Hili neno zeruzeru linafaa kutumika?

Hili neno zeruzeru linafaa kutumika?

May Day

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2018
Posts
6,311
Reaction score
9,027
Nilikuwa nasikiliza BBC SWAHILI leo ninamsikia Mtangazaji Ann Ngugi anatumia hilo neno, cha ajabu hata Wenzake, akiwemo Mbelechi wa Congo wametumia jina/neno 'wenye ulemavu wa ngozi' au Albino.

Ina maana BBC na ukubwa wao hawajui?
 
BBC hao hao nilimsikia reporter wao akiwaita watu wasioona 'vipofu'. Kutumia maneno kama zeruzeru, vipofu au viziwi kunakuwa kuna hali fulani ya udunishi ndani yake.

Ni vyema tukatumia majina yenye kuonesha thamani ya mtu mfano badala ya kuita
-zeruzeru tutumie mtu mwenye ulemavu wa ngozi
-kiziwi tutumie mtu mwenye ulemavu wa kusikia n.k



Sent using Jamii Forums mobile app
 
BBC hao hao nilimsikia reporter wao akiwaita watu wasioona 'vipofu'. Kutumia maneno kama zeruzeru, vipofu au viziwi kunakuwa kuna hali fulani ya udunishi ndani yake.

Ni vyema tukatumia majina yenye kuonesha thamani ya mtu mfano badala ya kuita
-zeruzeru tutumie mtu mwenye ulemavu wa ngozi
-kiziwi tutumie mtu mwenye ulemavu wa kusikia n.k



Sent using Jamii Forums mobile app
Kabisa, pia badala ya kipofu tunasema Mtu asiyeona au mwenye uoni hafifu.

Tatizo huyu Ann Ngugi ni Mkenya, wao wanatwanga tu neno moja kwa moja.

Cha ajabu yule wa Mwakilishi wao wa Congo kakwepa kutumia jina/neno Zeruzeru.
 
Nisha wahi pigwa bakora tatu na teacher kahonga kipagamo sc kisa kutamka neno zeruzeru ndipo Maelezo mangine yaka fuata
 
Kwani mtu asiyeona si ndo kipofu?
Mwnye ulemavu wa ngozi si ndo zeruzeru?
Asiyesikia si ndo kiZiwi?
Sasa kuna tatzo gani
Ni sawa na kusema "mtu mwenye kimo kirefu" badala ya mrefu
Au mtu kusema "mwenye umbo kubwa na nyama nyingi" baadala mnene
 
Inaitwa TAFSIDA kupunguza ukali wa maneno, hivyo BBC iwapo wamelitumia neno ZERUZERU kama kilivyo pasi na nia ya kudadavua kua "neno hili lisitumike hivi" kiandishi watakua wamekosea na inawezekana ni makosa tu ya kibinadam.

Katika kiswahili fasaha utangulizi wa maneno haya huonyesha tahadhari kabla ya matamshi ASHAKUM SI MATUSI ndipo ukalitaja neno ZERUZERU ingeweza kuswihi pia.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Inaitwa TAFSIDA kupunguza ukali wa maneno, hivyo BBC iwapo wamelitumia neno ZERUZERU kama kilivyo pasi na nia ya kudadavua kua "neno hili lisitumike hivi" kiandishi watakua wamekosea na inawezekana ni makosa tu ya kibinadam.

Katika kiswahili fasaha utangulizi wa maneno haya huonyesha tahadhari kabla ya matamshi ASHAKUM SI MATUSI ndipo ukalitaja neno ZERUZERU ingeweza kuswihi pia.

Sent using Jamii Forums mobile app
Waarabu wa afrika buana!!
 
BBC hao hao nilimsikia reporter wao akiwaita watu wasioona 'vipofu'. Kutumia maneno kama zeruzeru, vipofu au viziwi kunakuwa kuna hali fulani ya udunishi ndani yake.

Ni vyema tukatumia majina yenye kuonesha thamani ya mtu mfano badala ya kuita
-zeruzeru tutumie mtu mwenye ulemavu wa ngozi
-kiziwi tutumie mtu mwenye ulemavu wa kusikia n.k



Sent using Jamii Forums mobile app
mzee sasa hapo unakuwa unatoa maana sasa, kwa hiyo hao watu hawapaswi kuitwa majina yao bali kuelezewa sifa zao?
 
Hakuna cha "Waarabu wa Afrika" hapo bali hata kwa wenzetu na lugha zao, huwa wanatumia lugha za staha katika kuelezea ulemavu wa mtu! Kwa mfano, kwao kwa mtu aliye muungwana hawezi akasema XYZ is disabled bali atakuambia XYZ has disability.Au hawezi kusema "Disabled people come forward" bali "people with disability...."

Au XYZ has hearing impairment badala ya kusema XYZ is deaf! Badala ya kutumia XYZ is blind, watasema has visual impairment/visually impaired!!

Sio kwamba kumuita mtu deaf ni kosa but it sounds kind of rude and offensive kwa sababu kuwa kipofu ni zaidi ya kushindwa kuona; kuwa kiziwi ni zaidi ya kushindwa kusikia
Duh basi hao wenzako wana matatizo.
Wazungu naowajua mimi wanasemaga XYZ is blind,deaf,disabled etc.
Soma hata Bible inavyowataja hao watu
"And as Jesus walked the aisle, he met a blind man by the corner"
 
Back
Top Bottom