DOKEZO Hii 'Night Club' iliyojengwa kwenye eneo la hifadhi ya Mto Kanoni - Bukoba, sio salama kwa Watu, nani ametoa vibali?

DOKEZO Hii 'Night Club' iliyojengwa kwenye eneo la hifadhi ya Mto Kanoni - Bukoba, sio salama kwa Watu, nani ametoa vibali?

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

informer 06

Member
Joined
May 11, 2024
Posts
66
Reaction score
49
Uwepo wa Ukumbi wa muziki ambap pia una baa ndani yake (Night Club & Bar) uliopo kwenye eneo la Hifadhi ya Mto Kanoni ni jambo ambalo inaonekana kama mamlaka husika zinazotoa vibali vya ujenzi limefumbia macho wakati uhalisia eneo hilo linaonekana sio salama kwa Watu.
IMG_0204.jpeg
Awali katika eneo hilo kulijengwa baa lakini baada ya muda ikazuiwa kutokana na kubainika ujenzi ulivuka mipaka kwa kuingilia eneo la hifadhi ya Mto huo.

Katika mazingira hayo ambayo yanaibua maswali juu ya uwajibikaji wa mamlaka husika zinazotoa vibali, imekuwaje tena eneo hilo ikajengwa club ambapo miundombinu ya kuta imefika kabisa kwenye kingo za Mto!

Hata hivyo ujenzi huo umefanyika ikiwa kuna kibao kinachoonesha na kutoa marufuku na tahadhari kwa Mtu yeyote kutofanya shughuli zozote za kibinadamu eneo hilo.
IMG_0206.jpeg
IMG_0203.jpeg

Sasa najiuliza, mhusika ambaye ameratibu ujenzi huo yupo juu ya Sheria? Kwanini anakingiwa kifua au mbuyu umezungukwa?

Wito wangu kwa mamlaka husika zinazotoa vibali ikiwemo NEMC lakini pia TAKUKURU wafuatilie suala hilo na kuchukua hatua za haraka.

Ikizingatiwa kwa mara kadhaa katika eneo hilo la Mto Kanoni kumekuwa kukitokea mafuriko ambayo yanasababisha athari mbalimbali kwa wananchi walioko maeneo ya karibu.
IMG_0205.jpeg
Kwani pamoja na jengo hilo kuwa hapo, ikumbukwe kuwa kumekuwepo na mpango wa uboreshaji wa kingo za Mto Kanoni kupitia Miradi ya Kupendezesha Miji (TACTIC) Manispaa ya Bukoba, hivyo uwepo wa sehemu hiyo ya starehe inawezekana ikawa kikwazo kwa mradi.

Inadaiwa jengo hilo linamilikiwa na Mwenyekiti wa CCM Bukoba Mjini, Muganyizi Zachwa kama ni hivyo kweli basi yeye anatakiwa kutafakari na kufikiria usalama wa watu wengi wanaofika eneo hilo kwa ajili ya kuburudika.
IMG_0207.jpeg
 
Uwepo wa Ukumbi wa muziki ambap pia una baa ndani yake (Night Club & Bar) uliopo kwenye eneo la Hifadhi ya Mto Kanoni ni jambo ambalo inaonekana kama mamlaka husika zinazotoa vibali vya ujenzi limefumbia macho wakati uhalisia eneo hilo linaonekana sio salama kwa Watu.
Awali katika eneo hilo kulijengwa baa lakini baada ya muda ikazuiwa kutokana na kubainika ujenzi ulivuka mipaka kwa kuingilia eneo la hifadhi ya Mto huo.

Katika mazingira hayo ambayo yanaibua maswali juu ya uwajibikaji wa mamlaka husika zinazotoa vibali, imekuwaje tena eneo hilo ikajengwa club ambapo miundombinu ya kuta imefika kabisa kwenye kingo za Mto!

Hata hivyo ujenzi huo umefanyika ikiwa kuna kibao kinachoonesha na kutoa marufuku na tahadhari kwa Mtu yeyote kutofanya shughuli zozote za kibinadamu eneo hilo.
View attachment 3193847
Sasa najiuliza, mhusika ambaye ameratibu ujenzi huo yupo juu ya Sheria? Kwanini anakingiwa kifua au mbuyu umezungukwa?

