Hii ni Aibu kwa Serikali na TFF, Hongera Samatta kwa Kuwaumbua Wasiojali Wazalendo

Chakaza

JF-Expert Member
Joined
Mar 10, 2007
Posts
40,455
Reaction score
73,145
Kwa kweli picha iliyoonyeshwa na TFF na Serikali katika kuthamini mchango wa wachezaji wa Stars katika kutuletea furaha Watanzania ni kuwa hata yaliyofanywa na Kamati eti ya hamasa ni kutafuta sifa binafsi na kutumia nguvu na uvumilivu wa vijana hawa kujijenga kisiasa tuu lakini sio kwa nia njema.

Iweje wamsahau kijana Shomari Kapombe? Kijana kapigana michezo yote ya awali hadi kuumia mazoezini Afrika Kusini na bado katika orodha ya zawadi anasahaulika?

Yaani kweli mpaka Kapteni wa Taifa Stars Mbwana Samatta anaamua kugawana zawadi zake na mchezaji wake ni AIBU ILIOJE? Ina maana hata TFF haijui Kapombe kafanya nini? mbona kuna wachezaji wengine wameongezwa mechi ya mwisho na pengine hawakucheza kabisa lakini wamelamba zawadi na kuachwa mpiganaji aliyeumia akiwa vitani?

Haya yote yametokana na kuingiza kamati za kisiasa na upigaji hela tuu, huwezi kusema Jina la Kapombe wamesahau kwa bahati mbaya bali nikuwa walikuwa hawajui kabisa yuko wapi na pengine hata matibabu yana hudumiwa na Club yake pekee.

Hongera Samatta kwa kuwaumbua hawa wababaishaji wanaongojea wengine wamenyeke wao waje kujibebea sifa za bure.

 
Hao watu huwa hawaumbuki, kwani hawana haya wala hawaoni vibaya kuwafanyia wengine mambo mabaya!!
Subiri Setikali ya watu wako wafanye unayoamini ila tunachoshudia hao unaowashadidia ni matendo ya kutia kinyaa maana ubinafsi kwa kwenda mbele. Km ni Mbunge lakini muda mrefu yupo Dar akiilalamikia Serikali kudai demokrasia ili awe na uhuru usio na mipaka na haki bila kuwajibija.

Watanzania wa leo siyo wa jana wakujazana viwanjani kuwasikiliza wanasiasa majukwaani wakitoa ahadi hewa.

Serikali ya CCM iliyoko madarakani kwa sasa imejipambanua kwa utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi bila ajizi. Tunashuhudia viongozi wa Chama na Serikali wanazunguka kila kona ya nchi kutathmini kiwango cha utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mmh hakika sijaelewa umeandika nini naona tu CCM, au lugha iliyotumika ni ngumu au hujielewi unakurupuka tu?
 
Mmh hakika sijaelewa umeandika nini naona tu CCM, au lugha iliyotumika ni ngumu au hujielewi unakurupuka tu?
Yaelekea bado una kasumba ya kumsujudu mtu badala ya kile unachoamini mwenyewe. Katika hali hiyo hutoweza kunielewa

Hutoweza kuelewa kwa sababu kichwani mwako umejaza chuki dhidi ya utawala wa sheria.

Enzi za WaTz kufanya watakavyo kana kwamba Serikali imeenda likizo zimepitwa na wakati.

Nyakati ambapo wanasiasa waliamini majukwaa ndiyo njia sahihi ya kuonesha umaarufu wao si wakati huu wa TEHEMA.

JIFIKIRISHE ZAIDI HUENDA UKAJITAMBUA kwa kujiondoa ndani ya kisanduku cha fikra tegemezi ili uone na kufaidi Tanzania mpya.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
K Vant asubuhi asubuhi ni hatari!
 
We hamnazo maana si kwa ukurupukaji huu na mapumba unayomwaga.
 
Hii issue naona upinzani mnaikuza kama nae huyo alivyoikuza..

Mjibu hili.. kwa list ya majina yanayobidi apewe Waziri Mkuu.. huyo jina lake halimo? Au wapi TFF wamenena hawataki kumuweka?

Samatta kuandikia mtandaoni.. angeeleza kama alitumia njia ingine kuwaambia wakamkatalua.. ila kama ulikuwa mwanzo wa kuwakumbusha.. amechemsha.

Pili tuwaombee hao wachezahi na TFF haswa wasiweke utapeli.. wajue JPM atajua yote.

Wawe makini na kutoruhusu pesa na mali zikaleta majanga kabla..
 
Mbwana has sense of fair play in and out of pitch.Mungu akuzudishie mema.
 
Aisee huoni aibu? Unalazimisha watu waamini kile ulicholishwa? Matango porii...hata kama unapenda kusifia sio kwa kiwango hicho cha undezi
 
Hii kitu TFF haikuwa makini na serikali ikadandia kwa mbele kutaka sifa za kuonyesha wao ndio wamefanikisha kwa kutumia ile kamati uchwara
 
Mzee wa kukurupuka habari za sikunyingi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Unaongea nini ww? Nenda taifa kashuhudie yanayotokea kati ya polisi na chama cha siasa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…