Mkuu,
kwanza unatakiwa kujua kuwa Comoro ni mjumuiko wa visiwa vitatu kama sitakosea, Yaani comoro, ngazija na mayotte '' ambacho kipo chini ya ufaransa''.
Wale wanaokujaga kucheza michuano huku walikuwa wanatokea ngazija na comoro bila kushirikisha mayotte ambayo ni sehemu ya ufaransa.
Kuanzia misimu miwili uliopita visiwa vyote vitatu vimeungana na kutengeneza team moja ya taifa, yaani mayotte, ngazija na comoro.
Kwakuwa mayotte ipo chini ya ufaransa basi wachezaji wake wengi sana wanashiriki ligi mbalimbali za ufaransa za madaraja ya chini na baadhi ligi kuu ya ufaransa na wamelelewa katika misingi mizuri ya kimichezo.
Nakumbuka mechi yao ya kwanza kufanya maajabu ilikuwa dhidi ya Ghana walipotoka sare ya bila kufungana nadhani ilikuwa kufuzu afcon, baada ya hapo wakacheza na cameroon na kutoa nao sare ya goli 1-1 tena cameroon wakisawazisha dakika za lala salama, mechi nyingine ni dhidi ya moroco walitoa upinzani mkubwa sana japo walifungwa 1-3 kama sitokosea.
Baada ya hapo ni maajabu ambayo wameyafanya juzi kwa kumpiga togo kwake na kutoa sare na misri, akikomaa kuna uwezekano mkubwa sana wa kushiriki afcon 2021.
Wana wachezaji wengi sana wanaocheza nje, mara ya mwisho naangalia kwenye team yao kulikuwa na mchezaji mmoja tu anaecheza ligi ya africa na hawakuwa na mchezaji hata mmoja ambae anacheza comoro.
Kuna mchezaji wao anacheza Redstar belgade ambayo inacheza uefa champions league.