Wito wangu kwa mamlaka husika zinazotoa vibali ikiwemo NEMC lakini pia TAKUKURU wafuatilie suala hilo na kuchukua hatua za haraka.

Ikizingatiwa kwa mara kadhaa katika eneo hilo la Mto Kanoni kumekuwa kukitokea mafuriko ambayo yanasababisha athari mbalimbali kwa wananchi walioko maeneo ya karibu.
Kwani pamoja na jengo hilo kuwa hapo, ikumbukwe kuwa kumekuwepo na mpango wa uboreshaji wa kingo za Mto Kanoni kupitia Miradi ya Kupendezesha Miji (TACTIC) Manispaa ya Bukoba, hivyo uwepo wa sehemu hiyo ya starehe inawezekana ikawa kikwazo kwa mradi.

Inadaiwa jengo hilo linamilikiwa na Mwenyekiti wa CCM Bukoba Mjini, Muganyizi Zachwa kama ni hivyo kweli basi yeye anatakiwa kutafakari na kufikiria usalama wa watu wengi wanaofika eneo hilo kwa ajili ya kuburudika.
CCM ni chama cha wala rushwa. Nadhani umepata jawabu sahihi. CCM ni mfumo rasmi na halisi ambao umeruhisu rushwa ndiyo maana hata Takukuru hawafanyi uchunguzi wowote wa rushwa kubwa bila agizo la Waziri Mkuu, na kila uchunguzi ripoti zàke zinakomea kwa mkuu, hazifiki popote.

Wewe piga kelele wewe wanakuchora tu. Hapo mpunga umetembea kuanzia serikali ya mtaa hadi mkoa.
 
Uwepo wa Ukumbi wa muziki ambap pia una baa ndani yake (Night Club & Bar) uliopo kwenye eneo la Hifadhi ya Mto Kanoni ni jambo ambalo inaonekana kama mamlaka husika zinazotoa vibali vya ujenzi limefumbia macho wakati uhalisia eneo hilo linaonekana sio salama kwa Watu.
Awali katika eneo hilo kulijengwa baa lakini baada ya muda ikazuiwa kutokana na kubainika ujenzi ulivuka mipaka kwa kuingilia eneo la hifadhi ya Mto huo.

Katika mazingira hayo ambayo yanaibua maswali juu ya uwajibikaji wa mamlaka husika zinazotoa vibali, imekuwaje tena eneo hilo ikajengwa club ambapo miundombinu ya kuta imefika kabisa kwenye kingo za Mto!

Hata hivyo ujenzi huo umefanyika ikiwa kuna kibao kinachoonesha na kutoa marufuku na tahadhari kwa Mtu yeyote kutofanya shughuli zozote za kibinadamu eneo hilo.
View attachment 3193847
Sasa najiuliza, mhusika ambaye ameratibu ujenzi huo yupo juu ya Sheria? Kwanini anakingiwa kifua au mbuyu umezungukwa?

Wito wangu kwa mamlaka husika zinazotoa vibali ikiwemo NEMC lakini pia TAKUKURU wafuatilie suala hilo na kuchukua hatua za haraka.

Ikizingatiwa kwa mara kadhaa katika eneo hilo la Mto Kanoni kumekuwa kukitokea mafuriko ambayo yanasababisha athari mbalimbali kwa wananchi walioko maeneo ya karibu.
Kwani pamoja na jengo hilo kuwa hapo, ikumbukwe kuwa kumekuwepo na mpango wa uboreshaji wa kingo za Mto Kanoni kupitia Miradi ya Kupendezesha Miji (TACTIC) Manispaa ya Bukoba, hivyo uwepo wa sehemu hiyo ya starehe inawezekana ikawa kikwazo kwa mradi.

