Hii ni kwa wana kiswahili !

Hii ni kwa wana kiswahili !

JIMMY JORAM

Member
Joined
May 1, 2013
Posts
38
Reaction score
20
Naomba msaada wa majibu kuhusu hili swali! "Ufanano kati ya fonetiki na fonolojia."
 
1.Yote ni matawi ya isimu
2.Tafuta kitabu cha "mtaala wa isimu" cha Mgullu.
Unasoma wap wewe?
 
ni Kiswahili mkuu! wanaosomea Kiswahili vyuoni husoma 'kwa Kiswahili', hawasomi 'kiswahili'
Lilendi ubuheri mkuu; Ahsant kunijuza, still sijakuelewa.... kama siusumbufu kwako iwe lugha simple wengi tuchangie!! Best of luck.
 
Lilendi ubuheri mkuu; Ahsant kunijuza, still sijakuelewa.... kama siusumbufu kwako iwe lugha simple wengi tuchangie!! Best of luck.

Mi bukheri kabisa! usijali. ni hivi, lugha ni sayansi na hii sayansi haichagui lugha. sayansi inayotumika kuiangalia lugha ya kiingereza ndo inayotumika kuziangalia lugha zingine. kupitia sayansi hii unaweza kujua tofauti zilizopo kati ya lugha moja na nyingine katika Nyanja mbalimbali; ikiwemo isimu. hata lugha mama yako inaweza kuchunguzwa kisayansi pia tukaona ulingano wa Kiswahili na lugha yako(kama lugha mama yako sio Kiswahili) ninaposema wanasoma kwa Kiswahili ni kwamba wanatumia kanuni za sayansi ya lugha kukichambua Kiswahili kwenye matawi mbalimbali ya lugha. hata fasihi inasomwa kwa Kiswahili. dhana zilizomo kwenye fasihi zinaweza tolewa kwa Kiswahili, kiingereza, kichina, n.k kama nimekuchanganya pole ndg huenda nikawa bora mwalimu. karibu kwa ufafanuzi zaidi.
 
Mi bukheri kabisa! usijali. ni hivi, lugha ni sayansi na hii sayansi haichagui lugha. sayansi inayotumika kuiangalia lugha ya kiingereza ndo inayotumika kuziangalia lugha zingine. kupitia sayansi hii unaweza kujua tofauti zilizopo kati ya lugha moja na nyingine katika Nyanja mbalimbali; ikiwemo isimu. hata lugha mama yako inaweza kuchunguzwa kisayansi pia tukaona ulingano wa Kiswahili na lugha yako(kama lugha mama yako sio Kiswahili) ninaposema wanasoma kwa Kiswahili ni kwamba wanatumia kanuni za sayansi ya lugha kukichambua Kiswahili kwenye matawi mbalimbali ya lugha. hata fasihi inasomwa kwa Kiswahili. dhana zilizomo kwenye fasihi zinaweza tolewa kwa Kiswahili, kiingereza, kichina, n.k kama nimekuchanganya pole ndg huenda nikawa bora mwalimu. karibu kwa ufafanuzi zaidi.
Indeed; lugha change na lugha kongwe zinaburuzwa kuchambuliwa na lugha ya kiSayansi ambayo ndiyo endelevu!! au siyo? Ok principal za Sayansi, Madamu misingi ya elimu za juu na vigezo vinaeleweka kilugha stahiki. Nitajifunza kwa makini lugha siku baada ya siku... Ubarikiwe Mkuu
 
Indeed; lugha change na lugha kongwe zinaburuzwa kuchambuliwa na lugha ya kiSayansi ambayo ndiyo endelevu!! au siyo? Ok principal za Sayansi, Madamu misingi ya elimu za juu na vigezo vinaeleweka kilugha stahiki. Nitajifunza kwa makini lugha siku baada ya siku... Ubarikiwe Mkuu

bold: naomba nitoe maelezo machache kidogo: hatuzungumzii lugha ya kisayansi (scientific language) bali sayansi ya lugha (the science of language) ( sayansi inayoichambua lugha bila kujali uchanga au ukongwe wake). penye nia pana njia. naamini utafanikiwa kukijua Kiswahili. ukiifahamu lugha husika inakuwa rahisi kuichambua hiyo kwa kutumia sayansi ya lugha. nawe ubarikiwe pia!
 
Back
Top Bottom