Hii ya Kenya kuwasaidia Sudan na Somalia imekaa vipi

Hii ya Kenya kuwasaidia Sudan na Somalia imekaa vipi

Silly

JF-Expert Member
Joined
Nov 4, 2010
Posts
569
Reaction score
180
Ninakunwa kidogo na fikra nazopenda kuziita fupi za viongozi wengine barani Africa. Siku za hivi karibuni ndugu zetu jirani zetu wa Kenya wamepata kushambuliwa na watu wengi kupoteza maisha na katika mashambulizi yote - kikundi cha Alshabab kimetamba kuhusika. Katika masharti yao - Alshabab wanataka Kenya iondoe wanajeshi wake Somalia kitu ambacho viongozi wa Kenya wametoka na kukataa katakata kwamba hawaondoki hadi pale Somalia itakuwa safi.

Hapa majuzi pia Sudan ya Kusini imeingia katika mgogoro wa vita vya wenyewe pande zote zikishikilia kuwa na haki flani flani. Napo pia tumeona viongozi wa Kenya wakijitokeza na kutaka kuisaidia Sudan ili amani ipatikane. Hivi hawa viongozi ambao imekuwa vigumu kwao kuwahakikishia raia wao usalama wa kutembea na kufanya mambo yao kwa amani itakuwa vipi wajihusishe na vita kwa jirani zao wakati kwao nyumba yao inaungua kwa mashambulizi ya magaidi na wahalifu wa ndani.

Na ni vpi yule mpiga kura aliyewapa kazi hao jamaa ataweza kusikika..naomba mwenye kuelewa diplomasia anifafanulie ili nipate elewa.
 
Ukitaka kumuua nyoka tafuta kilipo kichwa chake. Tofauti ya hapo atakutesa sana. Kwa kifupi ni haki kabisa ya Kenya kupambana na magaidi walioko Somalia na S. Sudan kwani kenya ina maslahi yake huko. Wakenya wengi mpaka mawaziri wana asili ya Somalia
 
Ninakunwa kidogo na fikra nazopenda kuziita fupi za viongozi wengine barani Africa. Siku za hivi karibuni ndugu zetu jirani zetu wa Kenya wamepata kushambuliwa na watu wengi kupoteza maisha na katika mashambulizi yote - kikundi cha Alshabab kimetamba kuhusika. Katika masharti yao - Alshabab wanataka Kenya iondoe wanajeshi wake Somalia kitu ambacho viongozi wa Kenya wametoka na kukataa katakata kwamba hawaondoki hadi pale Somalia itakuwa safi.

Hapa majuzi pia Sudan ya Kusini imeingia katika mgogoro wa vita vya wenyewe pande zote zikishikilia kuwa na haki flani flani. Napo pia tumeona viongozi wa Kenya wakijitokeza na kutaka kuisaidia Sudan ili amani ipatikane. Hivi hawa viongozi ambao imekuwa vigumu kwao kuwahakikishia raia wao usalama wa kutembea na kufanya mambo yao kwa amani itakuwa vipi wajihusishe na vita kwa jirani zao wakati kwao nyumba yao inaungua kwa mashambulizi ya magaidi na wahalifu wa ndani.

Na ni vpi yule mpiga kura aliyewapa kazi hao jamaa ataweza kusikika..naomba mwenye kuelewa diplomasia anifafanulie ili nipate elewa.

Nitakujibu mimi kama Mkenya. Vurugu Somalia zimechukua miaka 24, kwa muda huo wote tumeadhirika sana kiuchumi na kijamii maana walitorokea kwetu kwa mamilioni. Wengine wakaingia kwenye kambi za wakimbizi na kiasi kikubwa wakaingia mijini kiharamu. Silaha ndogo zikawa nyingi kwetu, pesa chafu (money laundering), wahamiaji haramu wasiolipa kodi, bidhaa haramu na mengine mengi. Sisi ikawa hatuwezi ingilia mgogoro wao, ila tuwe neutral na kuwawezesha kuitengeneza nchi yao upya.
Wakawa hawadhibitiki hawa, mabomu na risasi kwao kila uchao, Marekani, Ethiopia na wengine wengi wakajaribu kuingilia lakini wapi.
Jamaa tulijaribu sana kuwalea hadi hata wakapigia rais wao kura wakiwa Kenya hapa. Alshabaab walipoibuka, wakavurugana wenyewe kwa wenyewe bila sisi kujihusisha.
Tatizo likaanza pale Alshabaab walipoanza kutuchokonoa, waliwateka watalii wetu, wakateka meli zilizoleta bidhaa EAC, Tanzania ikiwemo, wakawateka afisa wetu na mengine kadhaa. Ikawa sasa lazima kieleweke, jeshi letu shupavu na imara likaingia Somalia tena kwa vitisho na kuwafyeka jamaa. Wasomali walipenda sana jeshi letu maana humo ndani kuna wanajeshi wengi wenye asilia za Kisomali na walishirikiana sana na jamii maana walielewena kilugha na hata kidini tofauti na Wamarekani, Waethiopia na Waganda. Hili limewachukiza sana Alshabaab maana ndo unaona bali na kuwa kuna majeshi tokea nchi zingine huko, wao wamekomalia tu KDF waondoke.

