Pionaire
JF-Expert Member
- Oct 24, 2012
- 1,603
- 1,135
MANCHESTER DERBY,
Ni mechi za mpira wa miguu zinazowakutanisha timu kuu mbili nchini Uingereza ambao ni Watani wa Jadi kutokea jiji la MANCHESTER upande wa GREATER MANCHESTER, Nao ni MANCHESTER UNITED(Man United) na MANCHESTER CITY(Man City).
Viwanja vyao vya mchezo ni ETIHAD(Kwa Man City...unaochukua idadi ya watazamaji 53,400 ) na OLD TRAFFORD(Kwa Man United...unaochukua idadi ya watazamaji 74,310) na Vikiwa vimetenganishwa na umbali unaokaribia miles.4 sawa na 6.4 Km tu.
HISTORIA ZAO,
Man United ilianzishwa mnamo mwaka 1878 ikitambulika kwa jina la NewTon Health LYR F.C na baadae kubadilishwa jina lake na kuitwa Rasmi Manchester United F.C mnamo mwaka 1902 na mashabiki wa timu hiyo wakitambulika kama THE RED DEVILS(Mashetani wekundu).
Man City ilianzishwa mnamo mwaka 1880 ikitambulika kwa jina la St.Mark's(West Gorton) F.C, kisha ilibadilishwa ikawa Ardwick Association Football Club mwaka 1887 na baadae kubadilishwa jina lake na kuitwa Rasmi Manchester City F.C mnamo mwaka 1894 na mashabiki wa timu hiyo wakitambulika kama THE CITYZENS(Wana nchi) na SKY BLUES(Wana Anga).
UHUSIANO WAO NA JIJI LA MANCHESTER.
Timu zote mbili ni wawakilishi sahihi kutokea jiji la manchester kwa maana ya kwamba zote zinabeba historia ya jiji hilo...KWA KUWA MANCHESTER TOKEA HAPO KALE NI MJI WA PILI NYUMA YA LIVERPOOL(Bandari yake iliyoanzishwa mwaka.1701 kwa maagizo ya King.James wa Britain na kufa 1710 kisha kufufuliwa upya mnamo mwaka 1846) WENYE BANDARI KONGWE PALE UINGEREZA ILIYOANZISHWA 1.JAN 1894(Mwaka sawa na uliyopo kwenye Badge/Logo ya Man City).
Uwepo wa meli katika logo zote za vilabu hivii unawakilisha historia ya Bandari hiyo na Mlango wake mkuu wa kuingilia kutokea Baharini ukiweka umbali wa mile.36(km.58) tu kukuta upande wa magharibi mwa jiji hilo, hivyo kubadili taswira ya jiji la manchester kutoka kuwa Landlocked City na kuwa Port City.
Man city ikaenda mbali zaidi kwa kuiwakilisha mito mikuu mitatu iliyopo jijini manchester ijulikanayo kwa majina kama Irwell, Irk na Medlock kupitia mistari mitatu ya blue mpauko kwenye sehemu ya chini iliyo kwenye muundo wa diagonal katika ile bahari iliyobeba Meli. Kwenye Logo yao.
Kwa maana hiyo hii bandari ndo ilipelekea mapinduzi makubwa ya uchumi wa viwanda nchini uingereza yaliyoanzia Jijini manchester na tokea apo bandari hii imekuwa ni historia kubwa sana kwa Wakazi wa Jiji Hilo kwa Vizazi na Vizazi, na ata Wakazi wengi ambao ndo Mashabiki/Supporters/Wanachama wa hivyo vilabu walitokana na familia za wafanya kazi wa bandari hiyo na viwanda vilivyojaa jijini humo.
MAFANIKIO YAO KATIKA SOKA.
Man United.
Katika mafanikio ya soka la Mataji nchini Uingereza na ulaya Man united yupo mbele ya Man City kwa jumla ya vikombe.69...zikiwemo Ligi.20, kutokana na uwekezaji uliowekwa mapema tokea miaka ya 70's...na kupelekea timu iyo kutwaa mataji ya kutosha ndani na nje ya uingereza hasa katika miaka ya 80's chini ya mkufunzi mkuu Sir.Fergie.
Man City
Uku Man City wakiwa wanastruggle kwa kupanda ligi kuu na kushuka mara.4(Mwaka.1981, 1983, 1987 na 1998) na mara ya mwisho City kushuka daraja kutoka ligi kuu na kwenda championship ilikuwa ni 1998 na akaja kupanda tena mwaka.2001 na anzia hapo ndipo safari yao ya uhakika ya ligi kuu Uingereza ilipoanzia kwa kutoshuka tena daraja hadi kufikia mwaka.2008 timu iliponunuliwa na Sheikh Mansour bin Zayed Al Nahyan kupitia shirika lake mama la Abu Dhabi United Group kwa kiasi cha £210million...inayomiliki kampuni kubwa ya ndege ya ETIHAD AIRWAYS, CITY FOOTBALL GROUP(CFG).LTD...n.k
Hapo ndipo City ikabadilika kutoka kuwa timu ya kawaida Ligi kuu na kuwa timu kubwa uingereza na kutawala soka la nchini uingereza baada ya miaka miwili ya umiliki huo kwa takribani miaka.10 iliyopita hadi apa walipo leo hii. Hii imewapa jumla ya vikombe 14 katika kipindi cha miaka 14 ya umiliki mpya wa mansour...yakiwemo makombe 6 ya ligi wakikamilisha jumla ya makombe yao yote kuwa 36 kabatini mwao.
