Historia ya Kinjekitile Ngwale ni historia yenye utata!

Historia ya Kinjekitile Ngwale ni historia yenye utata!

Kanungila Karim

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2016
Posts
20,743
Reaction score
25,564
Leo katika kupekua kwangu mtandaoni, nimekutana na historia mbili tofauti zinazomzungumzia Kinjekitile. Kilichonivutia hadi kuamua kuwashirkikisha wasomaji wa kibaraza hiki ili tutafakari kwa pamoja ni kutokana na kupingana kwa historia hizo.

Wakati historia moja ikihoji kuwa Kinjekitile alikuwa shujaa au mshirikina? ambayo iliandikwa na mwandishi Aloyce Menda katika gazeti la Tanzania Daima la Ijumaa, Septemba 21,2006, nyingine ilikuwa ikidai kuwa historia yake imepotoshwa, ambayo nayo iliandikwa na mwandishi Evaristy Masuha katika gazeti hilo hilo la Tanzania Daima la Alhamisi, Agosti 21, 2008.

Kwa historia hizo mbili kunaonekana kuwa na walakini na ni vyema historia hii ikawekwa sawa kwa manufaa ya vizazi vijavyo, la sivyo tutajikuta tukiwa tumepoteza kumbukumbu hii muhimu kwa vizazi vyetu.

Naomba tuwekane sawa katika swala hili, Je ni yupi yuko sahihi kati ya waandishi hawa wawili?

>>BOFYA HAPA KUANGALIA WAPIGANAJI WA VITA VYA MAJI MAJI

***************************************

Na Aloyce Menda KINJEKITILE - Jemedari shujaa kweli au mshirikina laghai tu?
'Wakoloni wa Kijerumani waliita Vita ya Majimaji kuwa ni uasi wa Majimaji au Majimaji Rebellion kwa Kiingereza. Kwa Wakoloni, Kinjekitile alikuwa mhaini aliyekuwa anapinga utawala halali. Kwa dhana hiyo, Kinjekitile alikuwa shujaa kwa kupigania uhuru wa watu waliokuwa chini ya ukoloni.

Lakini kwa kutazama kwa kina mbinu za ukombozi alizotumia kupigania huo uhuru, sioni ushujaa wake. Vitabu vya historia vilivyoandikwa na wakoloni na hata vya wazalendo vinaonyesha wazi kwamba Kinjekitile alilaghai mamilioni ya watu wasioelimika, kwamba risasi za moto kutoka katika magobore ya askari wa Kijerumani zinaweza kugeuzwa maji na kuishia kulowesha tu miili yao bila madhara yoyote.

Kinjekitile alilaghai watu kwamba yeye anafahamu sayansi ya kijadi itakayotumiwa na ‘watu wake’ katika vita dhidi ya Wajerumani na kushinda. Sayansi yenyewe aliifundisha yeye mwenyewe kilaghai na kuisambaza kutoka Kilwa hadi Songea.

Watu wengi wakapotoshwa na kuamini kwamba risasi za moto zitageuka maji katika vita, kasha wakahamasishwa kuanzisha vita bila kujiandaa kwa mbinu nyingine za ziada! Silaha zao za jadi zilikuwa ni mawe, marungu, mundu, pinde, mishale na mikuki butu. Hatari iliyoje hiyo!

Kinjekitile mwenyewe hakwenda mstari wa mbele katika vita halisi, wala hakudiriki kusitisha mapambano alipoona maelfu ya ‘watu wake’ wakiteketezwa kwa risasi. Badala yake, alikaa mafichoni huku akiendelea kutuma wasaidizi wake kushawishi watu waamini ulaghai wake, na kwamba waliokuwa wanakufa kwa risasi hizo ni wale tu ambao hawakutimiza vyema masharti ya ‘sayansi’ yake aliyowapa.

‘Shujaa’ Kinjekitile alikuwa tapeli hatari sana kiasi kwamba, hakuwa na himaya maalumu ya kuishi, tofauti na walivyokuwa kina Chifu Mkwawa, Mtemi Mirambo and Mangi Sina. Bila shaka alikuwa anafahamu fika kwamba siku moja ulaghai wake utafikia mwisho, ambapo watu wangemgeukia na kumtoa roho yake, hivyo alijihami kabla kwa kuishi mafichoni kama afanyavyo gaidi Osama bin Laden hivi sasa.

