Uchaguzi 2020 Hili ni eneo Mojawapo kati ya Maeneo tuliyozidiwa akili na wale jamaa

Uchaguzi 2020 Hili ni eneo Mojawapo kati ya Maeneo tuliyozidiwa akili na wale jamaa

Shark

JF-Expert Member
Joined
Jan 25, 2010
Posts
29,775
Reaction score
29,746
Asubuhi ya tarehe 28 October niliamka mapema tu nikiwa na furaha. Nilikua nimepanga lazima " Nikachinje" watu watatu kutoka chama kile "Cha Siku Zote". Kichinjio changu kilikua tayari tayari stand by.

Siku hiyo jinsi nilivokua na hamu ya kuchinja wale Jamaa watatu hata chai niliwaza nije kunywa nikirudi kutoka "Machinjioni". Nikapiga number za kucheck kituo kilipo ili nisije nikaenda kwengine. Kituo ni kile kile Cha 2015, na bahat nzuri sijahama mtaa.

Basi nimefika eneo la tukio sikupata tabu kujua chumba kilipo. Tukio lilifanyika kwenye Shule ya Msingi, hivyo kituo changu ni darasa Mojawapo. Kura zinapigwa mbele kwenye angle ya opposite na mlango.

Nimeingia pale nikakuta jamaa kama wanne wa tume wamevaa T-shirt nyeupe zenye nembo ya tume. Pia kulikuwepo na wengine wawili wamevaa kawaida tu wanapiga story, nikajisemea hawa bila shaka ndo mawakala wa vyama. Kimoja labda ni CCM Ila kingine sijui ni kipi.

Mfanyakazi wa kwanza wa tume alioko karibu na mlango alichukua kadi yangu na kuanza kuita jina langu mara tatu. Niligeuka kule kwa mawakala nikaona wanasikiliza tu, hawafanyi chochote. Hapa ndipo nilipoanza kukosa nguvu, nikaona kabisa lengo langu la "kuchinja" halitotimia ipasavyo.

Baada ya hapo nikamaliza taratibu zingine na kuondoka kinyonge. Nilijua kabisa tu kwa utaratibu ule "hatutoboi" hata chembe. Kwa jinsi navyowajua "Wale Jamaa" pale tayari tushapigwa bao za mapema tu, kushinda hii game ni majaaliwa.

SHIDA IKO WAPI?
Vyama vilipewa orodha / register ya wapiga kura, ilifaa kila kituo wakala awe nayo angalau. Ili tukiwa tunaita majina wawe wanaweka tiki kwenye hizo nakala zao. Hii itawezesha kujua wangapi wamepiga kura kwenye kituo husika.

Lakini Sasa ndio unakuta mambo kama ya Kahama Ubunge jumla kura 50,000+ wakati Urais jumla kura 167,000+. Hakuna wakala anaejua idadi kamili ya waliopiga kura kwenye kituo alichosimamia. Sasa vitabu/register tulipewa za nini jamani? Wakala unaendaje kituoni bila kitabu? Hata wakiongeza idadi unajuaje?

Hivi ni kweli tuliamini hawa jamaa wataendesha Uchaguzi usiokua na figisu zozote mpaka tusahau jambo muhimu kama hili? Tuna wabunge wana uzoefu sana na hizi figisu, walishindwa kukumbuka jambo muhimu kama hili kweli? Sasa nini maana ya Mtumishi wa Tume kuita jina langu mara tatu ikiwa wakala hana popote anapo-verify?

Niliwaza nisiandike haya sababu uchaguzi umeshafanyika, lakini siwezi kukaa na dukuduku, hata baadae Uchaguzi ujao itasaidia.

Weekend njema.
 
muda wa mabadiliko ya mfumo huu mbovu
sema shida huwa tunajisahau sanaa...
 
Upinzani ulikufaga kitambo toka walipomkumbatia fisadi lowasa na kumpiga teke slaa!
 
Mimi nilipopigia kura, mawakala walikuwa wa CCM, CDM na ACT na wote walitumia daftari moja kuhakiki kila mpiga kura anapotajwa jina na namba yake.


By the way, ilikuwa ni kijijini, wote ni wakazi wa kijiji hicho hivyo hakukuwa na haja ya kuleteana manoma wakati maisha ya kawaida lazima yaendelee baada ya uchaguzi.

Washamba pekee ndiyo wamegeuza siasa kuwa uadui.
 
