MIXOLOGIST
JF-Expert Member
- Mar 1, 2016
- 14,311
- 36,056
Habari za jioni wana JF
Imetokea nikapata tafakari (reminisce) utamu wa maisha yetu ya kale. Pale ambapo ulikua unajiandaa kwenda shule asubuhi, kwa mbaali unasikia kipindi cha "mazungumzo baada ya habari" kikiendeshwa na Marehemu David Wakati.
Unachukua begi lako pamoja na ufagio wako wa chelewa mdogo mdogo mpaka shuleni. Unakutana na mchaka mchaka wenye nyimbo za kumponda adui nduli Idd Amini. Break ya saa nne unapata vipande vyako vya miogo na chachandu unashushia na maji ya bomba.
Mzaha wa darasani unaendelea mpaka kengele ya saa nane amabapo kinapigwa kipute cha mpira wa makaratasi au kitenesi au gozi magoli madogo au one touch mpaka mtakapo muuzi mwenye mpira basi game inaisha.
Straight home umechafuka kama zombie, unachezea vitasa kwa kuchelewa, kupoteza peni na kuchafuka. Baada ya drama zote hizo, una chill unapiga msosi huku ukisikiliza kipindi cha MIKINGAMO.
Wahenga wenzangu mtaongezea utamu
Imetokea nikapata tafakari (reminisce) utamu wa maisha yetu ya kale. Pale ambapo ulikua unajiandaa kwenda shule asubuhi, kwa mbaali unasikia kipindi cha "mazungumzo baada ya habari" kikiendeshwa na Marehemu David Wakati.
Unachukua begi lako pamoja na ufagio wako wa chelewa mdogo mdogo mpaka shuleni. Unakutana na mchaka mchaka wenye nyimbo za kumponda adui nduli Idd Amini. Break ya saa nne unapata vipande vyako vya miogo na chachandu unashushia na maji ya bomba.
Mzaha wa darasani unaendelea mpaka kengele ya saa nane amabapo kinapigwa kipute cha mpira wa makaratasi au kitenesi au gozi magoli madogo au one touch mpaka mtakapo muuzi mwenye mpira basi game inaisha.
Straight home umechafuka kama zombie, unachezea vitasa kwa kuchelewa, kupoteza peni na kuchafuka. Baada ya drama zote hizo, una chill unapiga msosi huku ukisikiliza kipindi cha MIKINGAMO.
Wahenga wenzangu mtaongezea utamu