Kwenye airport moja huko Japan wameweka kioo kikuubwa, ukisimama mbele yake kinataja jina lako na nchi unayoelea.
Mpemba mmoja akasimama mbele ya kioo akaambiwa jina lake ni Awadh Mkufu Mbaruku na ndege yake inaelekea Zanzibar.
Mpemba alishangaa sana, akaona ngoja ahakikishe kama kioo hakikubahatisha. Akavua koti akavaa kanzu, kilemba na miwani. Akarudi tena mbele ya kioo akaambiwa jina lake ni Awadh Mkufu Mbaruku na ndege inaelekea Zanzibar.
Mpemba akaenda kuvua kanzu akavaa zawadi alizomnunulia mkewe. Akavaa night dress,akapaka rangi za midomo, akatafuna kungu na kulegeza mwili. Akarudi tena mbele ya kioo, akaambiwa,"Jina lako Awadh Mkufu Mbaruku na ndege yako ishakuacha kwa ukhanithi wako".