Sudan, hata sijui hapa nianzie wapi, soma historia ya jinsi tumehusika kuwalea hadi wakajenga nchi mpya, sasa ndio hao wanachinjana kama kuku. Itabidi tuingilie kati na hata kwa fujo na nguvu za kijeshi, hatutaruhusu majanga kama ya Rwanda.
 
Nitakujibu mimi kama Mkenya. Vurugu Somalia zimechukua miaka 24, kwa muda huo wote tumeadhirika sana kiuchumi na kijamii maana walitorokea kwetu kwa mamilioni. Wengine wakaingia kwenye kambi za wakimbizi na kiasi kikubwa wakaingia mijini kiharamu. Silaha ndogo zikawa nyingi kwetu, pesa chafu (money laundering), wahamiaji haramu wasiolipa kodi, bidhaa haramu na mengine mengi. Sisi ikawa hatuwezi ingilia mgogoro wao, ila tuwe neutral na kuwawezesha kuitengeneza nchi yao upya.
Wakawa hawadhibitiki hawa, mabomu na risasi kwao kila uchao, Marekani, Ethiopia na wengine wengi wakajaribu kuingilia lakini wapi.
Jamaa tulijaribu sana kuwalea hadi hata wakapigia rais wao kura wakiwa Kenya hapa. Alshabaab walipoibuka, wakavurugana wenyewe kwa wenyewe bila sisi kujihusisha.
Tatizo likaanza pale Alshabaab walipoanza kutuchokonoa, waliwateka watalii wetu, wakateka meli zilizoleta bidhaa EAC, Tanzania ikiwemo, wakawateka afisa wetu na mengine kadhaa. Ikawa sasa lazima kieleweke, jeshi letu shupavu na imara likaingia Somalia tena kwa vitisho na kuwafyeka jamaa. Wasomali walipenda sana jeshi letu maana humo ndani kuna wanajeshi wengi wenye asilia za Kisomali na walishirikiana sana na jamii maana walielewena kilugha na hata kidini tofauti na Wamarekani, Waethiopia na Waganda. Hili limewachukiza sana Alshabaab maana ndo unaona bali na kuwa kuna majeshi tokea nchi zingine huko, wao wamekomalia tu KDF waondoke.

Sudan, hata sijui hapa nianzie wapi, soma historia ya jinsi tumehusika kuwalea hadi wakajenga nchi mpya, sasa ndio hao wanachinjana kama kuku. Itabidi tuingilie kati na hata kwa fujo na nguvu za kijeshi, hatutaruhusu majanga kama ya Rwanda.
Mkuu umetoa historia nzuri tu, lakini kinachonisumbua ni viongozi wa Kenya kwenda kwenye majukwaa na kujigamba huku wakijua vema ni kama kuongeza petroli kwa moto ambao tayari umekolea. kinachojitokeza kwa sasa ni mashambulizi yanayotokea ndani ya nchi - Kenya na kwa mifano tofauti, ina maana wanaoguswa zaidi ni wale wananchi wa kawaida, tumeshuhudia wasafiri wakipigwa na bomu na pia wengine wakiwa kwenye starehe na shopping. Kwa mazingira yale wanaopata shida ni raia wa kawaida, maana viongozi hawatumii vile vyombo. Pia nadhan kazi ya wana intelijensia ni pana zaidi lakini kwa staili hii ya kila sikubomu la muundo wa tofauti, lazma wajipange na kuwahusisha wananchi maana ndio wana nafasi nzuri zaidi kushinda hao ma intelijensia wanaotumia hela za walipa kodi wakati mabomu yanaendelea kulipuka
 
Mimi kama m-Tz nimesikia mengi kuhusu yanayowasibu jirani kweli Kenya imewasidia sana Somalia pia kutaka wawe na amani katika nchi yao, kupeleka majeshi ili kuteketeza Al shabab sio suluhu kabisa kwani Al shabab vita yao ni tofauti wanatega Bomu na kukimbia au kujilipua, vita ambayo nchi nyingi duniani yapo. Ni vita isiyowezekana.
Sasa twende upande mwingine Kenya wakati wa uchaguzi kulitokea mauwaji mengi ambapo mpaka sasa kesi ipo The Hague. Je waliopoteza maisha hao ndugu zao na walio against the government hawawezi fanya unyama huo wakijua hata tukilipua kila mahali bado serikali ina sikio moja na jicho moja tu AL SHABAAAB. Kwa hiyo wataendelea kukamata innocent ppl na kuendelea kuongeza nguvu Somalia na kuzidi kuporomosha uchumi wa nchi, hivyo basi serikali iangalie maadui ni nani kwa kila aina ya watu bila kukurupuka, natumaini muelewa ataelewa
 
Ukitaka kumuua nyoka tafuta kilipo kichwa chake. Tofauti ya hapo atakutesa sana. Kwa kifupi ni haki kabisa ya Kenya kupambana na magaidi walioko Somalia na S. Sudan kwani kenya ina maslahi yake huko. Wakenya wengi mpaka mawaziri wana asili ya Somalia

ha ha ha ha ha Arushaone umenikumbusha msemo wa mabosi wa MOSSAD ukitaka kuua nyoka piga kichwa basi na nadhani ndicho wanachokifanya kwenya kule somalia ingawa naona kama kichwa kinazinduka zinduka na tumabomu tunalipuka lipuka kenya
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom