DOKEZO Hiki ni Kituo Bubu cha Polisi?

DOKEZO Hiki ni Kituo Bubu cha Polisi?

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

Mwanagenzi

JF-Expert Member
Joined
Sep 11, 2006
Posts
738
Reaction score
273
Ukiwa unatokea Masaki, kwenye makutano ya barabara za Haile Selassie na Ali Hassan Mwinyi, jirani na Kanisa la Mt. Petro, Oysterbay, Dar es Salaam, pana taa za kuongozea magari. Kwa pembeni, pana kibanda ambacho hutumiwa na askari wa usalama barabarani kujikinga na jua. Sasa, kwa muda mrefu, pamekuwa na askari, ama wenye sare za "trafiki ", au wenye silaha za moto, ambao kazi yao kuu ni kuangalia magari yanayotoka upande wa Masaki, na kuhakikisha wanabaini kuwa dereva ana makosa. Baada ya hapo dereva huelekezwa kupaki gari pembeni, kwenye hicho kibanda na baada ya mazungumzo mafupi au marefu, dereva huruhusiwa kuendelea na safari yake.

Sina hakika kama utaratibu huu hufanywa kwa halali. Kwa kifupi sehemu hiyo imekuwa kama kituo bubu cha polisi. Na shaka yangu yangu kubwa ni kuwa badala ya askari wenye silaha za moto kuwa makini na kufuatilia hali ya usalama katika mazingira yale, kwa ujumla wake, wao inavyoelekea, wamejikita katika kukagua magari na madereva wanaotoka upande wa Masaki.

Naomba hili nalo wakalitazame.
 
Hata South Africa mapolisi wengi wapo maeneo ya wadosho. Masaki ni sehemu za wadosho na ni rahisi kufanyika tukio.

Siku jichanganye hayo maeneo utembee kwa mguu kuanzia usiku. Ndio utajua difenda kwa nini linatembea sana
 
hata south africa mapolisi wengi wapo maeneo ya wadosho.masaki ni sehemu za wadosho na ni rahisi kufanyika tukio.

siku jichanganye hayo maeneo utembee kwa mguu kuanzia usiku.ndo utajua difenda kwa nini linatembea sana
Hivi huko si ndiko alikosulubiwa Adam Malima RC wa Tanga
 
sio kuhakikisha gari linakuwa na kosa,si yangejaa magari hapo!!!

zinakaguliwa gari zenye madeni ambayo hayajalipwa.ukiona mtu kasogezwa pembeni anakwenda kulipishwa kwa lazima.
 
Pale mtu anaingizwa kichakani
Maana kale kamsitu ndani hamuonekani,watu wanafinywa sana
Mule na kutolewa mpunga [emoji1]
Bongo kiboko [emoji1]

Ova
 
sio kuhakikisha gari linakuwa na kosa,si yangejaa magari hapo!!!

zinakaguliwa gari zenye madeni ambayo hayajalipwa.ukiona mtu kasogezwa pembeni anakwenda kulipishwa kwa lazima.
Sawa,basi waufyeke kale kamsitu
[emoji1]

Ova
 
Back
Top Bottom