Hili ndio ombi maalumu la Mussa kwa binadamu kuondolea adhabu ya moto wa Jahannam

Hili ndio ombi maalumu la Mussa kwa binadamu kuondolea adhabu ya moto wa Jahannam

BAKIIF Islamic

JF-Expert Member
Joined
Jul 11, 2021
Posts
600
Reaction score
1,843
Naam,

Siku moja Nabii Mussa (a.s) alimueleza MUNGU yakwamba; Ewe Mwenyezi MUNGU nina maombi nataka nikuombe.

Mungu akamjibu, omba ombi lako lolote Mussa, mimi nitakujibu.

Mussa akamueleza Mwenyezi Mungu

Ewe mwenyezi Mungu, ninakuomba hizi habari za kuwachoma watu kwenye moto siku ya mwisho ni vyema ungeziondoa, watu wenyewe ni dhaifu hawana nguvu wala uwezo, wewe ndio una nguvu zote, na wewe ndio mwenye uwezo wa kila kitu, kwanini sasa uwachome hawa binaadamu dhaifu kwenye moto, mimi nakuomba ondoa hii adhabu ya kuchoma watu kwenye moto. Haya ni maombi yangu nakuomba ewe Mwenyezi Mungu.

Mwenyezi Mungu akamueleza Mussa:

Ewe Mussa, haraka sana tengeza shamba. Mussa akaanza kutengeneza shamba, akalisafisha shamba lake, akalima kisha akapanda mazao, baada muda kukamilika akaja akavuna mazao yake, akayahifadhi vizuri na kuyatunza, kisha akarudi shambani kwake, akakusanya vijiti, yaani mabua ya mimea yaliyokauka na kubakia hapo shambani, akavikusanya sehemu moja kisha akavichoma moto.

1690528034148.png

1690528072022.png


Mungu akaumueleza, ewe Mussa umefanya nini hapo?

Mussa akajibu: Nimekwisha vuna mazao yangu safi nimeyahifadhi ndani, sasa nina mpango huwenda msimu mwingine nitalima tena kwa hivyo hivi vijiti naona vitanisumbua ndio nimeamua nivichome moto kwasababu ni mabua sina faida nayo.

1690527891204.png


Mungu akamueleza Mussa;
Hivyo hivyo ulivyofanya Mussa, ndivyo na mimi Mwenyezi Mungu ninafanya kwa wanaadamu, katika binaadamu kuna watu ambao sina faida nao, nitawachoma katika moto wa Jahannam. Japokuwa wamezalika katika dunia hii lengo kuu ni kupata ile mbegu safi, ambayo mimi nitaihifadhi katika pepo yangu, na waliobakia ni mfano wa vijiti au mabua nitawachoma katika moto wa Jahannamu kwasababu sina faida nao hata kama wamezalika katika dunia. Kama ulivyofanya wewe Mussa.

1690528931673.png
 
Kibri ni hamu ya kujipatia ukuu dhidi ya wengine, pengine hata dhidi ya Mwenyezi Mungu. Kiburi ni hisia na fikra zilizopotoka kuhusu ukweli na uhalisia wa mambo.
Picha hizo ni kiwakilishi tu, lakini hazihusiani na hadithi hiyo
 
Nani alikuwa ananukuu hayo mazungumzo Kati ya Mwamba na Mussa Hadi wewe huku mavumbini umeyapatia?
Mussa (a.s) aliteremshiwa vitabu viitwavyo 'Suhfi' na Ibrahimu pia aliteremshiwa vitabu viitavyo 'Suhfi''. Kwa waislamu MUNGU amenukuu vitabu hivi kwa kuviita Suhufi ibraheema wamoosa . Qur'an (87:19)
 
Naam,

Siku moja Nabii Mussa (a.s) alimueleza MUNGU yakwamba; Ewe Mwenyezi MUNGU nina maombi nataka nikuombe.

MUNGU akamjibu, omba ombi lako lolote Mussa, mimi nitakujibu.

