ndiyomkuusana
JF-Expert Member
- Aug 2, 2012
- 666
- 426
HATIMAYE Serikali imeamua kuvunja ukimya na kutoa uamuzi kuhusu sakata la umiliki wa hisa za mgodi wa madini wa Tanzanite One uliopo wilayani Simanjiro mkoani Manyara na kuamuru wananchi pamoja na kampuni hiyo kugawana pasu kwa pasu asilimia 50 kila mmoja.
Hatua hiyo imekuja baada ya mvutano mkubwa kuibuka kuhusu umiliki wa mgodi huo kufuatia wachimbaji wadogo kutaka wapewe asilimia 50 kuchimba madini hayo ya vito huku sheria mpya ya madini ikiwabana wawekezaji hao kutochimba madini hayo ya vito kwa asilimia 100 isipokuwa si zaidi ya asilimia 50 tu.
Hata hivyo,itakumbukwa ya kuwa,Rais Jakaya Kikwete aliwahi kutoa ahadi katika kijiji cha Lengast wilayani Simanjiro mkoani humo wakati akijinadi katika kampeni za uchaguzi mkuu mwaka 2010 kwamba angemegea wachimbaji wadogo eneo la mgodi huo mara baada ya wawekezaji hao kumaliza mkataba wao ulioisha mwezi machi mwaka huu. Akizungumza katika mkutano wa kumpokea na kumkaribisha nyumbani Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi(CCM),Abdulrahamn Kinana, Waziri wa Nishati na Madini,Sospeter Muhongo alitamka kuwa hivi karibuni suluhisho litapatikana ambapo wawekezaji hao watamiliki asilimia 50 na wachimbaji watapewa asilimia 50.
Waziri huyo alienda mbali zaidi na kusisitiza ya kuwa Serikali inaangalia uwezekano wa kumiliki asilimia 60 katika mgodi huo huku akisema wamejidhatiti kuhakikisha migodi yote inalipa asilimia 4 kama mrabaha.
Naye Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Stephen Masele alitamka kwamba Serikali itahakikisha Mkoa wa Arusha unakuwa Kituo cha Kimataifa cha Madini ya Vito.
Alisema kuwa Serikali iko katika mchakato wa kuhakikisha kituo hicho kinajengwa hivi karibuni huku akiwaonya wale watakaowawekea vikwazo vijana wanaofanya biashara ya vito vya madini hususani ya Tanzanite.
source. mwananch.17.12.12
Hatua hiyo imekuja baada ya mvutano mkubwa kuibuka kuhusu umiliki wa mgodi huo kufuatia wachimbaji wadogo kutaka wapewe asilimia 50 kuchimba madini hayo ya vito huku sheria mpya ya madini ikiwabana wawekezaji hao kutochimba madini hayo ya vito kwa asilimia 100 isipokuwa si zaidi ya asilimia 50 tu.
Hata hivyo,itakumbukwa ya kuwa,Rais Jakaya Kikwete aliwahi kutoa ahadi katika kijiji cha Lengast wilayani Simanjiro mkoani humo wakati akijinadi katika kampeni za uchaguzi mkuu mwaka 2010 kwamba angemegea wachimbaji wadogo eneo la mgodi huo mara baada ya wawekezaji hao kumaliza mkataba wao ulioisha mwezi machi mwaka huu. Akizungumza katika mkutano wa kumpokea na kumkaribisha nyumbani Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi(CCM),Abdulrahamn Kinana, Waziri wa Nishati na Madini,Sospeter Muhongo alitamka kuwa hivi karibuni suluhisho litapatikana ambapo wawekezaji hao watamiliki asilimia 50 na wachimbaji watapewa asilimia 50.
Waziri huyo alienda mbali zaidi na kusisitiza ya kuwa Serikali inaangalia uwezekano wa kumiliki asilimia 60 katika mgodi huo huku akisema wamejidhatiti kuhakikisha migodi yote inalipa asilimia 4 kama mrabaha.
Naye Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Stephen Masele alitamka kwamba Serikali itahakikisha Mkoa wa Arusha unakuwa Kituo cha Kimataifa cha Madini ya Vito.
Alisema kuwa Serikali iko katika mchakato wa kuhakikisha kituo hicho kinajengwa hivi karibuni huku akiwaonya wale watakaowawekea vikwazo vijana wanaofanya biashara ya vito vya madini hususani ya Tanzanite.
source. mwananch.17.12.12