EINSTEIN112
JF-Expert Member
- Oct 26, 2018
- 21,711
- 35,644
Historia ya mkoa wa Shinyanga inaanza hata kabla ya wakoloni kuitawala Tanganyika mwaka 1890's-1961.
Wakoloni wa kwanza kutawala eneo la sasa la mkoa wa Shinyanga walikuwa ni wajerumani walioanza kutawala mwaka 1890's hadi waliposhindwa kwenye vita ya kwanza ya dunia mwaka 1918.
Wajerumani walipoingia na kuitawala Tanganyika walikuta eneo la sasa la mkoa wa Shinyanga linakaliwa na watu wa makabila ya Wasukuma, Wanyamwezi, Wasumbwa, Walongo na Watusi.
Katika utwala wa Wajerumani, waliweza kuigawa Tanganyika katika maeneo madogo ya kiutawala yanayoitwa Wilaya, ambapo eneo la sasa la mkoa wa Shinyanga lilikuwa ndani ya wilaya ya Tabora chini ya mkuu wa Wilaya anaye wajibika kwa Gavana wa Tanganyika.
Mara baada ya kuisha kwa vita ya kwanza ya dunia, Waingereza walianza kutawala eneo la sasa la mkoa wa Shinyanga kuanzia mwaka 1920 hadi wakati wa uhuru wa Tanganyika mwaka 1961.
Mara baada Tanganyika kupata Uhuru 1961, ilipofika mwaka 1963 wilaya ya Tabora iligawanywa na na serikali ya Jamhuri ya Tanganyika na kuzaa mkoa wa Tabora na Shinyanga.
#ASILI YA JINA NDAKI NA NGEREJA USUKUMANI WAKATI WA UKOLONI 1980's-1961.
Wakati, Wajerumani wanaingia usukumani kutawala walionekanani wakali na wakorofi sana.
Jambo ambalo wasukuma wakanda zote liliwafanya wawabatize kwa jina la "Bhadaki" wakiwa na maana ya Wakorofi/Wakali.
Hivyo Katika kipindi cha Wajerumani watoto wengi wa kiume waliozaliwa walipewa majina la "NDAKI".
Pia Katika kipindi cha Utawala wa Waingereza, Wasukuma walishindwa kutamka Waingereza badala yake wakawaita "Bhangereja."
Hivyo watoto wengi wakiume waliozaliwa Katika kipindi cha utawala wa Waingeraza walipewa majina ya "NGEREJA".
#ENEO LA SHINYANGA CHINI YA WATEMI(BHATEMI).
Kabla ya kuja kwa wakoloni eneo la mkoa wa Shinyanga lilikuwa chini ya watawala wa jadi wanaoitwa Watemi(Bhatemi)
Kila mtemi alimiliki eneo lake lenye mipaka linaloitwa Utemi(Bhutemi).
Mkoa wa Shinyanga ulikuwa chini ya watemi kutoka kabila la Wasukuma, Wanyamwezi na Wasumbwa.
Mfano eneo kubwa la wilaya ya Shinyanga na Kishapu lilitawaliwa na watemi(Bhatemi) wa kabila la wasukuma.
Eneo la wilaya ya Kahama lilitawaliwa na na watemi wa kabila la Wanyamwezi na eneo la Ushetu lilikaliwa na watemi wakabila la Wasumbwa.
#Ntemi Ng'hwaya Ng'wandu-BUSIYA
#Ntemi Kishimba -KAHAMA
#Ntemi Magope-USHETU
#Karibuni kwa nyongeza na kuboresha mapungufu ya makala hii.
#Imeandikwa na Mjukuuwa Nshimba ya Nyawa kutoka Nzega-Tabora.
Sent using Jamii Forums mobile app
Wakoloni wa kwanza kutawala eneo la sasa la mkoa wa Shinyanga walikuwa ni wajerumani walioanza kutawala mwaka 1890's hadi waliposhindwa kwenye vita ya kwanza ya dunia mwaka 1918.
Wajerumani walipoingia na kuitawala Tanganyika walikuta eneo la sasa la mkoa wa Shinyanga linakaliwa na watu wa makabila ya Wasukuma, Wanyamwezi, Wasumbwa, Walongo na Watusi.
Katika utwala wa Wajerumani, waliweza kuigawa Tanganyika katika maeneo madogo ya kiutawala yanayoitwa Wilaya, ambapo eneo la sasa la mkoa wa Shinyanga lilikuwa ndani ya wilaya ya Tabora chini ya mkuu wa Wilaya anaye wajibika kwa Gavana wa Tanganyika.
Mara baada ya kuisha kwa vita ya kwanza ya dunia, Waingereza walianza kutawala eneo la sasa la mkoa wa Shinyanga kuanzia mwaka 1920 hadi wakati wa uhuru wa Tanganyika mwaka 1961.
Mara baada Tanganyika kupata Uhuru 1961, ilipofika mwaka 1963 wilaya ya Tabora iligawanywa na na serikali ya Jamhuri ya Tanganyika na kuzaa mkoa wa Tabora na Shinyanga.
#ASILI YA JINA NDAKI NA NGEREJA USUKUMANI WAKATI WA UKOLONI 1980's-1961.
Wakati, Wajerumani wanaingia usukumani kutawala walionekanani wakali na wakorofi sana.
Jambo ambalo wasukuma wakanda zote liliwafanya wawabatize kwa jina la "Bhadaki" wakiwa na maana ya Wakorofi/Wakali.
Hivyo Katika kipindi cha Wajerumani watoto wengi wa kiume waliozaliwa walipewa majina la "NDAKI".
Pia Katika kipindi cha Utawala wa Waingereza, Wasukuma walishindwa kutamka Waingereza badala yake wakawaita "Bhangereja."
Hivyo watoto wengi wakiume waliozaliwa Katika kipindi cha utawala wa Waingeraza walipewa majina ya "NGEREJA".
#ENEO LA SHINYANGA CHINI YA WATEMI(BHATEMI).
Kabla ya kuja kwa wakoloni eneo la mkoa wa Shinyanga lilikuwa chini ya watawala wa jadi wanaoitwa Watemi(Bhatemi)
Kila mtemi alimiliki eneo lake lenye mipaka linaloitwa Utemi(Bhutemi).
Mkoa wa Shinyanga ulikuwa chini ya watemi kutoka kabila la Wasukuma, Wanyamwezi na Wasumbwa.
Mfano eneo kubwa la wilaya ya Shinyanga na Kishapu lilitawaliwa na watemi(Bhatemi) wa kabila la wasukuma.
Eneo la wilaya ya Kahama lilitawaliwa na na watemi wa kabila la Wanyamwezi na eneo la Ushetu lilikaliwa na watemi wakabila la Wasumbwa.
#Ntemi Ng'hwaya Ng'wandu-BUSIYA
#Ntemi Kishimba -KAHAMA
#Ntemi Magope-USHETU
#Karibuni kwa nyongeza na kuboresha mapungufu ya makala hii.
#Imeandikwa na Mjukuuwa Nshimba ya Nyawa kutoka Nzega-Tabora.
Sent using Jamii Forums mobile app