Hisa za voda zaporomoka

Hisa za voda zaporomoka

besaro

Member
Joined
Nov 9, 2015
Posts
52
Reaction score
40
Habari zenu wapambanaji wenzangu.
Kwa Leo ninayo machache juu ya mambo ya hisa za vodacom.
Tunajua ni jinsi gani zilipigiwa upatu kuwa biashara itakayokuja kututoa kimasomaso lakini kwa sasa habari sio nzuri sana kwa walionunua hisa bei imeporomoka kutoka 850( bei ya kununulia) hadi 770 bei ya hisa kwa sasa hapo ni bila makato yake so huu ni muda wa kujaribu kucheki fursa nyingine
 
Zitazidi kushuka tuu sababu watu wamepungua mpesa hatutumii mpesa sababu ya gharama kubwa tumeamia tigo pesa na airtel money
 
Naomba kujua ni vitu gani vinasababisha kupanda na kushuka
Kushuka na kupanda kwa hisa kunatokana na msukumo wa soko la hisa husika. Kwa kuwa soko hilo lina wanunuzi wengi na wauzaji wengi wasiofahamiana husemekana kuwa bei inayopatikana sokoni ndio bei halisi ya hisa husika. Kinachotokea ni kwamba, ikitokea watu wengi wanaomiliki hizo hisa wameingia sokoni ili kuuza hisa zao (kukawa na idadi kubwa ya hisa zinazo uzwa) na wakati huohuo kukawa na watu wachache wanaotaka kununua hisa hizo (hisa chache zinatakiwa). Huu wingi wa hisa zinazouzwa utailazimisha bei ya hisa kushuka. Fikiri katika namna rahisi, jana chungwa liliuzwa shg 150, leo machungwa toka shamba yaneletwa kwa wingi sokoni na wanunuzi ni wachache, kuna uwezekano mkubwa yakauzwa shg 100. Kupanda kutatokea pale ambapo hisa zinazouzwa ni chache lakini zinazo hitajiwa na watu ni nyingi.
 
Si dalili
Habari zenu wapambanaji wenzangu.
Kwa Leo ninayo machache juu ya mambo ya hisa za vodacom.
Tunajua ni jinsi gani zilipigiwa upatu kuwa biashara itakayokuja kututoa kimasomaso lakini kwa sasa habari sio nzuri sana kwa walionunua hisa bei imeporomoka kutoka 850( bei ya kununulia) hadi 770 bei ya hisa kwa sasa hapo ni bila makato yake so huu ni muda wa kujaribu kucheki fursa nyingine

Si dalili nzuri, unaanza kwa kupoteza fedha.
Angalau ingekuwa inaongezeka hata sh 50 per share,
 
Biashara kwa kipindi hiki, changamoto zipo nyingi
 
Kushuka na kupanda kwa hisa kunatokana na msukumo wa soko la hisa husika. Kwa kuwa soko hilo lina wanunuzi wengi na wauzaji wengi wasiofahamiana husemekana kuwa bei inayopatikana sokoni ndio bei halisi ya hisa husika. Kinachotokea ni kwamba, ikitokea watu wengi wanaomiliki hizo hisa wameingia sokoni ili kuuza hisa zao (kukawa na idadi kubwa ya hisa zinazo uzwa) na wakati huohuo kukawa na watu wachache wanaotaka kununua hisa hizo (hisa chache zinatakiwa). Huu wingi wa hisa zinazouzwa utailazimisha bei ya hisa kushuka. Fikiri katika namna rahisi, jana chungwa liliuzwa shg 150, leo machungwa toka shamba yaneletwa kwa wingi sokoni na wanunuzi ni wachache, kuna uwezekano mkubwa yakauzwa shg 100. Kupanda kutatokea pale ambapo hisa zinazouzwa ni chache lakini zinazo hitajiwa na watu ni nyingi.


so who decides zipande au kushuka?
 
so who decides zipande au kushuka?

Possibly watu waki piga sana simu kwa Voda hisa zake zitapanda???
Km Ni kuwekeza tayari miundo mbinu yote ipo intact.
Ki nini kita determine kupanda au kushuka kwa hizo hisa.
 
Nilijua tu huu mchezo wa hisa utaishia hapa. Unaanzaje biashara ya hisa kipindi cha financial crisis hivi.
 
so who decides zipande au kushuka?
wanaouza na kununua hisa (demand and supply)
wauzaji wakiwa weng kuliko wanunuz hisa zinashuka bei wanunuz wakiwa weng kuliko wanaonunua hisa zitapanda bei
kuna mambo yanayoweza kusababisha wanunuz wawe weng
1.financial perfomance ya kampuni..kama kampuni itakua inaperfom vzr ina generate more profit lazma watu weng watatamani kununua hisa so wanunuz wataongezeka na hisa zitapanda bei

2. dividend announcement kuna kampuni zinatangaza magawio mara kwa mara so hii lazma ikuze thaman za hisa

3. money circulation..mzunguko wa hela pia ukiwa mkubwa watu weng watakua na uwezo wa ku-afford kununua hisa so lazma bei yake itapanda

ziko nyng hzo ni baadhi
 
Back
Top Bottom