Historia ya dini ya Hindi Pwani ya Afrika Mashariki

Historia ya dini ya Hindi Pwani ya Afrika Mashariki

Kanungila Karim

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2016
Posts
20,743
Reaction score
25,564
SEHEMU YA KWANZA

KWA UFUPI TU:Katika taaluma ya theolojia duniani wanatambua uwepo wa dini ya hindu. Kihistoria dini hii ya hindu ilianzia kuchipuka mnamo kwenye miaka ya 500KK-300BK.


707b7b9d5875755fdd64a54eda6ed777.jpg


Dini hii kwa mara ya kwanza ilipata kuchipukia kwenye maeneo ya Bonde la Indus(sehemu ambayo ustaharabu kwa watu wa bara hilo ulipoanzia), na inasemekekana hata neno Hindu ndipo lilianzia huko. Asilimia kubwa waumini wa kwanza walikuwa Wahindi waliopata kuishi kwenye maeneo hayo ya bonde la Indus, ambapo kulikuwa na mito ambayo ndio iliyosababishwa ustaharabu kwa Wahindi waliopata kuishi huko. Hakika katika historia ya Afrika mashariki tunatambua sana uwepo wa wahindi. Hii ina maana kuwa ujio wa Wahindi Afrika mashariki kulileta mabadiliko makubwa sana. Kwani Wahindi hao walikuja na utamaduni wao ambao aidha ulipendwa au haukupenda na watu wa waafrika mashariki. Ukweli ni kwamba sio kila sehemu au nchi Wahindi hawa walipata kufika. Hivyo tunapozungumzia ujio wa dini ya hindu Afrika mashariki tunaangalia maeneo kama Zanzibar, Kenya na Uganda. Maeneo yaliorodheshwa hapo ndio tutakayo anagalia namna dini ya Hindu ilifika na kukua kwake.



DINI YA HINDU KISIWANI ZANZIBAR. Historia inafafanua kuwa, ujio wa waarabu wa awamu ya pili ulilenga mabadiliko makubwa sana ya uchumi. Mabadiliko hayo ya uchumi yalileta mabadiliko mpaka kwenye masuala ya kijamii, hasa ukuaji wa dini ya Uislamu na Hindu. Kwa hakika ujio wa wafanya biashara wa kiarabu ulisababisha ujio wa Wahindi kisiwani Zanzibar. Inafafanuliwa kuwa mara baada ya Said Sayyid kuhamisha makazi yake kutoka Mascat, Oman na kuja kisiwani Zanzibar mnamo miaka ya 1840, kwa lengo la kukuza baishara.Ukweli ni kwamba alifanya mabadiliko makubwa sana. Na kutokana na wakati huo harakati za kupinga biashara ya utumwa zilishaanza, kwa Said Sayyid ilikuwa changamoto kubwa sana. Hivyo aliamua kufanya mabadiliko makubwa sana katika mfumo wa biashara. Na kutokana na idadi ya wafanyakazi wa kiarabu kuwa ndogo, Sayyid Said aliamua kualika Wahindi kwa lengo la kufanya baishara. Wapo Wahindi ambao walikuwa wafanyakazi kwenye mashamba na viwanda vya sultan Sayyid Said, na wapo Wahindi ambao walianzisha maduka yao wenyewe. Hivyo ujio wa wahindi hao ulifanya maendeleo ya biashara kukuwa kwa kiasi kikubwa.

Inaendelea

Sent using Jamii Forums mobile app
 
SEHEMU YA PILI
Kutokana na uwepo wa Wahindi hao, ambao walikuwa wakizaliana siku baada ya siku, kuliibuka na kukua kwa tamaduni za kihindi. Na moja ya utamaduni ni kukuwa kwa Imani na falsafa za dini ya Hindu. Hivyo kisiwani Zanzibar kukawa na dini mpya ya Wahindi iliopata kukuwa kwenye miaka ya 1840. Pamoja na kukua huko kwa dini hiyo, haikufanya dini zingine kama Uislamu na Ukristo kutokukuwa. Kwani kila wanajamii walipata muda wa kufanya ibada zao, hii inamaana kuwa Wakristo waliabudu, Waislamu pia waliabudu. Na inafafanuiwa kuwa idadi ya Wahindi waliopata kufika kisiwani Zanzibar walitoka maeneo ya Punjab ( ikiwa na maana ya mji uliopo kwenye mito mitano) na mji wa Gujarat. Ifahamike tu kwamba kwa upande fulani dini ya Hindu iliweza kusambaa mpaka maeneo ya Dar es salaam, ambapo inafafanuliwa kuwa Wahindi wengi walifika na kuishi hapo. Na wengie wao walikuwa wafanyabishara. Kulikuwa na mfanya bishara wa kihindi aliyefahamika kwa jina la Ismail, yeye alikuwa maarufu sana kutokana na ufanyaji wake wa biashara mnamo miaka ya 1850.
Mpaka kufikia miaka ya 1880, ambapo mara baada ya mkutano wa Berlin ambapo Waingereza walikabidhiwa kisiwa cha Zanzibar, bado Wahindi walikuwa na uhuru wa kuabuni kisiwani hapo.