Vita ilipokaribia mwisho wake kwa wazalendo wengi kufa kama sisimizi, Kinjekitile alitokomea pasipojulikana na hadi leo haifahamiki ‘shujaa’ huyo alizikwa wapi.

Mamilioni ya wazalendo kusini mwa Tanzania walikufa kwa njaa, maradhi na kukosa makazi baada ya vita hii. Wakoloni wa Kijerumani waliteketeza mashamba yao, mifugo na nyumba na kuhakikisha wanavunja misingi yote ya kiuchumi kama mbinu ya kujihami dhidi ya ‘maasi’ mengine.’Unaweza kubofya hapa ili kuisoma historia hii kwa undani
Vita ya Majimaji: Historia iliyopotoshwa Na Evaristy Masuha Alhamisi, Agost 21, 2008

‘Leo napenda kuchimba zaidi ukweli huo huku nikijarijbu kutoa ukweli mwingine ambao utathibitisha historia hii huku nikiendelea kuwakumbusha Watanzania ambao watakuwa aidha wamesahau au hawakupata nafasi nzuri ya kuijua vita hiyo iliyokuja kujulikana kama “Vita ya Majimaji”.

Vita hiyo ilianza Julai mwaka 1905. Pigano la mwisho lilifanyika katika maeneo ya mpaka wa Tunduru na Masasi katika Kijiji cha Lusesule.

Mwaka 1907 wakati vita hiyo iliyokuwa kati ya serikali ya Wajerumani na Waafrika waliochoshwa na utawala wa suluba ikiendelea, Waafrika ambao walikuwa ni muungano wa makabila ya kusini hadi pwani ya Tanganyika, walikuwa wakipiga mishale na mikuki yao huku wakitamka neno ‘mashe’.

Neno hilo lipo kwenye lugha ya Kimatumbi ambalo tafsiri ya Kiswahili, ni ‘maji’, kama walivyoelekezwa na kiongozi wao hayati Kinjekitile Ngwale. Hiyo ndiyo iliyokuja kuzaa jina la ‘majimaji’.

Mwisho wa vita, Waafrika walishindwa vibaya na wengi wao kuuawa. Hapo ndipo historia ikaja kumtambua Kinjekitile kama kiongozi wa vita aliyewaahidi askari wake ushindi kutoka kwenye dawa aliyoamini ingeweza kubadilisha risasi kuwa maji, kitu ambacho hakikuwa kweli.

Historia hiyo tuliipokea na ndiyo tunayowafundisha vijana wetu na inatamka wazi kwamba dawa haikuwa kweli, kwani hakuna risasi hata moja iliyogeuka kuwa maji na matokeo yake Waafrika wengi walipoteza uhai wao.

Hapo ndipo nakosoa historia hiyo kulingana na mlolongo wa matukio yaliyofuatia hadi mwisho wa vita hiyo ambayo mwanzo ilikuwa ya ushindi mkubwa kwa Waafrika.

Historia hii ina tuambia kuwa Vita ya Majimaji ilianza mwaka 1905 Julai na mwezi mmoja baadaye yaani Agosti 24, mwaka 1905 Kinjekitile alinyongwa katika Kijiji cha Mhoro, Rufiji.
Tangu hapo wapiganaji wa Kiafrika wakaendelea kupigana bila kiongozi wao hadi Januari 1907.

Kwa mtazamo kama huo, tunaweza kupata picha ambayo itatufikisha katika ukweli wa historia ambayo walio kuwa na jukumu au uwezo wa kuhifadhi historia hiyo walilifanya makusudi kabisa ili tuamini kile walichokitaka wao.

Mwanzo wa Vita ya Majimaji huko Umatumbini ilikuwa ni mwendelezo wa vita ya muda mrefu kati ya utawala wa Wajerumani na Wamatumbi ambao walikuwa wamechoka kabisa kutawaliwa.

Hiyo ilitokana na Wajerumani walioingia kama marafiki, kugeuka kuwa wakatiili. Waafrika walichukizwa na kitendo cha kufanyishwa kazi katika mashamba ya Wajerumani kutwa nzima bila malipo.

Hali hiyo ilijenga chuki kati ya Waafrika na Wajerumani, hivyo Wamatumbi walianzisha vita iliyokuwa ya Mzungu na Mwafrika popote pale walipokuwa wakikutana.

Hali hiyo ilishtukiwa na Wajerumani na hivyo wakaamuru Wamatumbi wote kuepukana na asili yao ambayo ilikuwa ni kutembea na fimbo au mkongojo kwani ilikuja kugundulika kwamba, mikongoja hiyo ndiyo ilikuwa ikigeuka silaha dhidi ya Wajerumani.

