion 200 tu ni wa kuokoteza so unaweza kufanya biashara nyingi bila ushindan na ndani ya mwaka miaka miwili uko poa. Sisem ucjenge au ucwekeze kwenye ujenz nachosema kwa kijana sio biashara labda uniambie umeamua kukaa hapo hapo ulipo. Kwanza ukiwa na mia tu ukaingia hapo Guanzhou miaka miwili tu tunakusahau. Usiogope maisha kias hicho chief. Kwasababu tu tumetoka familia masikin. Ni bora ununue viwanja vikae ila sio nyumba.
Well said mkuu.......

Umeandika kitu kikubwa na muhimu sana kulingana na maisha na mazingira ya sasa......
 
Biashara ya kujenga nyumba ya kupanga ni nzuli sana lkn pesa inarudi taratibu sana, yaaani unakuja kuirudisha pesa yako baada ya miaka 10 tofauti na biashara nyingine, mjamaa amejenga nyumba yenye dhamani ya milion 70 hapo kuanzia kununua kiwanja mpaka nyumba kukamilika, amenga vyumba 3 , chamba cha kwanza anapangisha 200000 kwa mwezi kutokana na jinsi kilivyo maana kina mlango mmjo lkn kwa ndani kuna vyumba viwili vya kulala ,sebule jiko na choo, unalipia laki 2 kwa kila mwezi, chumba cha pili unalipa 150000 kwa mwezi hiki kipo chumba na sebule choo na jiko na .cha tatu unalipia laki, kila chumba kina mita yake ya umeme ,ukija piga hesabu kwa mwezi anaingiza 450000 (laki 4 na nusu ) sasa mpaka aipate milion 70 itachukua miaka mingapi?, hii sio biashara ya kufanya urudishe pesa ili ufanya biashara nyingine, mfano mioni 70 ukanunua hata dala dala ambayo kwa kila cku inakuingizia laki ndani ya mwezi hukosi milioni 2 ambapo kwa mwaka hukosi milioni 20,ndani ya miaka 3 pesa yako imerudi unakwenda kufungua biashara nyingine
Hehe eti biashara ya daladala. Hizi hesabu za kwenye makaratasi hizi
 
Back
Top Bottom