Hii ndo mistari ya bongo fleva iliyoandikwa na mwanafunzi wakati akifanya mitihani ya kidato cha 4

Hakuna cha tatizo kubwa wala nini, mbona wenzao wengine waliopata four na zero hawakuandika matusi wala mistari ya bongo fleva? Bangi tu hizo!
 
Mingine hii hapa...Lol, its so bad actually

 
Hii ni insane kabisa hapa inabidi liwepo fundisho huyu nadhani kaingia kwenye record ya nacte
 
This is just sad; it is not even funny. Nilimsikiliza huyo nama nikajua tuna tatizo kuvwa zaidi.

not real sad mwanakijiji wanavuna walichopanda pale baraza akuna uozo mkubwa wa kugawa mitihani ,,,mchezo mchafu huyo mama akiwa mmoja wao na wanawapa watu kadhaa wakitoa maelekezo kiasi kadhaa
sasa mpaka ana fika fm4 ni mkubwa ameona upumbavu wakila siku wa barza hilo akaona kwa nini asiwape mistari tu wakafie nayo mbele ya safai unafikiri huyu mtoto kufanya hivyo mwisho wa maisha..nop...
HUYO MAMA ANATAKIWA ASEMA WAZI VYANZO VYA MITIHANI KUVUJA NA KWA NINI WATU WANAKUTWA WAMEANDIKA MAJIBU YANAFANANAA KAMA SI MICHEZO MICHAFU YA WALIMU
 
Mi najaribu kufikiria huyo mtoto yawezekana kiakili hayuko sawa!Miaka minne anavuna misari ya bongo fleva?

Wazazi tuwe makini na watoto wetu la sivyo tutakuwa na jamii ya mataahira!Natamani kumtia machoni huyo toto jinga!
 
Nafikiri angeweka wazi ni mwanafunzi gani wa shule ipi, na iwe ndo utaratibu wa kuwaanika wanafunzi wenye tabia kama hiyo!
Itasaidia hawa watoto wawe committed na wanachokifanya!
Hiyo bongo flava itamsaidia nini? Ni mara 100 angeweka sababu ya ugumu wa maisha uliosababishwa na magamba!
 
System nzima ya elimu Tanzania ni hovyo. Inasikitisha maana sijui Taifa linakoelekea..
 
Watoto wa kizazi cha utawala wa Kikwete hao
 
Kweli matumbo yanazaa, mwanamke akijifungua anaambiwa hongera mwaya urudie tena! Itry to imagine kama ni mwanangu sijui nitamfanya nini, haya huyo kaandika mistari ya bongo fleva, je huyu aliyeandika matusi kwenye mitihani yake yote saba,? wanafunzi hawa lazima wanajulikana, wasakwe wafikishwe kwenye vyombo vya sheria, its better ukaacha blank kuliko kutukana na kuandika bongo fleva, eti wazazi wangu wako level ya juu, nyooo!
 
kama mwalimu wake anavaa suruali kati kati ya makalio, unategemea nini.
 
hawa ndio watoto wetu tunaowahangaikia usiku na mchana ili wapate elimu ambayo tunaamini itawapa mwangaza na muongozo katika maisha yao ya badae wao wanafanya mambo haya laiti wangejua uchungu tuupatao wazazi walezi wao wasingalifanya mambo kama haya
halafu hawa ndio vijana tunaowategemea kuliendeleza taifa siku za usoni
ujinga na ushenzi mtupu hawa ndio wakati wa kusoma wao wanajitaidi kuandika mistari na kukaa nje ya nyumba za watu kupiga makelele ya kujaribisha mistari hivi hawajui kuwa ukitaka kuwa mwanamuziki mzuri lazima pia uwe na elimu na ufahamu wa mambo mbalimbali. inasikitisha sana
 
wadau wakubwa wa bongo fleva wana wajibu wa kuwaelimisha vijana na wanafunzi kuwa elimu ni muhimu katika fani ya sasa ya muziki/bongofleva. nashauri wizara iwachukulie hatua wanafunzi kama hawa. hata f4 alifika vipi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…