Hata wewe una mwisho pia, ...
Kuwa mwizi au jambawazi sio jambo la fahari wala heshima katika jamii, Ila ajabu nyie maccm mnalizungumzia kwa fahari na majigambo kama watu wenye vichaa hivi.
Tatizo ni nini humo ndani ya chama chenu? Au mmeshikwa na kichaa kama mwenyekiti wenu anavyo jinadi kuwa anacho?
 
Yaaani wao walimeshaamini kua bila hujuma hatuwezi shinda ..ndio maana ikifika kampeni wanaanza kuratibu wizi wao
 
Lawama zote kwa Tume, kama wangetoa vitambulisho vya mawakala mapema hayo yote yasingetokea.

Unaposema uliona jamaa ndani wenye nembo za Tume na wengine wawili, hao wawili unasema mmoja alikuwa wa CCM, huyo mwingine unajiridhisha kusema tu alikuwa wa Chadema lakini uhakika huo huna.

Wasimamizi wa Tume peke yao walikuwa ni sawa na wasaidizi wa CCM, bado palikuwepo na wenyeviti wa serikali za mitaa, na wajumbe wao vituo vingi, kwamba Tume iliwanyima mawakala barua makusudi wakijua fika CCM ingepata msaada toka kwa hao wengine wakiwemo polisi waliokuwepo vituoni kulinda usalama wa kura feki za CCM.
 
Niliota mbinu iliyotumika ila haitasaidia.....maana uchaguzi imeisha, na hiyo mbinu ilitumika baada ya plan A ikishindikana ya kuongeza Kura,hiyo mbinu, ngoja nitoe picha kidogooo, mengine mtamalizia wenyewe,
Je nani alijihakikishia kuwa juma amejiandikisha vituo vingapi kwenye kata au Jimbo??? Je kama kajiandikisha mara kumi kwenye vituo tofauti?
Je kama alipewa vitambulisho kumi kwa kila kituo??
Je walivyoruhusu hata kama hauna kitambulisho cha tume,utumie kitambulisho kingine?? Hapo vipp wadau, bao la mkono Hilo
Eti utaniuliza ukipiga Kura unapakwa wino...hahahah... Mchina anashindwa kitu....
Nawaza Tu, nikiwa ndotoni.... Wakaandaliwa watu 50, wakajiandikisha vituo 10, na kila mmoja anapiga Kura 10 kwa MTU mmoja,je jumla zitapigwa Kura 500, za bao la mkono... Hahahaha. Nawatania ndugu zangu, haiwezi kutokea uchaguzi ulikuwa wa Uhuru na haki
 
Mtatafuta Visingizio
Lakini Ukweli upo pale pale
Huyo Mamluki wenu Kupata hata 20% Ilikuwa Ndoto kwake
Mtu gani Akisimama ni Risasi Matusi hana Jipya
 
Niliota mbinu iliyotumika ila haitasaidia.....maana uchaguzi imeisha, na hiyo mbinu ilitumika baada ya plan A ikishindikana ya kuongeza Kura,hiyo mbinu, ngoja nitoe picha kidogooo, mengine mtamalizia wenyewe,
Je nani alijihakikishia kuwa juma amejiandikisha vituo vingapi kwenye kata au Jimbo??? Je kama kajiandikisha mara kumi kwenye vituo tofauti?
Je kama alipewa vitambulisho kumi kwa kila kituo??
Je walivyoruhusu hata kama hauna kitambulisho cha tume,utumie kitambulisho kingine?? Hapo vipp wadau, bao la mkono Hilo
Eti utaniuliza ukipiga Kura unapakwa wino...hahahah... Mchina anashindwa kitu....
Nawaza Tu, nikiwa ndotoni.... Wakaandaliwa watu 50, wakajiandikisha vituo 10, na kila mmoja anapiga Kura 10 kwa MTU mmoja,je jumla zitapigwa Kura 500, za bao la mkono... Hahahaha. Nawatania ndugu zangu, haiwezi kutokea uchaguzi ulikuwa wa Uhuru na haki
Kuyaongea Simple ila Hakuna lolote
Wala Jipya
 
Mtatafuta Visingizio
Lakini Ukweli upo pale pale
Huyo Mamluki wenu Kupata hata 20% Ilikuwa Ndoto kwake
Mtu gani Akisimama ni Risasi Matusi hana Jipya
Wewe unazungumziaje swala la Kahama kura za Ubunge hazizidi 55,000 lakini za Urais ni zaidi ya 165,000??
 
Back
Top Bottom