Yoda
JF-Expert Member
- Jul 22, 2018
- 48,475
- 70,102
Tangu kupata uhuru wake kutoka USSR mwaka 1991 Ukraine lilikuwa ni taifa linalopata viongozi wanaopokezana mitazamo na mielekeo wakipokezana kufungamana kati ya West (EU&US) au Russia kwa vipindi tofauti lakini kadri muda ulivyosonga mbele raia wengi wa taifa hilo walizidi kuwa na muelekeo wa West zaidi hali iliyopelekea bunge na urais kutawaliwa na viongozi wenye mtazamo na wanaotaka kufungamana na West zaidi kuliko Russia.
Mwaka 2010 akachaguliwa Viktor Yanukovych kuwa Rais wa Ukraine ambaye alikuwa ni Pro-Russia na mwenye maslahi binafsi ya biashara na Russia lakini bunge bado likawa na wabunge wengi zaidi ambao ni Pro-West. Yanukovych akaingia na malengo ya kufuta maendele yaliyopigwa kuelekea Ulaya na mtangulizi wake Viktor Yushchenko ambaye alikuwa Pro-West, tatizo likawa hakuwa na idadi ya wabunge wa kutosha kupitisha sera za kuilekeza Ukraine upande wa Russia.
Mwaka 2013 bunge la Ukraine likapitisha muswaada wa Ukraine kuingia mkataba wa kisiasa na biashara huru na Umoja wa Ulaya. Yanukovych akogoma kuusaini mkataba dakika za mwisho kabisa . November mwaka huo yakaibuka maandamano makubwa nchi nzima yalioendelea mpaka 2014.
Rais Yanukovych ambaye alikuwa ni Pro-Russia aliondolewa madarakani kwa maandamano ya raia nchi nzima baada ya kukataa kusaini mkataba wa biashara na EU na madai mengine yaliyofuatia ya waandamanaji kama kuporomoka kwa demokrasia, uhuru wa raia na kukithiri kwa rushwa.
Putin kuona Russia kapoteza mtu wake muhimu Kyiv akaanza kufanya vurugu Crimea na maeneo mengine ya Ukraine mashariki kisha akaingiza majeshi huko na sababu kubwa ya kushindwa kuzuiwa wakati huo ni serikali ya dhaifu ya Ukraine.
Baada ya hapo EU na USA waliwekeza pesa nyingu na utaalamu kuijenga serikali ya Ukraine na jeshi lake, Putin akaendelea kuona Ukraine ikizidi kuimarika, ikamtisha na akajua hataweza tena kuifanya koloni lake "vassal state" akaivamia nchi nzima wakati huu kwa lengo la kuweka tena kibaraka wake Kyiv, akakutana na jeshi lililoimarika zaidi kuliko la 2015, akapata upinzani mkali.Aliposhindwa lengo kuu akahamishia nguvu mashariki ili aigawe hiyo nchi asitoke mikono mitupu.
Matokeo yoyote yatakayopatikana baada ya mgogoro huu ikiwa Ukraine itaendelea kubaki taifa huru itakuwa ni ushindi mkubwa kwake.
Mwaka 2010 akachaguliwa Viktor Yanukovych kuwa Rais wa Ukraine ambaye alikuwa ni Pro-Russia na mwenye maslahi binafsi ya biashara na Russia lakini bunge bado likawa na wabunge wengi zaidi ambao ni Pro-West. Yanukovych akaingia na malengo ya kufuta maendele yaliyopigwa kuelekea Ulaya na mtangulizi wake Viktor Yushchenko ambaye alikuwa Pro-West, tatizo likawa hakuwa na idadi ya wabunge wa kutosha kupitisha sera za kuilekeza Ukraine upande wa Russia.
Mwaka 2013 bunge la Ukraine likapitisha muswaada wa Ukraine kuingia mkataba wa kisiasa na biashara huru na Umoja wa Ulaya. Yanukovych akogoma kuusaini mkataba dakika za mwisho kabisa . November mwaka huo yakaibuka maandamano makubwa nchi nzima yalioendelea mpaka 2014.
Rais Yanukovych ambaye alikuwa ni Pro-Russia aliondolewa madarakani kwa maandamano ya raia nchi nzima baada ya kukataa kusaini mkataba wa biashara na EU na madai mengine yaliyofuatia ya waandamanaji kama kuporomoka kwa demokrasia, uhuru wa raia na kukithiri kwa rushwa.
Putin kuona Russia kapoteza mtu wake muhimu Kyiv akaanza kufanya vurugu Crimea na maeneo mengine ya Ukraine mashariki kisha akaingiza majeshi huko na sababu kubwa ya kushindwa kuzuiwa wakati huo ni serikali ya dhaifu ya Ukraine.
Baada ya hapo EU na USA waliwekeza pesa nyingu na utaalamu kuijenga serikali ya Ukraine na jeshi lake, Putin akaendelea kuona Ukraine ikizidi kuimarika, ikamtisha na akajua hataweza tena kuifanya koloni lake "vassal state" akaivamia nchi nzima wakati huu kwa lengo la kuweka tena kibaraka wake Kyiv, akakutana na jeshi lililoimarika zaidi kuliko la 2015, akapata upinzani mkali.Aliposhindwa lengo kuu akahamishia nguvu mashariki ili aigawe hiyo nchi asitoke mikono mitupu.
Matokeo yoyote yatakayopatikana baada ya mgogoro huu ikiwa Ukraine itaendelea kubaki taifa huru itakuwa ni ushindi mkubwa kwake.