Hii ni katiba ya Watanzania au ya CCM/CDM?

Lilambo

JF-Expert Member
Joined
Jun 5, 2013
Posts
2,523
Reaction score
207
Watanzania wenzangu kwa sasa tupo katika mchakato wa katiba mpya. Lakini kwa muono wangu nadhani katiba hii siyo ya watanzania kama tunavyotaraji. Katiba hii kwa sasa inatawaliwa na vyama vikuu viwili vya siasa yaani Chadema na CCM kupitia hii kitu wanayoita mabaraza ya katiba ya chadema au mabaraza ya CCM. Vyama hivi vimekuwa vikiwahubiria watanznia maoni ambayo yana maslahi kwa chama husika katika mikutano na vikao vyao, mwisho ndiyo hualika watu wachache kutoa maoni. Kwa hali hii inaandaliwa katiba ya ccm/cdm na siyo watanznia. Pia kumekuwa na kampeni ya kutuma maoni kupitia mabaraza mbalimbali ya vyama hivi. Swali ni je, maoni haya tunayoyatuma katika vyama hivi hayawezi kuchakachuliwa? Kuna teknolojia gani inayotumika, ambapo kama mtz nikituma pale ccm maoni yng yatafika pasipo kuchakachuliwa? Ilikuwa ni vyema Tume ikapita kwa watanzania na si haya mabaraza ya ccm/cdm. Mfano tazama suala la muungano, CCM wanataka serikali 2 kwa kutazama maslahi na kuwashawishi watu kukubali Chadema nao wanaamini serikali 3 ni daraja la kuwaweka Magogoni hivyo wamekuwa wakihubiri. Watanzania wenzangu tusikubali kuyumbishwa na wanasiasa tuangalie mambo yatakayotusaidia watu wa hali ya chini. Tuache kushabikia maoni ya vyama vya siasa yenye lengo la kubeba maslahi ya vyama vyao.
 
Mkuu,

Umenena vyema kabisa, kwanza ieleweke wazi kuwa CHADEMA imevalia njuga suala la katiba kwa imani kwamba katiba mpya ndio jibu lao kwenda Ikulu.

Nadhani wananchi tuwe makini sana na ushawishi wanaotupa hawa waganga njaa (CHADEMA), ni ukweli ulio wazi kuwa wana hamu sana ya kwenda Ikulu, ila njaa yao hiyo kamwe haiwezi kushindana na akili ya watanzania, watanzania wamehamua kupata katiba mpya sio kwa kuiwezesha CHADEMA kuingia Ikulu, bali ni katika kujichagulia namna ambavyo tunataka kuendesha nchi yetu, kuanzia mambo ya kiuongozi, utoaji haki na mifumo ya uwakilishi n.k, ndio dhumuni kuu hili na CCM inajua hivyo.
 
Tume ya Warioba siyo ya Chadema. Iko kwa mujibu wa sheria. Lakini baada ya kutoa Rasimu ya Katiba ambayo Warioba anasemanimetokana na maoni ya wananchi, CCM inapingana nayo. Je, CCM inapingana na maoni ya wananchi kwanini? Ungesema kuwa hii katiba ya wananchi CCM inataka iwe kama ya kwao.
 
Chadema lazima wajue kwamba sisi Watanzania tumeshatoa maoni yetu na mabaraza ya wilaya yanaelekea mwisho na kwamba Serikali tatu hatutaki, na pia hatuwezi kukubali kutumiwa na kikundi cha watu wachache kwa faida yao.
Hawa watu(chadema) ni wafanyabiashara wanasaka masoko.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…