Hiki kitu hakiwakeri wadada

Unique Flower kuna thread nimeandika leo asubuhi humu MMU hebu isome na nimekusogezea hapa ili ikusaidie kubadirisha mtazamo wako.

Haijalishi utakuwa unaamini hauna muonekano mzuri kwa sababu kila mtu anakutoa dosari bado haupo pekeako.Kila mtu unaemjua hajaridhika na muonekano wake.

Celebrity unaemuona yupo na muonekano mzuri sana yeye mwenyewe anatamani angekuwa na muonekano ambao wewe unavutiwa nao

Watu wote ambao unawaona kwenye Tv, magazeti, matangazo, Mitandao ya kijamii,mabango,filamu hawana muonekano ambao unaona wapo nao

Kuna Photoshop, filters hufanya kazi ya kuboresha muonekano,.Inapigwa picha kisha inachukuliwa miguu ya mtu mwengine inawekwa,sura inaondolewa chunusi,kufutwa vipele,tumbo kutengenezwa vizuri,rangi kuboreshwa mtu anakuwa anavutia mpaka yeye mwenyewe anajionea wivu.

b.FURAHIA KAZI ZA MWILI WAKO SIO MUONEKANO WAKO
Unaweza kufurahia namna unaweza kuona , kusikia,kukaa,kugusa vitu,kutembea,kuvuta harufu,kucheza ,kula n.k badala ya muonekano wa mΓ umbile yako.

Mbali na muonekano wako angalia kazi gani mwili wako unafanya kwako.

c.Epuka kujilinganisha na wengine
Ukianza kujilinganisha na wengine utagundua kwamba hauna muonekano mzuri au utajiona upo na muonekano mzuri sana kuliko wengine.

Ukianza kujilinganisha na wengine haisaidii chochote.Watu wengine kuwa na muonekano mzuri haipunguzi au kuongeza chochote kwenye muonekano wako.
Huwa unalinganisha muonekano wako na marafiki,ndugu,wapita njia,watu maarufu,kila mtu n.k lakini mwisho wa siku muonekano wa mtu yeyote uwe mzuri sana au sio mzuri hauwezi kukusaidia chochote,hauwezi kuongeza au kupunguza uzuri au ubaya wa muonekano wako.

d.Shinda wasiwasi juu ya muonekano wako
Ukiwa na wasiwasi utaanza kufikiria yafuatayo
"Kwanini nilivaa nguo ileile ambayo aliniona nayo siku ile tumekutana atahisi nipo na nguo moja "

"Najua watu walibaki wananisema vibaya kwa nguo zangu"

"Sauti yangu mbaya si nitatia aibu nikianza kuongea hapa"

Unajenga wasiwasi kwa watu ambao wao pia wanajenga wasiwasi kuhusu muonekano wao mbele yako.

Unashindwa kujiamini mbele ya watu wasiojiamini mbele yako.

Watu wote ambao unajenga hofu juu ya kile wanafikiria juu yako wao pia wanajenga hofu juu yako kwa kile ambacho unafikiria kuhusu wao.

Kwa asili binadamu huwa hatuwezi kutosheka na kitu chochote hivyo huwezi kuwa mzuri mwenye kuvutia kwa 100% katika macho ya mtu yeyote.

Hakuna binadamu mzuri kwa 100% au ambaye ni mbaya kwa 100% hivyo kujitesa sana ili uwe mzuri katika macho ya kila mtu haiwezekani hivyo furahia maisha yako kama yalivyo sio kama unavyohisi watu wengine wanataka kukuona.

Kwa sababu kila mtu huwa na mtazamo tofauti haiwezekani kuwa mzuri au mbaya kwa 100%.

Kitu chochote chenye kukufanya uwe mzuri kwa mtu mmoja kinaweza kukufanya uwe mbaya kwa mwengine.
 
Ndo ilitakiwa tuendelee kuwa vile! Now kuna vitoto vya 2000 vya kizazi cha kina zuchu vinaleta Upuuzi tu! Mijadala isiyojenga wala kumsaidia mtu kutoka Hatua moja kwenda Hatua nyingine
 
Ushauri mzuri sanaπŸ‘πŸ‘πŸ‘
 
Ndo ilitakiwa tuendelee kuwa vile! Now kuna vitoto vya 2000 vya kizazi cha kina zuchu vinaleta Upuuzi tu! Mijadala isiyojenga wala kumsaidia mtu kutoka Hatua moja kwenda Hatua nyingine
Tatizo hata JF nayo sasa hivi imekuwa kama mitandao ya kijamii tu, sasa hivi vitoto vingi vipo humu havina ajira vinakula kwao na vinapenda maisha ya kuiga mtandaoni na vimekimbia Stress za Instagram, Tiktok, Facebook vimekuja humu kuchafua hali ya hewa. Na hauwezi kuzuia mtu kwa sababu naye ana haki
 
πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Kwani wewe umeambiwa na mwana una sura mbaya baada ya kutuma picha πŸ˜…πŸ˜…πŸ˜…
 
Huwezi kuondoa ubaya kwa ubaya.
Unapowakandia unajiharibia ...huenda mumeo yuko huku bila wewe kujua.
Acha watukane wewe usibadilishwe na mtu
Mume wangu nipo nae hapa amenitoa lunch leo.
 
 
πŸ™πŸ™†
 
Hakuna mwanaume mzuri...uzuri wa mwanaume ni pesa tu.....halafu suala la mademu wa JF ni kweli wengi ni wabovu sana.....mwanzoni nilijichanganya kwa demu mmoja wa JF anasura kama kiatu nikala lakini nikajuta...baada ya hapo kila demu wa JF nikipanga kuonana naye ninajificha kwanza sehemu halafu namchora kwanza kama haeleweki natoka mbio halafu nawablock........katika mademu sita mmoja tu ndiyo alikuwa na nafuu kidogo maana alikuwa na kishkwambi na miguu imekaa poa ila sura kwa mbaali yuko sexy...ila wale wengine watano wote walikuwa wabaya kichizi nikawakimbia na kuwablock yaani huwezi hata kukaa naye mahali hata ukiwalewea pombe wanabaki vilevile wabovu.......nimeona nipumzike kwanza na mademu wa humu
 
Dah sijajua
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…