Hiyo ilikuwa mwaka 1896, baada ya serikali ya kikoloni kuweka mkazo na sheria kali dhidi ya Mmatumbi yeyote anayepatikana akitembea na aina yoyote ya mti. Mwaka 1898, Wamatumbi wakagundua mbinu nyingine ambapo sasa maboga waliyokuwa wakilima zaidi kugeuka kuwa silaha.

Wamatumbi ambao kwa asili walikuwa watu jasiri sana, walianza kupambana na kila Mzungu waliyekutana naye kwa kumponda kwa boga. Vita hiyo ambayo inajulikana kwa Kimatumbi kama ‘Ngondo ya Mayawa’, yaani vita ya maboga.

Staili hiyo iliwashitua Wajerumani ambao sasa walianza kupambana na Wamatumbi kwa mtutu wa bunduki pamoja na sheria za kufungwa na wengine kuhukumiwa kunyongwa. Hapo tena Mmatumbi akawa amekubali kushindwa.

Kwa mtiririko wa matukio kama hayo ambayo sasa yalielekea kuwakatisha tamaa Wamatumbi, ndipo mzee hodari na mganga maarufu sana kwa ukanda huo, mganga aliyekuwa na mifugo mbalimbali nyumbani kwake, ikiwamo nyoka na samba, alisimama na kuwaahidi Wamatumbi kuingia katika vita aliyoiita vita ya ushindi.

Mzee huyu ambaye vitabu vya historia vinamtambua kama Kinjekitile, ukweli halisi wa jina lake aliitwa Kinjeketile, yaani kimeniitikia kwa lugha ya Kimatumbi.

Kwa mjibu wa imani ya Wamatumbi, mzee Kinjekitile aliyewarejesha Wamatumbi katika roho ya ujasiri kutoka katika roho ya kukata tamaa, alizama ndani ya Mto Rufiji na kuibuka baada ya siku mbili, akiwa na mizizi ya dawa hiyo. Hiyo ilikuwa mwaka 1903.’
 
Bana wee usituchoshe bana!! hata km alikuwa muongo lkn aliwatesa wakoloni safi sana miaka yooote hiyo! vita tuuuu!! huoni kuwa aliwaendesha wazungu?? hivi mim....wa mingine ikoje bana ? yaani anachukia sana kumponda huyu shujaa!

ungekuwa karibu heeee!! tatizo lako unadhani wazungu watakupenda
 
At least alijaribu kupingana na watawala ambao walikuwa juu sana kiuwezo, tafauti na wengine ambao hawakunyanyua hata kidole kuwasema wakoloni.

Muacheni mzee Kinje alale salama huko aliko, musimuhukumu kwa yaliyoko sasa hivi.
 
Kinjekitile/Kinjeketile ni mtu muhimu kwenye Vita vya maji maji japo historia yake inahitaji utafiti zaidi.
 
Kinjekitile/Kinjeketile ni mtu muhimu kwenye Vita vya maji maji japo historia yake inahitaji utafiti zaidi.
Naam! Nadhani kuna kilichofichwa. Na walioiandika hii historia ni wazungu waliopigana nae, kwa tafiti yangu ndogo sana nimegundua mengi sana nikiwa kilwa vijiji vya kibata, ali mchumo, kivinje n.k
 
Leo katika kupekua kwangu mtandaoni, nimekutana na historia mbili tofauti zinazomzungumzia Kinjekitile. Kilichonivutia hadi kuamua kuwashirkikisha wasomaji wa kibaraza hiki ili tutafakari kwa pamoja ni kutokana na kupingana kwa historia hizo.

Wakati historia moja ikihoji kuwa Kinjekitile alikuwa shujaa au mshirikina? ambayo iliandikwa na mwandishi Aloyce Menda katika gazeti la Tanzania Daima la Ijumaa, Septemba 21,2006, nyingine ilikuwa ikidai kuwa historia yake imepotoshwa, ambayo nayo iliandikwa na mwandishi Evaristy Masuha katika gazeti hilo hilo la Tanzania Daima la Alhamisi, Agosti 21, 2008.

Kwa historia hizo mbili kunaonekana kuwa na walakini na ni vyema historia hii ikawekwa sawa kwa manufaa ya vizazi vijavyo, la sivyo tutajikuta tukiwa tumepoteza kumbukumbu hii muhimu kwa vizazi vyetu.

