Sio kwa wapenzi tuu bali kwa watu wote in general. Kama unaongea na mtu kwenye simu nafikiri ni vizuri ukamaliza nae kwanza badala ya ku-hold hold kila wakati ili uongee na mtu mwingine. Kama unaongea na watoto wadogo sawa inaweza eleweka lakini na watu wazima ni bora aseme tuu umpigie au akupigie baadae. It is all about manners. Mara nyingi watu hawa ndio unaowakuta wanaongea kwenye simu huku waki-drive.
EMT hapo sasa unatusema wengine bana
Japo huwa siuzi chai ila kwa hapo umetugussa mkuu
EMT hayo siyataki kabisa yanikute na wala siyataki kabisa
Ila kwenye kuongea na simu wakati niko kwenye driving hiyo ipo sana mkuu
Sio kwa wapenzi tuu bali kwa watu wote in general. Kama unaongea na mtu kwenye simu nafikiri ni vizuri ukamaliza nae kwanza badala ya ku-hold hold kila wakati ili uongee na mtu mwingine. Kama unaongea na watoto wadogo sawa inaweza eleweka lakini na watu wazima ni bora useme tuu utampigia au akupigie baada ya muda fulani. It is all about manners. Mara nyingi watu hawa ndio unawakuta wanaongea kwenye simu huku waki-drive.
kama unataka upige simu upewe full attention piga simu kuanzia saa sita usiku hadi saa kumi.
La unapopiga simu mchana jua mtu yupo kwenhe mihangaiko, uvumilie. Aache kusaka pesa kwa ajili ya simu? Au asipokee simu?
Heshima zenu wana MMU,
Mi kuna jambo huwa linanipa shida sana, Hivi inapotokea unampigia simu mpenzi/mchumba/mume/mke au mtu yeyote ambae unamuheshimu ghafla katikati ya mazungumzo yenu unashangaa anakuwa anaongea na watu wengine wakati bado upo online, alaf anarud kuendelea na mazungumzo yenu.
Hii inatokea wakati mpo kwenye mazungumzo Mara ghafla unasikia anatoa maelezo au anamwagiza kitu fulan mtu mwingine alaf baadae ndo anarudi kwako kuendelea na mazungumzo.
Unashangaa tena baada ya dakika chache anakuacha tena na kuendelea na mazungumzo mengine kisha anarud, we utasikia tu eeh tuendelee.
Hii hali inapotokea mara kwa mara kwenye mazungumzo yenu inamaanisha nini?
mimi huwa natafsiri kuwa huyo mtu ananidharau ama ninachoongea nae kwake ni pumba.
wana jamvi hii mnaichukuliaje?