demigod
JF-Expert Member
- Jan 2, 2015
- 8,292
- 15,250
Walianza Berkane. Wakafanya umafia wao kwa Adebayor.
Wakafuata Yanga SC. Wakafanya umafia wao Kwa Aziz KI.
Akaja Rais wa Vipers SC akafanikiwa kuwabania Ceaser Nzoki. Hata ikawafanya waende Nigeria kum’beba OKRAH.
Kocha Stuart naye amewakataa kwa kigezo cha kushindwa kumuweka wazi kiasi cha bajeti ya usajili cha klabu kwa dirisha hili.
Nasikia hata huyo Sylla wa Horoya nae huenda wakamkosa kwa sababu wako kwenye ushindani na kigogo mmoja wa kaskazini huko.
Leo hii nao watoto wadogo wa mjini aka walima Alizeti wamefanikiwa kuingilia kati mazungumzo ya Habibu Kyombo na kufanikisha usajili wake.
Inasemekana kuwa Simba SC walikuwa wanapanga kumpa mchezaji huyo dau dogo kwakuwa alikuwa free agent na pili hakuwa akihitajika na timu nyingine kubwa ya hapa nchini.
Hizo taarifa zikasambaa si tu miongoni mwa watu wa karibu na Kyombo bali pia hata zikamfikia yule Mbunge aliyemsajilisha Fei Toto pale Singida United (Enzi hizo).
Huyo bwana baada ya kupata taarifa hizo akapandisha dau nono kwa mchezaji kama signing fee yake pia akamuahidi mshahara mnono ambao Simba SC hawakuwa tayari kumlipa.
Dogo akatamanika na akizingatia ana vina saba na U’yanga akaona asihangaike kwenda kuichezea timu ambayo hana mapenzi nayo ya dhati kutoka moyoni kwa ujira mdogo.
Msimu huu hawa jamaa wamechanganyikiwa mno.
Siamini na wala sitaki kuamini ninachoona kinaendelea kwenye kambi yao.
Wakafuata Yanga SC. Wakafanya umafia wao Kwa Aziz KI.
Akaja Rais wa Vipers SC akafanikiwa kuwabania Ceaser Nzoki. Hata ikawafanya waende Nigeria kum’beba OKRAH.
Kocha Stuart naye amewakataa kwa kigezo cha kushindwa kumuweka wazi kiasi cha bajeti ya usajili cha klabu kwa dirisha hili.
Nasikia hata huyo Sylla wa Horoya nae huenda wakamkosa kwa sababu wako kwenye ushindani na kigogo mmoja wa kaskazini huko.
Leo hii nao watoto wadogo wa mjini aka walima Alizeti wamefanikiwa kuingilia kati mazungumzo ya Habibu Kyombo na kufanikisha usajili wake.
Inasemekana kuwa Simba SC walikuwa wanapanga kumpa mchezaji huyo dau dogo kwakuwa alikuwa free agent na pili hakuwa akihitajika na timu nyingine kubwa ya hapa nchini.
Hizo taarifa zikasambaa si tu miongoni mwa watu wa karibu na Kyombo bali pia hata zikamfikia yule Mbunge aliyemsajilisha Fei Toto pale Singida United (Enzi hizo).
Huyo bwana baada ya kupata taarifa hizo akapandisha dau nono kwa mchezaji kama signing fee yake pia akamuahidi mshahara mnono ambao Simba SC hawakuwa tayari kumlipa.
Dogo akatamanika na akizingatia ana vina saba na U’yanga akaona asihangaike kwenda kuichezea timu ambayo hana mapenzi nayo ya dhati kutoka moyoni kwa ujira mdogo.
Msimu huu hawa jamaa wamechanganyikiwa mno.
Siamini na wala sitaki kuamini ninachoona kinaendelea kwenye kambi yao.