HILI HALIKUBALIKI

mandarijunior

Member
Joined
Feb 14, 2017
Posts
33
Reaction score
37
KATIKA Misimu minne ya ligi kuu Tanzania bara kuanzia 2012, Young African SC tumetwaa taji mara 3 na Azam FC 1, Msimu huu panapo majaaliwa itakuwa mara yetu ya tatu mfululizo . . Inasikitisha kuona ndugu zetu wamekuwa wakipambana kutafuta ushindi kupitia kamati! Waliwahi mchezesha Ibrahim Ajib akiwa na kadi 3 za njano, Walimchezesha Novalty Lufunga ambaye alikuwa ana kadi nyekundu lakini yote haya kwao yalipita kama upepo, wakabadili sheria na utaratibu wa ligi ili kujikinga makosa yao. . Kwa Ajib wakasema ni ruksa mchezaji kuchagua michezo na kwa Lufunga wakadai rufaa imecheleweshwa maisha yakaendelea.

Leo mchana kamati ya masaa 72 ilikaa, ilijadili rufaa ya klabu ya Simba wanaolalamika kuhitaji wapewe alama 3 kwa kuwa Kagera Sugar walimchezesha mchezaji mwenye kadi 3 za njano, mvutano ulikuwa mkubwa na kufanya kamati hiyo kushindwa kutoa maamuzi leo hadi siku ya alhamisi. . Jambo lililowazi ni kuwa mchezaji huyo kadi moja ni ya kombe la shirikisho sio ligi kuu lakini cha kusikitisha watani zetu wanajaribu kupindua pindua sheria ili tu wapate hizo alama 3, Ndio maana wameamua kujipa muda waweze kujitengenezea sheria yao.

Kwa hili Wana- Yanga hatutokubali kamwe, tumetumia gharama kubwa kusajili wachezaji pamoja na walimu bora, timu imekuwa inaendeshwa kwa mazingira bora yote hiyo ni kuhakikisha tunafanya vema katika michuano inayotukabili lakini wengiñe wanajifungia vyumbani kuandaa sheria kandamizi kwa kuwa tu wao wamekuwa na idadi kubwa ya wajumbe katika kamati.

Ni kamati hii hii hadi leo wameiweka kapuni rufani ya Yanga SC waliyowakatia African Lyon, kwa kumchezesha mchezaji Venance Ludovic, huku akiwa hajakamilisha taratibu zake za uhamisho kutoka Mbao FC ya Mwanza. Hizi ni pointi mbili za wazi ambazo Yanga wanastahili kupewa lakini swala limekuwa gumu tu kwa kuwa ni Yanga.

Watani zetu tunajua mna kiu ya Ubingwa lakini ubingwa haupatikani kwa njia hizo, mnatuvurugia na kuharibu ligi yetu na soka letu kwa ujumla kisa tu mtimize azma yenu ilhali mkijua uwezo wenu mdogo! Tucheze mpira taratibu na sheria husika ziamue lakini sio kwa ubabaishaji mnaoufanya.

SIKU NJEMA Mwananchi.

- Hissan Salum Iddi.
 
We nawe! Kwahiyo ukisajili kwa fedha nyingi lazima uwe bingwa? Figisu zote za kutwaa ubingwa wa uongo,bado tu hujaona ukweli hujulikana mnapocheza mechi za CAF? Kama si Malinzi pale TFF yanga hamna uwezo wa kutwaa ubingwa. Hukumbuki mechi zenu jinsi marefa wanavyopindua maamzi?mf mechi ya simba na mlipocheza na majimaji.Kama wewe una muda mrefu hapa Jf,utakumbuka nilivyosema mpaka simba iwe kwenye peak ndipo timu ya Taifa itakuwa bora. Sasa jiulize kwanini nilisema hivyo.
 
Hoja hapa ni hiyo rufaa yenu kwa kagera ndo inayojadiliwa msimu hu inatumika nguvu kubwa kuwafanya simba muwe mabingwa na hiyo hoja yako uchwara ya kuwa simba ikiwa kwenye form na stars inakuwa hivyo haina maana yoyote
 
Mmeshakuwa wasemaj w kagera
 
Mkuki kwa nguruwe tatzo wanasahau mapema sana hawa mikia ss kwa Ajibu walitujibu kirahisirahisi tu leo wao mishipa ya shingo imewasimama!
 
acheni kulia lia tusubili kamati ifanye kazi yake
 
Yanga kweli masikini manji kaumwa kidogo bado kidogo tu mpitishe bakuli
 
Pointless
 
Simba ni bora kwenye masubwi tu,uwanjani ni bashite tu
 
Kama timu ikipewa point nje ya uwanja, basi ni dhahiri mpira wetu bado tunayo safari ndefu sana kufikia mafanikio. Maana mahaba yana nafasi kuliko weledi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…