KWA MTAZAMO WANGU, naamini kwamba dini hii haikusambaa sana na haikupata waumini ambao sio Wahindi kwa sababu zifuatazo. Kwanza, idadi kubwa ya Wahindi waliofika kisiwani zanzibara wliletwa kama wafanya kazi. Hivyo suala la kusambaza dini yao haikuwa suala la kipaumbele.kwani walikuja kufanya bishara tu.. Hivyo hawakuona haja ya kutumia muda mwingi kusambaza dini yao.
Pili wengi wa wafanyabiashara wa kihindi hawakuwa wanafalsafa ambao wangetumia muda wao kuandika maandiko mengi kwa lengo la kukuza dini yao. Hivyo muda mwingi waliutumia katika kufanya biashara na sio kuandika viatabu. Na mwisho, idadi kubwa ya watu waliokuwa kisiwani Zanzibar ni waafrika, ambao walienda Zanzibar kama watumwa na wangine kama wafanyakazi. Hivyo ilikuwa vigumu sana kwa Wahindi hao kupata muda wa kukaa na waafrika hao na kukuza dini yao, hivyo dini hii haikusambaa na kukua sana tofauti na Uislamu na Ukristo.

Inaendelea

Sent using Jamii Forums mobile app
 
SEHEMU YA TATU
cfc55273eb0ea06a9b5539251c26454c.jpg

Kama ilivyokwisha fafanuliwa kuwa mara baada ya mkutano wa Berlin wa mwaka 1884/1885, nchi ya Kenya na Uganda ikawa chini ya Waingereza. Na mpaka kuanzia miaka ya 1890 nchi hizi mbili au makoloni haya yalikuwa chini ya utawala wa waingereza.
Hivyo waingereza walitaka kuanzisha utawala wao na mfumo mpya wa uchumi. Sambamba na hilo kulifanyika harakati za ujenzi wa reli ambayo iliunganisha maeneo ya Mombasa na Kisumu hadi Uganda. Na ifahamike tu kwamba, wakati Saidi Sayyid anahamia kisiwani Zanzibar, tayari Waingereza walikuwa na mahusino na sulatni huyo.
Hivyo kitendo cha sultani kuwaleta Wahindi kisiwani Zanzibar na kufanya shughuri zao, kiliwafanya Waingereza kuwaelewa sana Wahindi.Kwani Wahindi walikuwa wakifanya kazi kwa bidii sana na walikuwa wanajua sana mahesabu. Hivyo hata katika kuendeleza makoloni yao,Waingereza waliwatumia sana Wahindi.
Na inafafanuliw kuwa Mwanzoni kabisa mwa miaka ya 1890, Waingereza waliwaalika Wahindi kama wafanyabiashara katika makoloni yao. Lakini ilipofikia mwanzo mwa miaka ya 1902, waingereza walianza kuwatumia Wahindi kama wafanyakazi wa ujenzi wa reli. Wafanyakazi hao walitoka maeneo yale yale Punjab na Gujarat. Na ikumbukwe tu kwamba maeneo haya ndio yale maeneo ambayo dini ya Hindu inaapoanzia au kuchipukia.
Inaendelea

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna jambo huwa najiuliza sana kuhusu Wahindi na ustaarabu wa pwani ya Tanzania. Historia inaonesha kwamba wahindi walileta kwa namna moja ama nyingine tamaduni yao kwenye tamaduni ya watu wa Pwani ya Tanzania.

Lakini ni kwa nini wao hawako daraja moja na waarabu ama wazungu wa Kiingereza na kijerumani? Ama na wao wametumbukizwa kwenye kapu moja na Wareno ambao ni kama vile hawakuwahi kuwepo kwenye Pwani hiyo?

Mohamed Said
 
Kwa bara wahindi walikuwa wakiishi bagamoyo, ila baada ya reli ya mjerumani kukamilika na bandari kujengwa wahindi wote walihamia dar es salaam. Mji wa bagamoyo ukafa kibiashara.
 
Back
Top Bottom