Mussa akamueleza Mwenyezi MUNGU:

Ewe mwenyezi MUNGU, ninakuomba hizi habari za kuwachoma watu kwenye moto siku ya mwisho ni vyema ungeziondoa, watu wenyewe ni dhaifu hawana nguvu wala uwezo, wewe ndio una nguvu zote, na wewe ndio mwenye uwezo wa kila kitu, kwanini sasa uwachome hawa binaadamu dhaifu kwenye moto, mimi nakuomba ondoa hii adhabu ya kuchoma watu kwenye moto. Haya ni maombi yangu nakuomba ewe Mwenyezi MUNGU.

Mwenyezi MUNGU akamueleza Mussa:

Ewe Mussa, haraka sana tengeza shamba. Mussa akaanza kutengeneza shamba, akalisafisha shamba lake, akalima kisha akapanda mazao, baada muda kukamilika akaja akavuna mazao yake, akayahifadhi vizuri na kuyatunza, kisha akarudi shambani kwake, akakusanya vijiti, yaani mabua ya mimea yaliyo kauka na kubakia hapo shambani, akavikusanya sehemu moja kisha akavichoma moto.

View attachment 2701162
View attachment 2701163

MUNGU akaumueleza, ewe Mussa umefanya nini hapo?

Mussa akajibu: Nimekwisha vuna mazao yangu safi nimeyahifadhi ndani, sasa nina mpango huwenda msimu mwingine nitalima tena kwa hivyo hivi vijiti naona vitanisumbua ndio nimeamua nivichome moto kwasababu ni mabua sina faida nayo.

View attachment 2701157

MUNGU akamueleza Mussa;
Hivyo hivyo ulivyo fanya Mussa, ndivyo na mimi Mwenyezi MUNGU ninafanya kwa wanaadamu, katika binaadamu kuna watu ambao sina nao faida, nitawachoma katika moto wa Jahannam. Japokua wamezalika katika dunia hii lengo kuu ni kupata ile mbegu safi, ambayo mimi nitaihifadhi katika pepo yangu, na waliobakia ni mfano wa vijiti au mabua nitawachoma katika Moto wa Jahannamu kwasababu sina faida nao hata kama wamezalika katika dunia. Kama ulivyofanya wewe Mussa.

View attachment 2701172

Sitory za pauka pakwa hizo,hazina uhalisia wowote.
 
Naam,

Siku moja Nabii Mussa (a.s) alimueleza MUNGU yakwamba; Ewe Mwenyezi MUNGU nina maombi nataka nikuombe.

MUNGU akamjibu, omba ombi lako lolote Mussa, mimi nitakujibu.

Mussa akamueleza Mwenyezi MUNGU:

Ewe mwenyezi MUNGU, ninakuomba hizi habari za kuwachoma watu kwenye moto siku ya mwisho ni vyema ungeziondoa, watu wenyewe ni dhaifu hawana nguvu wala uwezo, wewe ndio una nguvu zote, na wewe ndio mwenye uwezo wa kila kitu, kwanini sasa uwachome hawa binaadamu dhaifu kwenye moto, mimi nakuomba ondoa hii adhabu ya kuchoma watu kwenye moto. Haya ni maombi yangu nakuomba ewe Mwenyezi MUNGU.

Mwenyezi MUNGU akamueleza Mussa:

Ewe Mussa, haraka sana tengeza shamba. Mussa akaanza kutengeneza shamba, akalisafisha shamba lake, akalima kisha akapanda mazao, baada muda kukamilika akaja akavuna mazao yake, akayahifadhi vizuri na kuyatunza, kisha akarudi shambani kwake, akakusanya vijiti, yaani mabua ya mimea yaliyo kauka na kubakia hapo shambani, akavikusanya sehemu moja kisha akavichoma moto.

View attachment 2701162
View attachment 2701163

MUNGU akaumueleza, ewe Mussa umefanya nini hapo?

Mussa akajibu: Nimekwisha vuna mazao yangu safi nimeyahifadhi ndani, sasa nina mpango huwenda msimu mwingine nitalima tena kwa hivyo hivi vijiti naona vitanisumbua ndio nimeamua nivichome moto kwasababu ni mabua sina faida nayo.