Naomba tuwekane sawa katika swala hili, Je ni yupi yuko sahihi kati ya waandishi hawa wawili?

>BOFYA HAPA KUANGALIA WAPIGANAJI WA VITA VYA MAJI MAJI

***************************************

Na Aloyce Menda KINJEKITILE - Jemedari shujaa kweli au mshirikina laghai tu?
'Wakoloni wa Kijerumani waliita Vita ya Majimaji kuwa ni uasi wa Majimaji au Majimaji Rebellion kwa Kiingereza. Kwa Wakoloni, Kinjekitile alikuwa mhaini aliyekuwa anapinga utawala halali. Kwa dhana hiyo, Kinjekitile alikuwa shujaa kwa kupigania uhuru wa watu waliokuwa chini ya ukoloni.

Lakini kwa kutazama kwa kina mbinu za ukombozi alizotumia kupigania huo uhuru, sioni ushujaa wake. Vitabu vya historia vilivyoandikwa na wakoloni na hata vya wazalendo vinaonyesha wazi kwamba Kinjekitile alilaghai mamilioni ya watu wasioelimika, kwamba risasi za moto kutoka katika magobore ya askari wa Kijerumani zinaweza kugeuzwa maji na kuishia kulowesha tu miili yao bila madhara yoyote.

Kinjekitile alilaghai watu kwamba yeye anafahamu sayansi ya kijadi itakayotumiwa na ‘watu wake’ katika vita dhidi ya Wajerumani na kushinda. Sayansi yenyewe aliifundisha yeye mwenyewe kilaghai na kuisambaza kutoka Kilwa hadi Songea.

Watu wengi wakapotoshwa na kuamini kwamba risasi za moto zitageuka maji katika vita, kasha wakahamasishwa kuanzisha vita bila kujiandaa kwa mbinu nyingine za ziada! Silaha zao za jadi zilikuwa ni mawe, marungu, mundu, pinde, mishale na mikuki butu. Hatari iliyoje hiyo!

Kinjekitile mwenyewe hakwenda mstari wa mbele katika vita halisi, wala hakudiriki kusitisha mapambano alipoona maelfu ya ‘watu wake’ wakiteketezwa kwa risasi. Badala yake, alikaa mafichoni huku akiendelea kutuma wasaidizi wake kushawishi watu waamini ulaghai wake, na kwamba waliokuwa wanakufa kwa risasi hizo ni wale tu ambao hawakutimiza vyema masharti ya ‘sayansi’ yake aliyowapa.

‘Shujaa’ Kinjekitile alikuwa tapeli hatari sana kiasi kwamba, hakuwa na himaya maalumu ya kuishi, tofauti na walivyokuwa kina Chifu Mkwawa, Mtemi Mirambo and Mangi Sina. Bila shaka alikuwa anafahamu fika kwamba siku moja ulaghai wake utafikia mwisho, ambapo watu wangemgeukia na kumtoa roho yake, hivyo alijihami kabla kwa kuishi mafichoni kama afanyavyo gaidi Osama bin Laden hivi sasa.

Vita ilipokaribia mwisho wake kwa wazalendo wengi kufa kama sisimizi, Kinjekitile alitokomea pasipojulikana na hadi leo haifahamiki ‘shujaa’ huyo alizikwa wapi.

Mamilioni ya wazalendo kusini mwa Tanzania walikufa kwa njaa, maradhi na kukosa makazi baada ya vita hii. Wakoloni wa Kijerumani waliteketeza mashamba yao, mifugo na nyumba na kuhakikisha wanavunja misingi yote ya kiuchumi kama mbinu ya kujihami dhidi ya ‘maasi’ mengine.’Unaweza kubofya hapa ili kuisoma historia hii kwa undani
Vita ya Majimaji: Historia iliyopotoshwa Na Evaristy Masuha Alhamisi, Agost 21, 2008

‘Leo napenda kuchimba zaidi ukweli huo huku nikijarijbu kutoa ukweli mwingine ambao utathibitisha historia hii huku nikiendelea kuwakumbusha Watanzania ambao watakuwa aidha wamesahau au hawakupata nafasi nzuri ya kuijua vita hiyo iliyokuja kujulikana kama “Vita ya Majimaji”.

Vita hiyo ilianza Julai mwaka 1905. Pigano la mwisho lilifanyika katika maeneo ya mpaka wa Tunduru na Masasi katika Kijiji cha Lusesule.