Inadaiwa jengo hilo linamilikiwa na Mwenyekiti wa CCM Bukoba Mjini, Muganyizi Zachwa kama ni hivyo kweli basi yeye anatakiwa kutafakari na kufikiria usalama wa watu wengi wanaofika eneo hilo kwa ajili ya kuburudika.
Jamani mengine yaache yqpite kwanza hangaikieni mambo ya msingi kama stand na solo kuu, hiyo night club iache kwanza
 
Hizi ni ngonjera tu. Ujio wa mradi wa Tactic katika eneo la mto kanoni yaani kujenga kingo maana yake ni kuondoa changamoto za mafuriko mjini Bukoba. Mto Kanoni unapita kwenye kata zaidi ya 7 ikiwemo Kagondo, Rwamishenye, Nshambya, Hamugembe, Bilele, Bakoba na Miembeni kati ya kata 14 zilizopo manispaa ya Bukoba. Hatuwezi kubomoa majumba ya watu kwa sababu mto huu tumeishi nao miaka yote, ujio wa mradi wa Tactic ni faraja kwetu kwa maana sasa hivi hatutakuwa na mawazo ya mafuriko. Alafu hiyo Club wala haijajengwa mtoni penyewe zipo hatua za kutosha tu kuruhusu mambo mengine kuendelea. Rio de Janeiro ni kisima cha burudani kwa sasa mkoani Kagera, na imekuwa changamoto kwa bara na clubs nyingine ndio maana hizi story zinaanza. Hapo ilipo Rio de Janeiro leo ilikuwepo Sky Motel mbona haya hatukuyasema? Kwa sbb kilichofanyika ni maboresho tu. Na kuwa mwenyekiti wa CCM isiwe sababu ya kumkatisha tamaa, kabla ya huo uenyekiti yeye ni mfanyabiashara wa muda mrefu katika tasnia ya burudani. Aungwe mkono, ashauriwe pale inapobidi na sio kutweza jitihada zake na za wawekezaji wengine.
Katika kipindi hiki ambacho Mkuu wa Mkoa wa Kagera Hajat Fatma Mwassa ameufungua mkoa kupitia jitihada mbalimbali anazozifanya na kupitia matamasha ya Ijuka Omuka ameendelea kuwakaribisha wawekezaji wa ndani na nje kuja Kagera kuona fursa zilizopo, hivyo serikali ya mkoa ishaandaa mazingira safi ya uwekezaji, hakuna tena longo longo, atakaye na aje na wengi wameonesha muitikio kuwekeza katika maeneo ya Viwanda, mahoteli, elimu na mengineyo hata Bilionea Mulokozi anakuja kuwekeza viwanda Kagera. Serikali inaendelea kuboresha miundombinu ikiwemo miradi mingine ya Tactic ni pamoja na Soko kubwa la Kisasa, stendi ya kisasa, barabara za lami, lakini wakati huo barabara ya njia nne inaendelea kujengwa kutokea round about ya Rwamishenye hadi round about ya mjini kati, ujenzi wa tawi la chuo kikuu cha Dar es Salaam unaendelea, mipango ya ujenzi wa airport ya Omukajunguti inaendelea vizuri pamoja na maboresho na ukarabati wa bandari za Bukoba na Kemondo kazi inaendelea kwa kasi ikiwa ni maandalizi ya kupokea meli ya Mv. Mwanza Hapa Kazi Tu.
Ahsante sana Mhe Rais wetu Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa miradi hii mikubwa ya maendeleo ambayo sasa inaufungua mkoa wetu na tunakushukuru kwa kutuletea RC Hajat Fatma Mwassa ambae ni mama mchapakazi, tangu amefika Kagera siku hizi hatujadili tena kwa nini tumashika mkia kwenye kila jambo bali tunajipongeza kwa kuwa wa kwanza kwenye mbio za Mwenge, kufanya vizuri kwenye uandikishaji na ametuleta pamoja Wanakagera kupitia tamasha aliloliasisi la Ijuka Omuka ambapo Wanakagera sasa wanatamani kurudi kuwekeza nyumbani, na wazee wa mkoa wa Kagera wamempa jina la Ma Kankiza na Ma Katalemwa. Make Kagera Great Again, bye bye Kitandugao.
 