View attachment 2701157

MUNGU akamueleza Mussa;
Hivyo hivyo ulivyo fanya Mussa, ndivyo na mimi Mwenyezi MUNGU ninafanya kwa wanaadamu, katika binaadamu kuna watu ambao sina nao faida, nitawachoma katika moto wa Jahannam. Japokua wamezalika katika dunia hii lengo kuu ni kupata ile mbegu safi, ambayo mimi nitaihifadhi katika pepo yangu, na waliobakia ni mfano wa vijiti au mabua nitawachoma katika Moto wa Jahannamu kwasababu sina faida nao hata kama wamezalika katika dunia. Kama ulivyofanya wewe Mussa.

View attachment 2701172
Jehanamu ni sehemu nje kidogo ya Yerusalemu ambapo walukouwa wsakichomea maiti miaka hiyo.

Mungu muweza muweza wa yote mjuzi wa yote na mwenye upendo wote hawezi kuumba ulimwengu wenye kuruhusu maabaya yatokee ili aje kuchoma viumbe vyake.

Huyo Mungu ni tungo tu za hadithi na hayuko kwenye uhalisia.
 
Jehanamu ni sehemu nje kidogo ya Yerusalemu ambapo walukouwa wsakichomea maiti miaka hiyo.

Mungu muweza muweza wa yote mjuzi wa yote na mwenye upendo wote hawezi kuumba ulimwengu wenye kuruhusu maabaya yatokee ili aje kuchoma viumbe vyake.

Huyo Mungu ni tungo tu za hadithi na hayuko kwenye uhalisia.
Hata serikali ya nchi inayosema inapenda watu wake kindakindaki, linapokuja swala la taaluma inabagua, nyinyi wote mtakwenda darasani, mtafundishwa kwa usawa na kisha mtapimwa, watakaofuata utaratibu watachukuliwa na watakaovuruga utaratibu watatupwa mtaani.
 
Huyu mussa ndio yule aliyewakomboa wayahudi misri?

Kama ndiye hii story yako chanzo chake Ni kipi?
Kama Ni koran mbona hii story kwenye Bible haipo? Kwa sababu chanzo Cha maandiko ya koran kuusu maisha ya wayahudi kabla mtume mudi ajaanzisha uislamu karne ya 7 Ni Bible au Bible ya kiyahudi

Kingine baada ya mussa kutoka misri alikwenda jangwani pamoja na wayahudi, huko jangwani mussa na wayahudi hawakuwai kulima chochote zaidi ya kula mana iliyoshushwa na mungu toka angani

Kama hii Ni hekaya sawa, ila Kama Ni maandiko ya mungu itakuwa umetungwa katika karne ya 7
 
Mungu ndiye aliyeumba yote.
Ubaya na uovu uliumbwa na Mungu.
Uzuri na Wema nao aliuumba Mungu.

Ukichagua mazuri utaishi katika Ulimwengu wa Watu Wazuri.
Ukichagua Mabaya utaishi katika Ulimwengu wa wabaya.

Hakuna kuchomwa Moto hizo ni Stori za kutunga tuu.
 
Mungu ndiye aliyeumba yote.
Ubaya na uovu uliumbwa na Mungu.
Uzuri na Wema nao aliuumba Mungu.

Ukichagua mazuri utaishi katika Ulimwengu wa Watu Wazuri.
Ukichagua Mabaya utaishi katika Ulimwengu wa wabaya.

Hakuna kuchomwa Moto hizo ni Stori za kutunga tuu.
Mkuu, mantiki yako ya kukataa kwamba hakuna reward kwa wema na wabaya ni nini haswa? Yaani unamaanisha ukitenda mabaya utalipwa wema na ukitenda mema utalipwa wema pia?
Ni kanuni zipi za kifalsafa unazotumia haswa kukanusha na kupinga habari za moto.
 
Naamini Mungu yupo
ila kuhusu dini,
yaani dini hii ni halali na dini zile sio halali hapana dini ni utamaduni mila na desturi za jamii husika katika miongozo waliojiwekea.
 
Naamini Mungu yupo
ila kuhusu dini,
yaani dini hii ni halali na dini zile sio halali hapana dini ni utamaduni mila na desturi za jamii husika katika miongozo waliojiwekea.
Wewe unaamini Mungu yupi?

Unajua kuwa swala la Mungu linamezwa na dini.

Embu nambie Mungu wako unayemuamini ana sifa zipi
 
Back
Top Bottom