USHINDANI WAO KILA WANAPOKUTANA.
Derby ya kwanza baina ya Man United na Man City ilipigwa mwaka 1881 Nov.12...ambapo Newton Heath LYR(ambayo ndo Man United ya Sasa) wakishinda bao 3 bila dhidi ya St.Marks(ambayo ndo Man City kwa sasa). Hadi kufikia mchezo Ambao utapigwa apo kesho( Oct.2.2022) Majira ya saa.10 Jioni Kwenye dimba la etihad utakuwa ni mchezo wa derby wa 188 kati yao.
Na katika michezo ya jumla 187 hiyo Man united akiwa imeshinda jumla ya michezo.77 na kupoteza 57 huku Man City akiwa ameshinda jumla ya michezo.57 nakupoteza michezo..77, na wakitoka Sare ya michezo 53(KATIKA MICHEZO YOTE ZIKIWEMO CHARITY NA FRIENDLY MATCHES).
Na katika michezo ya pamoja Ya ushindani pekee ni jumla ya michezo.164, City wakiwa wameshinda michezo.51 na kupoteza.65 uku United ikishinda michezo.65 na kupoteza.51 na wote wakitoa sare ya michezo.48, Na Cha kushangaza zaidi wamefungana idadi sawa jumla ya magoli.227 na kuruhusu Idadi sawa jumla ya Magoli.227.
Na Tokea waanze kukutana vipigo vikubwa na vya aibu(yaani Kuanzia goli.5+) kuwahi kutokea kati yao Man United kapigwa vingi mara.4 huku city akiwa kapigwa mara.1 tu kama muonavyo hapo.
Swali Je iyo kesho ni nani ataongeza USHINDI UPANDE WAKE???
Hatimaye Man City wameongeza ushindi mwingine kwenye Cabinet yao na kupelekea ushindi wa jumla kuwa michezo.58 katika MANCHESTER DERBY YA 188.
Mchezo uliopigwa Oct.2.2022 ETIHAD, Na City kuibuka na ushindi wa Bao: 6-3 dhidi ya United.
Ni mechi za mpira wa miguu zinazowakutanisha timu kuu mbili nchini Uingereza ambao ni Watani wa Jadi kutokea jiji la MANCHESTER upande wa GREATER MANCHESTER, Nao ni MANCHESTER UNITED(Man United) na MANCHESTER CITY(Man City).
Viwanja vyao vya mchezo ni ETIHAD(Kwa Man City...unaochukua idadi ya watazamaji 53,400 ) na OLD TRAFFORD(Kwa Man United...unaochukua idadi ya watazamaji 74,310) na Vikiwa vimetenganishwa na umbali unaokaribia miles.4 sawa na 6.4 Km tu.
HISTORIA ZAO,
Man United ilianzishwa mnamo mwaka 1878 ikitambulika kwa jina la NewTon Health LYR F.C na baadae kubadilishwa jina lake na kuitwa Rasmi Manchester United F.C mnamo mwaka 1902 na mashabiki wa timu hiyo wakitambulika kama THE RED DEVILS(Mashetani wekundu).
Man City ilianzishwa mnamo mwaka 1880 ikitambulika kwa jina la St.Mark's(West Gorton) F.C, kisha ilibadilishwa ikawa Ardwick Association Football Club mwaka 1887 na baadae kubadilishwa jina lake na kuitwa Rasmi Manchester City F.C mnamo mwaka 1894 na mashabiki wa timu hiyo wakitambulika kama THE CITYZENS(Wana nchi) na SKY BLUES(Wana Anga).
UHUSIANO WAO NA JIJI LA MANCHESTER.
Timu zote mbili ni wawakilishi sahihi kutokea jiji la manchester kwa maana ya kwamba zote zinabeba historia ya jiji hilo...KWA KUWA MANCHESTER TOKEA HAPO KALE NI MJI WA PILI NYUMA YA LIVERPOOL(Bandari yake iliyoanzishwa mwaka.1701 kwa maagizo ya King.James wa Britain na kufa 1710 kisha kufufuliwa upya mnamo mwaka 1846) WENYE BANDARI KONGWE PALE UINGEREZA ILIYOANZISHWA 1.JAN 1894(Mwaka sawa na uliyopo kwenye Badge/Logo ya Man City).
Uwepo wa meli katika logo zote za vilabu hivii unawakilisha historia ya Bandari hiyo na Mlango wake mkuu wa kuingilia kutokea Baharini ukiweka umbali wa mile.36(km.58) tu kukuta upande wa magharibi mwa jiji hilo, hivyo kubadili taswira ya jiji la manchester kutoka kuwa Landlocked City na kuwa Port City.
