Hili wazo limekaaje?

Africa Tanzania

JF-Expert Member
Joined
Jun 13, 2015
Posts
1,504
Reaction score
2,272
Mimi nasimamia biashara zangu nyingi tu, zenye faida japo sio kwa 100%

Wazo langu ni

Mteja anakuja kwangu, anaweka pesa yake mfano 100,000/=

Halafu kila mwezi atakuwa anapata commission ya 15% kutoka kwangu!

Hii itafanyika kimkataba na kisheria zaidi....

Na mteja huyo atakuwa na uwezo wa kuchukua pesa yake aliyoweka mara baada ya mkataba wake kuisha!

Wazo ni hilo....

Naombeni changamoto zake au maswali nitayajibu!
 
Una Mali isiyohamishika pindi ukishindwa kunirudishia hela yangu? Hapa wewe ni mkopaji na unakopa kwa riba hila sasa mkopaji anamuwekea mkopeshaji masharti! Maajabu haya
 
asilimia 15 ni nyingi mno, labda Kama unataka kumdhulumu. Kiwango rafiki si zaidi ya asilimia 5. Na kiwango cha kuwekeza kisiwe chini ya laki 5.
 
Ukiwa tayali niambie nkupe ka milion niwe nchukuapo huto tu asilimia
 
Hii naona haina tofauti na wanayoifanya mtaani.Unakopa laki kwa mwezi unamlipa laki na 20.Ukishindwa mnaweza kukubaliana akapokea 20 kama faida take na mkataba wa laki kwa laki na 20 unabaki palepale.Tofauti hapo itakuwa kuandikishiana kisheria.Unaweza boresha kwenye hiyo asilimia 15%japo wengi wameshauri upunguze na muda wa mkataba kuwa mrefu badala ya kupunguza asilimia ya faida.
 
Kitu unachotaka kufanya ni kizuri sana kikubwa ni kuwa muwazi tu na kuwa na details zote za kutosha I mean mimi km investor ninae wekeza kwenye biashara yako ntataka niijue vizuri biashara yako ni nn na inaendeshwaje na changamoto zake zikoje na ikiwezekana uwe na platform Fulani ambayo inatoa details zaidi kwa wawekezaji wako unless ww ni bank ctataka kujua hivyo vitu kwa kuongezea km una details zote nishilikishe na mm PM ntafurahi kuwekeza kwako na iwe passive income kwangu
 
Hauruhusiwi kisheria maana hiyo ni kazi ya bank au mashirika yanuwekezaji kama UTT labda ufanye kimya kimya ambapo ni vigumu mtu kukuamini labda watu unaofahamiana nao au uwe na dhamana.
 
PesaBOX hii inakuja soon ni ya jamaa nasoma UDSM ,mtu anaweka ela kwenye app ya pesabox kwa mpesa,tigopesa, halopesa etc ina act-kama fixid account uki-invest ela yako hapa jamaa anatumia kufanya investiment na kutoa mikopo ("his own risk"). kwa hiyo mfano ukiweka labda 50000 kwa miezi miwili unaapata faida ya 2.5% ambapo mtu atachukua jumla 51,250. lakini kwa kipindi hicho huyo jamaa anaitumia hiyo ela yako kuzalisha zaidi ya 20%. Unaweza kuanzisha app au website ku mchallenge jamaa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…