Daniel Mbega
JF-Expert Member
- Mar 20, 2013
- 338
- 180
NDOTO za Yanga kuingia kwenye ushindani wa kuwania mamilioni ya fedha zinaweza kupata mwanzo mzuri Jumamosi, Februari 27, 2016 ikiwa wataing’oa mashindanoni Cercle de Joachim ya Mauritius katika Ligi ya Mabingwa Afrika.
Mabingwa hao wa soka Tanzania Bara, wanarudiana na timu hiyo bingwa mara mbili wa Ligi Kuu ya Mauritius wakiwa wanajivunia ushindi wa bao 1-0 walioupata Februari 13, 2016 mjini Curepipe.
Hata hivyo, kama historia inaweza kuchangia matokeo, basi Yanga iko katika nafasi kubwa ya kufuzu kwa hatua hiyo dhidi ya timu kutoka Visiwa vilivyoko ndani ya Bahari ya Hindi.
ZAIDI SOMA HAPA...