Man city ikaenda mbali zaidi kwa kuiwakilisha mito mikuu mitatu iliyopo jijini manchester ijulikanayo kwa majina kama Irwell, Irk na Medlock kupitia mistari mitatu ya blue mpauko kwenye sehemu ya chini iliyo kwenye muundo wa diagonal katika ile bahari iliyobeba Meli. Kwenye Logo yao.
Kwa maana hiyo hii bandari ndo ilipelekea mapinduzi makubwa ya uchumi wa viwanda nchini uingereza yaliyoanzia Jijini manchester na tokea apo bandari hii imekuwa ni historia kubwa sana kwa Wakazi wa Jiji Hilo kwa Vizazi na Vizazi, na ata Wakazi wengi ambao ndo Mashabiki/Supporters/Wanachama wa hivyo vilabu walitokana na familia za wafanya kazi wa bandari hiyo na viwanda vilivyojaa jijini humo.
MAFANIKIO YAO KATIKA SOKA.
Man United.
Katika mafanikio ya soka la Mataji nchini Uingereza na ulaya Man united yupo mbele ya Man City kwa jumla ya vikombe.69...zikiwemo Ligi.20, kutokana na uwekezaji uliowekwa mapema tokea miaka ya 70's...na kupelekea timu iyo kutwaa mataji ya kutosha ndani na nje ya uingereza hasa katika miaka ya 80's chini ya mkufunzi mkuu Sir.Fergie.
Man City
Uku Man City wakiwa wanastruggle kwa kupanda ligi kuu na kushuka mara.4(Mwaka.1981, 1983, 1987 na 1998) na mara ya mwisho City kushuka daraja kutoka ligi kuu na kwenda championship ilikuwa ni 1998 na akaja kupanda tena mwaka.2001 na anzia hapo ndipo safari yao ya uhakika ya ligi kuu Uingereza ilipoanzia kwa kutoshuka tena daraja hadi kufikia mwaka.2008 timu iliponunuliwa na Sheikh Mansour bin Zayed Al Nahyan kupitia shirika lake mama la Abu Dhabi United Group kwa kiasi cha £210million...inayomiliki kampuni kubwa ya ndege ya ETIHAD AIRWAYS, CITY FOOTBALL GROUP(CFG).LTD...n.k
Hapo ndipo City ikabadilika kutoka kuwa timu ya kawaida Ligi kuu na kuwa timu kubwa uingereza na kutawala soka la nchini uingereza baada ya miaka miwili ya umiliki huo kwa takribani miaka.10 iliyopita hadi apa walipo leo hii. Hii imewapa jumla ya vikombe 14 katika kipindi cha miaka 14 ya umiliki mpya wa mansour...yakiwemo makombe 6 ya ligi wakikamilisha jumla ya makombe yao yote kuwa 36 kabatini mwao.
USHINDANI WAO KILA WANAPOKUTANA.
Derby ya kwanza baina ya Man United na Man City ilipigwa mwaka 1881 Nov.12...ambapo Newton Heath LYR(ambayo ndo Man United ya Sasa) wakishinda bao 3 bila dhidi ya St.Marks(ambayo ndo Man City kwa sasa). Hadi kufikia mchezo Ambao utapigwa apo kesho( Oct.2.2022) Majira ya saa.10 Jioni Kwenye dimba la etihad utakuwa ni mchezo wa derby wa 188 kati yao.
Na katika michezo ya jumla 187 hiyo Man united akiwa imeshinda jumla ya michezo.77 na kupoteza 57 huku Man City akiwa ameshinda jumla ya michezo.57 nakupoteza michezo..77, na wakitoka Sare ya michezo 53(KATIKA MICHEZO YOTE ZIKIWEMO CHARITY NA FRIENDLY MATCHES).
Na katika michezo ya pamoja Ya ushindani pekee ni jumla ya michezo.164, City wakiwa wameshinda michezo.51 na kupoteza.65 uku United ikishinda michezo.65 na kupoteza.51 na wote wakitoa sare ya michezo.48, Na Cha kushangaza zaidi wamefungana idadi sawa jumla ya magoli.227 na kuruhusu Idadi sawa jumla ya Magoli.227.
Na Tokea waanze kukutana vipigo vikubwa na vya aibu(yaani Kuanzia goli.5+) kuwahi kutokea kati yao Man United kapigwa vingi mara.4 huku city akiwa kapigwa mara.1 tu kama muonavyo hapo.
Swali Je iyo kesho ni nani ataongeza USHINDI UPANDE WAKE???
Hatimaye Man City wameongeza ushindi mwingine kwenye Cabinet yao na kupelekea ushindi wa jumla kuwa michezo.58 katika MANCHESTER DERBY YA 188.
Mchezo uliopigwa Oct.2.2022 ETIHAD, Na City kuibuka na ushindi wa Bao: 6-3 dhidi ya United.