Mwaka 1907 wakati vita hiyo iliyokuwa kati ya serikali ya Wajerumani na Waafrika waliochoshwa na utawala wa suluba ikiendelea, Waafrika ambao walikuwa ni muungano wa makabila ya kusini hadi pwani ya Tanganyika, walikuwa wakipiga mishale na mikuki yao huku wakitamka neno ‘mashe’.

Neno hilo lipo kwenye lugha ya Kimatumbi ambalo tafsiri ya Kiswahili, ni ‘maji’, kama walivyoelekezwa na kiongozi wao hayati Kinjekitile Ngwale. Hiyo ndiyo iliyokuja kuzaa jina la ‘majimaji’.

Mwisho wa vita, Waafrika walishindwa vibaya na wengi wao kuuawa. Hapo ndipo historia ikaja kumtambua Kinjekitile kama kiongozi wa vita aliyewaahidi askari wake ushindi kutoka kwenye dawa aliyoamini ingeweza kubadilisha risasi kuwa maji, kitu ambacho hakikuwa kweli.

Historia hiyo tuliipokea na ndiyo tunayowafundisha vijana wetu na inatamka wazi kwamba dawa haikuwa kweli, kwani hakuna risasi hata moja iliyogeuka kuwa maji na matokeo yake Waafrika wengi walipoteza uhai wao.

Hapo ndipo nakosoa historia hiyo kulingana na mlolongo wa matukio yaliyofuatia hadi mwisho wa vita hiyo ambayo mwanzo ilikuwa ya ushindi mkubwa kwa Waafrika.

Historia hii ina tuambia kuwa Vita ya Majimaji ilianza mwaka 1905 Julai na mwezi mmoja baadaye yaani Agosti 24, mwaka 1905 Kinjekitile alinyongwa katika Kijiji cha Mhoro, Rufiji.
Tangu hapo wapiganaji wa Kiafrika wakaendelea kupigana bila kiongozi wao hadi Januari 1907.

Kwa mtazamo kama huo, tunaweza kupata picha ambayo itatufikisha katika ukweli wa historia ambayo walio kuwa na jukumu au uwezo wa kuhifadhi historia hiyo walilifanya makusudi kabisa ili tuamini kile walichokitaka wao.

Mwanzo wa Vita ya Majimaji huko Umatumbini ilikuwa ni mwendelezo wa vita ya muda mrefu kati ya utawala wa Wajerumani na Wamatumbi ambao walikuwa wamechoka kabisa kutawaliwa.

Hiyo ilitokana na Wajerumani walioingia kama marafiki, kugeuka kuwa wakatiili. Waafrika walichukizwa na kitendo cha kufanyishwa kazi katika mashamba ya Wajerumani kutwa nzima bila malipo.

Hali hiyo ilijenga chuki kati ya Waafrika na Wajerumani, hivyo Wamatumbi walianzisha vita iliyokuwa ya Mzungu na Mwafrika popote pale walipokuwa wakikutana.

Hali hiyo ilishtukiwa na Wajerumani na hivyo wakaamuru Wamatumbi wote kuepukana na asili yao ambayo ilikuwa ni kutembea na fimbo au mkongojo kwani ilikuja kugundulika kwamba, mikongoja hiyo ndiyo ilikuwa ikigeuka silaha dhidi ya Wajerumani.

Hiyo ilikuwa mwaka 1896, baada ya serikali ya kikoloni kuweka mkazo na sheria kali dhidi ya Mmatumbi yeyote anayepatikana akitembea na aina yoyote ya mti. Mwaka 1898, Wamatumbi wakagundua mbinu nyingine ambapo sasa maboga waliyokuwa wakilima zaidi kugeuka kuwa silaha.

Wamatumbi ambao kwa asili walikuwa watu jasiri sana, walianza kupambana na kila Mzungu waliyekutana naye kwa kumponda kwa boga. Vita hiyo ambayo inajulikana kwa Kimatumbi kama ‘Ngondo ya Mayawa’, yaani vita ya maboga.

Staili hiyo iliwashitua Wajerumani ambao sasa walianza kupambana na Wamatumbi kwa mtutu wa bunduki pamoja na sheria za kufungwa na wengine kuhukumiwa kunyongwa. Hapo tena Mmatumbi akawa amekubali kushindwa.

