Hisa zinalipa

Hisa zinalipa

LEO VII

Senior Member
Joined
Feb 7, 2013
Posts
118
Reaction score
34
Msaada Wa kimawazo tafadhali, wajasiliamali tunaamini moja kati ya rasilimali za kumiliki ni HISA, Mimi sina uzoefu kabisa kabisa kuhusu HISA, ntapataje uzoefu?, Je kampuni gani zinalipa vizuri? Vitu gani vya kutilia mkazo? Hasara zake ni zipi? Nawasilisha wakuu..
 
Mkuu kumiliki hisa za kampuni fulani kunaitajika kazi kubwa na ziada kuifanya. Katika nchi zilizoendelea kuna watu hawa wanafanya kazi kutafuta ( research) habari za makampuni na kuzichambua vitabu vya mapato na matumiz na pia kusuggest kama hii kampuni ni njema au lah.

Kibongo bongo ni ngumu sana. Lakin inawezekana. Makapuni ambayo yako stable na uhakika wa mauzo ni makampuni ya bia, cement na mabenki yenye mitaji mikubwa.

Usije ukamiliki vitu kama mashirika ya ndege na vitu ambavyo competition ya bidhaa ni kubwa .kumbuka lengo ni kuinvest kwenye kampuni ambazo zina bidhaa moja au zaidi na zina pata faida. Pia ukumbuke kuangalia history charts au mapato ya miaka angalau mitano nyuma au zaidi. Pia kuna kitu wanaitwa dividends ni jambo zuri la kuangalia.

Unaweza kwenda kwenye maofisi ya kampuni utakayo na kuwaomba financial documenta zao na kwamba unataka ununue hisa. Pia angalia ni wapi unaweza kununua unaweza ukanunua zikiwa juu sana na zikashuka na zisipande tena labda mpaka baada ya miaka kadhaa au mwezi. Kwa bongo bado tuko nyuma sana kupata hiz info.




The king.
 
Asanteni sana wakubwa, nimepata kitu hapa!
 
Back
Top Bottom