Hizi ni ngonjera tu. Ujio wa mradi wa Tactic katika eneo la mto kanoni yaani kujenga kingo maana yake ni kuondoa changamoto za mafuriko mjini Bukoba. Mto Kanoni unapita kwenye kata zaidi ya 7 ikiwemo Kagondo, Rwamishenye, Nshambya, Hamugembe, Bilele, Bakoba na Miembeni kati ya kata 14 zilizopo manispaa ya Bukoba. Hatuwezi kubomoa majumba ya watu kwa sababu mto huu tumeishi nao miaka yote, ujio wa mradi wa Tactic ni faraja kwetu kwa maana sasa hivi hatutakuwa na mawazo ya mafuriko. Alafu hiyo Club wala haijajengwa mtoni penyewe zipo hatua za kutosha tu kuruhusu mambo mengine kuendelea. Rio de Janeiro ni kisima cha burudani kwa sasa mkoani Kagera, na imekuwa changamoto kwa bara na clubs nyingine ndio maana hizi story zinaanza. Hapo ilipo Rio de Janeiro leo ilikuwepo Sky Motel mbona haya hatukuyasema? Kwa sbb kilichofanyika ni maboresho tu. Na kuwa mwenyekiti wa CCM isiwe sababu ya kumkatisha tamaa, kabla ya huo uenyekiti yeye ni mfanyabiashara wa muda mrefu katika tasnia ya burudani. Aungwe mkono, ashauriwe pale inapobidi na sio kutweza jitihada zake na za wawekezaji wengine.
Katika kipindi hiki ambacho Mkuu wa Mkoa wa Kagera Hajat Fatma Mwassa ameufungua mkoa kupitia jitihada mbalimbali anazozifanya na kupitia matamasha ya Ijuka Omuka ameendelea kuwakaribisha wawekezaji wa ndani na nje kuja Kagera kuona fursa zilizopo, hivyo serikali ya mkoa ishaandaa mazingira safi ya uwekezaji, hakuna tena longo longo, atakaye na aje na wengi wameonesha muitikio kuwekeza katika maeneo ya Viwanda, mahoteli, elimu na mengineyo hata Bilionea Mulokozi anakuja kuwekeza viwanda Kagera. Serikali inaendelea kuboresha miundombinu ikiwemo miradi mingine ya Tactic ni pamoja na Soko kubwa la Kisasa, stendi ya kisasa, barabara za lami, lakini wakati huo barabara ya njia nne inaendelea kujengwa kutokea round about ya Rwamishenye hadi round about ya mjini kati, ujenzi wa tawi la chuo kikuu cha Dar es Salaam unaendelea, mipango ya ujenzi wa airport ya Omukajunguti inaendelea vizuri pamoja na maboresho na ukarabati wa bandari za Bukoba na Kemondo kazi inaendelea kwa kasi ikiwa ni maandalizi ya kupokea meli ya Mv. Mwanza Hapa Kazi Tu.
Ahsante sana Mhe Rais wetu Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa miradi hii mikubwa ya maendeleo ambayo sasa inaufungua mkoa wetu na tunakushukuru kwa kutuletea RC Hajat Fatma Mwassa ambae ni mama mchapakazi, tangu amefika Kagera siku hizi hatujadili tena kwa nini tumashika mkia kwenye kila jambo bali tunajipongeza kwa kuwa wa kwanza kwenye mbio za Mwenge, kufanya vizuri kwenye uandikishaji na ametuleta pamoja Wanakagera kupitia tamasha aliloliasisi la Ijuka Omuka ambapo Wanakagera sasa wanatamani kurudi kuwekeza nyumbani, na wazee wa mkoa wa Kagera wamempa jina la Ma Kankiza na Ma Katalemwa. Make Kagera Great Again, bye bye Kitandugao.
Mbona picha zinaonyesha kuna umbali kidogo sana kutoka mto ulipo hadi jengo lilipoanzia una uhakika mita60 zimefuatwa mkuu? Kwenye ndio tujifunzeni kusema ndio na hapana iwe hapana.
 
Mbona picha zinaonyesha kuna umbali kidogo sana kutoka mto ulipo hadi jengo lilipoanzia una uhakika mita60 zimefuatwa mkuu? Kwenye ndio tujifunzeni kusema ndio na hapana iwe hapana.
Mwaka 2014 wakati wa tathmini ya mradi wa LVEMP ilionekana nyumba zaidi ya 300 zipo ndani ya mita 60, unapata wapi fedha za kubomoa nyumba 300 ulipe fidia, sasa mradi wa Tactic ni mkombozi kwa kujenga kingo za mto bila kuhatarisha makazi ya watu walio wengi. Mradi utaangaliwa unahitaji mita ngapi, nimesema hapo zaidi ya kata 7 kati ya 14 zinapitiwa na mto kanoni kwa maana nyingine ukienda na suala la mita 60 makazi mengi ya watu utayaondoa. Tusifungwe na mazingira tulo nayo kufanya maendeleo. Kama wenzetu wanajenga majumba hadi chini ya bahari, na sisi lazima tubadilike.
 