Kwa mtiririko wa matukio kama hayo ambayo sasa yalielekea kuwakatisha tamaa Wamatumbi, ndipo mzee hodari na mganga maarufu sana kwa ukanda huo, mganga aliyekuwa na mifugo mbalimbali nyumbani kwake, ikiwamo nyoka na samba, alisimama na kuwaahidi Wamatumbi kuingia katika vita aliyoiita vita ya ushindi.

Mzee huyu ambaye vitabu vya historia vinamtambua kama Kinjekitile, ukweli halisi wa jina lake aliitwa Kinjeketile, yaani kimeniitikia kwa lugha ya Kimatumbi.

Kwa mjibu wa imani ya Wamatumbi, mzee Kinjekitile aliyewarejesha Wamatumbi katika roho ya ujasiri kutoka katika roho ya kukata tamaa, alizama ndani ya Mto Rufiji na kuibuka baada ya siku mbili, akiwa na mizizi ya dawa hiyo. Hiyo ilikuwa mwaka 1903.’
Huwezi kumwita laghai maana aliamini alichosema. Kwa macho ya leo unaweza kusema alikuwa mtu bila elimu. Ukitaka kudharau elimu ya jadi utamwita mjinga, lakini kamwe laghai. Mimi ni nisingesema hivi. Alikuwa na ujumbe wake, alikuwa na maono yake (sijui alivuta au kutafuna nini?).
Wengine walipokea wito wake na kufanya mambo yao, maana yeye mwenyewe alinyongwa tayari kwenye siku za kwanza. Matokeo yalikuwa mabaya. Makadirio ya vifo ni watu lakhi waliangamizwa, hasa kutokana na njaa na magonjwa.
Wajerumani waliona baadaye kwamba walifanya kosa lililosababisha upinzani, walibadilisha mitindo ya utawala na kupunguza ukali. (maana Majimaji ilitokea sambamba na vita ya Waherero katika koloni ya Afrika Kusini-Magharibi = Namibia)

Lakini kijeshi upinzani wa Majimaji haukuwa kweli hatari kwao. Maana wengine kama Wahehe na Wasangu na Wanyamwezi na Wachagga ama hawakuelewa watu wa kusini-mashariki walifanya nini, au hawakuona sababu ya kujiunga nao, au walikumbuka bado bombomu ya Wajerumani (ambazo wat wa kusini-magharibi wakiona mara ya kwanza). Kilele cha mapigano kilitokea Mahenge ambako Wajerumani wanne, askari Wasudani 60 pamoja na wasaidizi Wabena 200 au 300 waliweza kujitetea kirahisi kwa sababu walikuwa na bombomu 2 na wapiganaji wa Majimaji walishambulia katika foleni bila kujificha, wakiamini nguvu ya maji wakafa mamia.
 
Huwezi kumwita laghai maana aliamini alichosema. Kwa macho ya leo unaweza kusema alikuwa mtu bila elimu. Ukitaka kudharau elimu ya jadi utamwita mjinga, lakini kamwe laghai. Mimi ni nisingesema hivi. Alikuwa na ujumbe wake, alikuwa na maono yake (sijui alivuta au kutafuna nini?).
Wengine walipokea wito wake na kufanya mambo yao, maana yeye mwenyewe alinyongwa tayari kwenye siku za kwanza. Matokeo yalikuwa mabaya. Makadirio ya vifo ni watu lakhi waliangamizwa, hasa kutokana na njaa na magonjwa.
Wajerumani waliona baadaye kwamba walifanya kosa lililosababisha upinzani, walibadilisha mitindo ya utawala na kupunguza ukali. (maana Majimaji ilitokea sambamba na vita ya Waherero katika koloni ya Afrika Kusini-Magharibi = Namibia)

Lakini kijeshi upinzani wa Majimaji haukuwa kweli hatari kwao. Maana wengine kama Wahehe na Wasangu na Wanyamwezi na Wachagga ama hawakuelewa watu wa kusini-mashariki walifanya nini, au hawakuona sababu ya kujiunga nao, au walikumbuka bado bombomu ya Wajerumani (ambazo wat wa kusini-magharibi wakiona mara ya kwanza). Kilele cha mapigano kilitokea Mahenge ambako Wajerumani wanne, askari Wasudani 60 pamoja na wasaidizi Wabena 200 au 300 waliweza kujitetea kirahisi kwa sababu walikuwa na bombomu 2 na wapiganaji wa Majimaji walishambulia katika foleni bila kujificha, wakiamini nguvu ya maji wakafa mamia.

Sawa mkuu
 
Back
Top Bottom