KERO Hili Dampo katika Shule ya Msingi Oysterbay (Manyara) ni hatari kwa Afya, liondolewe

KERO Hili Dampo katika Shule ya Msingi Oysterbay (Manyara) ni hatari kwa Afya, liondolewe

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

BigTall

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2022
Posts
525
Reaction score
1,257
photo_2024-09-16_09-59-29.jpg

photo_2024-09-16_09-59-28.jpg
Wanafunzi wanaosoma Shule ya Msingi Oysterbay, iliyopo Wilaya ya Babati Mkoa Manyara wapo hatarini kupata magonjwa ya mlipuko kama Kipindupindu kutokana uchafu uliozagaa pembezoni mwa Shule hiyo.

Mimi ni mkazi wa Jirani na shule hiyo, kuna Dampo kubwa lililojaa uchafu na kutokana na upepo na Wanyama wengine kupita eneo hilo, kumekuwa na uchafu mwingi unaosambaa na kuwa kero zaidi kwa wapita njia.

Shule hiyo Kongwe iliyopo katikati ya Mji wa Babati, pamoja na uwepo wa Dampo ilo lilijaaa uchafu mwingi haina uzio, hivyo hakuna utulivu kwa Wanafunzi na wala uchafu wenyewe unaozagaa hapo.

Upande mmoja shule hiyo imepakana na uwanja wa mpira wa miguu na Stendi ya Zamani ambapo kwa sasa ni inatumika kama Soko.
photo_2024-09-16_09-59-26.jpg

photo_2024-09-16_09-59-26 (2).jpg

photo_2024-09-16_09-59-27.jpg
Kukosekana kwa uzio kumesababisha Shule hiyo iwe bize muda wote, yaani usiku na mchana, hiyo ni kwa kuwa wakazi wa Mji wa Babati wabatumia eneo hilo la Shule kama njia ya mkato kwa kuwa hakuna uzio, jambo ambalo linasababisha kukosekana utulivu wa Wanafunzi na Walimu wakati wa masomo.
 
Oysterbay ni Ghuba ya Chaza.

Ni jina la sehemu iliyo baharini, ikiyo na ghuba na iliyo na chaza.

Sasa huko Manyara kuna ghuba wapi na chaza wanapatikana vipi?

Acheni kulimbuka na majina ya watu.
 
Wanafunzi wanaosoma Shule ya Msingi Oysterbay, iliyopo Wilaya ya Babati Mkoa Manyara wapo hatarini kupata magonjwa ya mlipuko kama Kipindupindu kutokana uchafu uliozagaa pembezoni mwa Shule hiyo.

Mimi ni mkazi wa Jirani na shule hiyo, kuna Dampo kubwa lililojaa uchafu na kutokana na upepo na Wanyama wengine kupita eneo hilo, kumekuwa na uchafu mwingi unaosambaa na kuwa kero zaidi kwa wapita njia.

Shule hiyo Kongwe iliyopo katikati ya Mji wa Babati, pamoja na uwepo wa Dampo ilo lilijaaa uchafu mwingi haina uzio, hivyo hakuna utulivu kwa Wanafunzi na wala uchafu wenyewe unaozagaa hapo.

Upande mmoja shule hiyo imepakana na uwanja wa mpira wa miguu na Stendi ya Zamani ambapo kwa sasa ni inatumika kama Soko.
Kukosekana kwa uzio kumesababisha Shule hiyo iwe bize muda wote, yaani usiku na mchana, hiyo ni kwa kuwa wakazi wa Mji wa Babati wabatumia eneo hilo la Shule kama njia ya mkato kwa kuwa hakuna uzio, jambo ambalo linasababisha kukosekana utulivu wa Wanafunzi na Walimu wakati wa masomo.
hatari gani hiyo ndugu mwananchi,

Rai mazalendo mmoja tu anaweza kujitolea kusafisha eneo hilo la shule na watoto wakaendelea kujifunza wakiwa wamezungukwa na mazingira safi na salama ya kujifunzia...

Mambo haya ya kizalendo saa zinngine si ya kulalamikia mamlaka tu kila mara, ukiwa na nafasi na kauwezo kidogo unajitolea tu,

kwani taka nyepesi chache kama hizo utatumia dk ngap bana, kulalamikia kila kitu sio vizuri sana ndrugu zango 🐒
 
Oysterbay ni Ghuba ya Chaza.

Ni jina la sehemu iliyo baharini, ikiyo na ghuba na iliyo na chaza.

Sasa huko Manyara kuna ghuba wapi na chaza wanapatikana vipi?

Acheni kulimbuka na majina ya watu.
Ukistaajabu ya manyara utayaona ya kahama na oysterbay, masaki, manzese na kariakoo
 
Oysterbay ya huko porini mbona haiji? Hiyo shule mngeweza hata kuiita jina la legend wa huko Tlaatlaah Primary School.
hebu hebu sisitiza kumueleze kwanza huyo mzazi muungwana na mtoa hoja, ambae uskute hata ni mwalimu wa shule hiyo, hebu asaidie kizalendo kuziondo hizo takataka mara moja 🐒
 
Ukistaajabu ya manyara utayaona ya kahama na oysterbay, masaki, manzese na kariakoo
Oysterbay ipo mpaka New York. Ni sehemu yenye ghuba na chaza.

Hizo nyingine ni ulimbukeni tu.
 
Back
Top Bottom