Hili shauri lifunguliwe kwenye mamlaka ipi?

Boko halal

Senior Member
Joined
May 14, 2014
Posts
175
Reaction score
124
Kuna mgogoro wa ardhi kati ya familia moja, Iko hivi mzee mmoja aligawa ardhi kwa vijana wake wawili, yeye akabaki na sehemu ndogo ya ardhi, baadae mzee yule akaoa mke mwingine na baada ya mwaka akafariki, sasa huyu mama mjane anadai mme wake enzi za uhai wake alimpa eneo ambalo kwa sasa linamilikiwa na wale vijana, wale vijana nao wanakataa kuwa baba yao aligawia maeneo hayo hata kabla hajamuoa mama yao mdogo.

Huyu mama afungue shauri kwenye mamlaka ipi? Mahakama au baraza la ardhi la kata, ikumbukwe imepita miaka zaidi ya 13 toka kifo cha mme wake.
 
Hapo ameshakuwa time barred, anachoweza kufanya ni kuomba kuongeza muda kwa waziri (katiba na sheria)
 
Daaah hao wanahitaji ushauri serius kabisaa wa kisheria, sababu wako nje ya muda wa kisheria kwa karibu kila kitu, iwe ni ardhi iwe mirathi. Na kuna hatua ndefu za kufuata hapo.
 
Taratibu ndefu kwasababu ya mda unaokubalika kisheria. Pili kama maelezo yako ni kweli basi huyo mama hana chake hapo. Mzee alishagawa Mali yake hata kabla hajaolewa. Labda kwenye kile kipande alichokuwa akiishi na mzee kama kina shida. I stand to be corrected
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…