Pre GE2025 Hiki hapa kinaweza kuing'oa CCM Ikulu 2025

Pre GE2025 Hiki hapa kinaweza kuing'oa CCM Ikulu 2025

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

jjackline

Senior Member
Joined
Jul 25, 2024
Posts
111
Reaction score
274
Miongoni mwa wabunge waliopata umaarufu katika Bunge la mwaka 2015 - 2020, ni Selemani Bungala, maarufu kama Bwege, aliyekuwa mbunge wa Kilwa Kusini kupitia Chama cha Wananchi (CUF) kabla ya kutangaza kuhamia ACT Wazalendo baada ya Bunge kuvunjwa.

Mwananchi imefanya mahojiano maalumu na mbunge huyu wa zamani ambaye amezungumzia mambo tofauti, ikiwemo siasa za upinzani, maisha yake baada ya kukatwa mguu na mtazamo wake kwenye siasa kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2025.

Bwege anasema upinzani hauwezi kukishinda Chama cha Mapinduzi (CCM) bila wao kuungana ili kuwa na nguvu ya kukabiliana na chama hicho tawala ambacho kina nguvu kubwa ya kifedha, mamlaka na mtaji wa watu. Anapendekeza asimamishwe mgombea mmoja atakayeungwa mkono na vyama vyote vya siasa.

Chanzo: Mwananchi
 
hata wakiungana CCM ni jabali lenye mizizi mirefu kuliondoa usifikirie kabisa kuhusu sanduku la kura.
 
Miongoni mwa wabunge waliopata umaarufu katika Bunge la mwaka 2015 - 2020, ni Selemani Bungala, maarufu kama Bwege, aliyekuwa mbunge wa Kilwa Kusini kupitia Chama cha Wananchi (CUF) kabla ya kutangaza kuhamia ACT Wazalendo baada ya Bunge kuvunjwa.

Mwananchi imefanya mahojiano maalumu na mbunge huyu wa zamani ambaye amezungumzia mambo tofauti, ikiwemo siasa za upinzani, maisha yake baada ya kukatwa mguu na mtazamo wake kwenye siasa kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2025.

Bwege anasema upinzani hauwezi kukishinda Chama cha Mapinduzi (CCM) bila wao kuungana ili kuwa na nguvu ya kukabiliana na chama hicho tawala ambacho kina nguvu kubwa ya kifedha, mamlaka na mtaji wa watu. Anapendekeza asimamishwe mgombea mmoja atakayeungwa mkono na vyama vyote vya siasa.

Chanzo: Mwananchi
Tatizo la upinzani tukianzia ndani ya vyama vyenyewe, kila mmoja anaunyemelea uongozi wa juu, sasa tuje kwenye URAIS wa nchi, unadhani kuna chama kitakubali mteule wao asigombee uraisi?
 
Back
Top Bottom