Mwaka 2014 wakati wa tathmini ya mradi wa LVEMP ilionekana nyumba zaidi ya 300 zipo ndani ya mita 60, unapata wapi fedha za kubomoa nyumba 300 ulipe fidia, sasa mradi wa Tactic ni mkombozi kwa kujenga kingo za mto bila kuhatarisha makazi ya watu walio wengi. Mradi utaangaliwa unahitaji mita ngapi, nimesema hapo zaidi ya kata 7 kati ya 14 zinapitiwa na mto kanoni kwa maana nyingine ukienda na suala la mita 60 makazi mengi ya watu utayaondoa. Tusifungwe na mazingira tulo nayo kufanya maendeleo. Kama wenzetu wanajenga majumba hadi chini ya bahari, na sisi lazima tubadilike.
Eneo hilo silijui ila kwa maelezo ya mtoa uzi pamoja na picha inaonyesha wazi kuna uwalakini. Point yako ni mjema mkuu kuwa tusifungwe na m,azingira tuliyo nayo.....Mchawi ni ccm huyaacha hayo maeneo mita60 kwa kisingizio cha kutunza vya maji/mazingira mwisho wa wiki anapewa mwekezaji anaharibu zaidi
 
Uwepo wa Ukumbi wa muziki ambap pia una baa ndani yake (Night Club & Bar) uliopo kwenye eneo la Hifadhi ya Mto Kanoni ni jambo ambalo inaonekana kama mamlaka husika zinazotoa vibali vya ujenzi limefumbia macho wakati uhalisia eneo hilo linaonekana sio salama kwa Watu.
Awali katika eneo hilo kulijengwa baa lakini baada ya muda ikazuiwa kutokana na kubainika ujenzi ulivuka mipaka kwa kuingilia eneo la hifadhi ya Mto huo.

Katika mazingira hayo ambayo yanaibua maswali juu ya uwajibikaji wa mamlaka husika zinazotoa vibali, imekuwaje tena eneo hilo ikajengwa club ambapo miundombinu ya kuta imefika kabisa kwenye kingo za Mto!

Hata hivyo ujenzi huo umefanyika ikiwa kuna kibao kinachoonesha na kutoa marufuku na tahadhari kwa Mtu yeyote kutofanya shughuli zozote za kibinadamu eneo hilo.
View attachment 3193847
Sasa najiuliza, mhusika ambaye ameratibu ujenzi huo yupo juu ya Sheria? Kwanini anakingiwa kifua au mbuyu umezungukwa?

Wito wangu kwa mamlaka husika zinazotoa vibali ikiwemo NEMC lakini pia TAKUKURU wafuatilie suala hilo na kuchukua hatua za haraka.

Ikizingatiwa kwa mara kadhaa katika eneo hilo la Mto Kanoni kumekuwa kukitokea mafuriko ambayo yanasababisha athari mbalimbali kwa wananchi walioko maeneo ya karibu.
Kwani pamoja na jengo hilo kuwa hapo, ikumbukwe kuwa kumekuwepo na mpango wa uboreshaji wa kingo za Mto Kanoni kupitia Miradi ya Kupendezesha Miji (TACTIC) Manispaa ya Bukoba, hivyo uwepo wa sehemu hiyo ya starehe inawezekana ikawa kikwazo kwa mradi.

Inadaiwa jengo hilo linamilikiwa na Mwenyekiti wa CCM Bukoba Mjini, Muganyizi Zachwa kama ni hivyo kweli basi yeye anatakiwa kutafakari na kufikiria usalama wa watu wengi wanaofika eneo hilo kwa ajili ya kuburudika.
Huu ni umbea na unafiki wa kiwango cha lami, kwa sababu ujenzi wake umefanyika muda mrefu na wewe ulikuwepo. Sasa hivi ndo unapiga makelele au umezibiwa ridhiki??
 
Kwa Mbowe tuking'oa mchicha tukasema kwamba analima katika chanzo cha mto - huyu jamaa wanasema ni kigogo wa CCM yupo sahihi.

Tunywe mchuzi nyama tunazikaribia.
 
Back
Top Bottom